• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

HATUA ZILIZOCHUKULIWA NA SERIKALI KUJAA KWA MAJI KATUBUKA. Social Services

Posted on: April 24th, 2025

Na Mwandishi Wetu

Hali ya kujaa kwa maji na kuathiri Wananchi wanaoishi jirani na Bwawa la Katubuka limeibuka Leo katika Baraza la Madiwani la kupokea na kujadili taarifa za Kata Manispaa ya Kigoma/Ujiji lililoketi Leo April 24, 2025.


Suala hilo limejadiliwa mara baada ya Diwani wa Kata ya Katubuka Mhe. Moshi Mayengo kuwasilisha taarifa za Kata hiyo.  


Akizungumza katika Mkutano huo Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. David Rwazo amesema elimu imeendelea kutolewa kwa Wakazi wa maeneo hayo kuhama ili kuepuka kadhia ya ongezeko la maji kutokana na Mvua zinazoendelea kunyesha.  


Amesema  Serikali ikishirikiana na Wadau mbalimbali wa Maendeleo wakiwemo UNICEF na IOM (UN-Migration) wameshatoa Mahitaji ya kibinadamu kwa Wananchi wa eneo hilo kama vile Mchele, maharage, Sukari, Sabuni, dagaa magodoro, Shuka, na neti huku akisema Halmashauri imeomba Serikali kupitia Mradi wa TACTICS unaoendelea,  kujenga Km 4.36 hadi kwenye mtaro wa asili wa Mungonya unaoelekeza maji yake ziwani.



Amesema tayari Ofisi ya Mkurugenzi imetenga  eneo la kuhifadhi watu (Rescue area) katika Kata ya Katubuka  na kutenga Chumba cha darasa Shule ya Msingi Majengo ili kuwasaidia wanaokosa eneo la kujihifadhi.


Barabara zilizovamiwa na maji tayari zimefungwa, na  kukatwa kwa umeme katika eneo hilo huku akisema elimu imetolewa kwa Kamati za Maafa ngazi ya mtaa namna ya kukabiliana na kujikinga na magonjwa ya mlipuko.


Akizungumza katika kikao hicho Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini Mhe. Ngenda Kilumbe Ngenda amesema tayari Wataalamu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu wameshafika Manispaa ya Kigoma/Ujiji katika kuhakikisha Wananchi hao wanapata msaada wa kibinadamu mara baada ya kutoa hoja ya dharura kujadiliwa Bungeni na Serikali kutuma Wataalamu.


Zaidi bofya www.kigomaujijimc.go.tz

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • WAJASIRIAMALI WAENDELEA KUFIKIWA NA WATAALAMU KIGOMA UJIJI. Social services

    May 30, 2025
  • UGAWAJI WA VYANDARUA BURE UNAENDELEA KWENYE VITUO KIGOMA UJIJI. Health protection

    May 29, 2025
  • WAJASIRIAMALI KIGOMA UJIJI WATEMBELEWA NA WATAALAMU.

    May 28, 2025
  • RC ANDENGENYE AZINDUA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA MKOA WA KIGOMA. Malaria protection

    May 28, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa