Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa ameziagiza Halmashauri kutenga fedha kwaajili ya kuwanunulia vifaa watu wenye ulemavu na kuwajengea miundombinu rafiki itakayowawezesha kutekeleza shughuli zao bila bughudha.
Waziri Mkuu ametoa Rai hiyo leo tarehe 13 Juni,2025 alipomwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan wakati wa Maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Kimataifa ya kukuza uelewa kuhusu Ualbino yaliyofanyika katika uwanja wa Mwanga Community Centre Mkoani Kigoma.
Amesema anaamini Halmashauri hazitashindwa kuwahudumia watu wenye ulemavu ambao wako kwenye maeneo yao kwakuwa idadi yao si kubwa na kwamba suala la kuwanunulia vifaa kama vile Baiskeli za kutembelea pamoja na vifaa vingine ni jambo linalowezekana.
Aidha katika Maadhimisho hayo yaliyohudhuriwa pia na Waziri wa nchi ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Ajira na Watu wenye ulemavu Mhe.Ridhiwan Kikwete, Waziri Mkuu amezindua programu janja ya ‘Albino Mobile App’ ambayo itawezesha kufanya usajili na ukusanyaji wa taarifa za watu wenye ualbino kwa njia ya kidigitali.
Maadhimisho haya hufanyika kila ifikapo tarehe 13 Juni ambapo mara hii ni ya 10 yakiwa yamebeba Kaulimbiu isemayo "Kushiriki katika Uchaguzi ni Haki,kuchagua na kuchaguliwa,linda haki za watu wenye Ualbino.
Manispaa ya Kigoma Ujiji
Sanduku la Posta: S.L.P 44
Simu: +255 28 2802535
Namba ya Simu: +255765660847
Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz
Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa