• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

KAMATI YA SIASA YA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) WILAYA YA KIGOMA YAKAGUA UTEKELEZAJI WA ILANI MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI , YARIDHISHWA NA USIMAMIZI WA MIRADI, Political

Posted on: June 13th, 2021

Na Mwandishi Wetu

Kamati ya siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kigoma leo June 13, imefanya ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya chama hicho Manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa kipindi cha  mwaka mmoja July 2020 hadi June 2021 na kuridhishwa na miradi iliyotekelezwa


Ziara hiyo imefanyika ikiongozwa na Mwenyekiti wa Chama hicho wilaya Alhaji Yassin Mtalikwa ambapo wajumbe wa kamati hiyo wamepongeza ubora wa viwango wa miradi inayoendelea kujengwa chini ya usimamizi wa Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji

Katika ziara hiyo jumla ya miradi yenye zaidi ya thamani ya Fedha za Kitanzania Million mia saba (700,000,000/=) imekaguliwa huku Mwenyekiti huyo akipongeza usimamizi unaofanyika na Wataalamu kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo  


Mwenyekiti huyo akiwa katika Zahanati ya Rusimbi ambapo Ujenzi wa wodi ya wazazi unaendelea amewapongeza Wananchi wa Kata hiyo kwa kuunga juhudi ya ujenzi kwa kuchangia kiasi cha fedha za Kitanzania Million saba laki saba elfu sitini na moja na mia tano ( Tsh 7,761,500/=) huku Serikali ikitoa Kiasi cha million hamsini (Tsh 50,000,000/=) na kiasi cha Million kumi (Tsh 10,000,000/=) zikihitajika katika ukamilishaji wa Jengo hilo


Ameendelea kupongeza Wananchi wa Kata ya Katubuka kwa ujenzi wa msingi wa vyumba viwili vya madarasa  katika Shule ya Msingi Majengo na Serikali ikitoa kiasi cha fedha Million hamsini (Tsh 50,000,000/=) katika ukamilishaji wa vyumba hivyo huku akiwataka wakazi wote wa Manispaa hiyo kuendelea kuchangia nguvu kazi na fedha katika miradi inayotekelezwa katika maeneo yao


Miradi mingine iliyotekelezwa ikihusisha nguvu ya wananchi ni pamoja na  ujenzi wa vyumba viwili (2) vya madarasa na ofisi za walimu mbili (2) Shule ya Msingi Kabingo na Serikali ikitoa fedha za Kitanzania Million hamsini (Tsh 50,000,000/=) katika ukamilishaji wa ujenzi huo, Ujenzi wa Zahanati ya Buronge na Serikali ikitoa fedha za Kitanzania Million thelathini (Tsh 30,000,000/=) katika ukamilishaji wa Ujenzi huo

Akihitimisha ziara hiyo Mwenyekiti huyo amewataka Wataalamu kuendelea kusimamia miradi katika viwango vinavyotakiwa ili iweze kunufaisha wakazi wa wote wa Manispaa hiyo na  kuendelea kufanya kazi kwa kushirikiana na Chama Cha Mapinduzi kwa kupokea maoni na ushauri katika miradi mbalimbali



Naye kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Frednand Filimbi ameishukuru kamati ya Chama Cha Mapinduzi kwa kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali huku akisema Ofisi ya Mkurugenzi ikishirikiana na wataalamu itaendelea kusimamia miradi katika viwango bora na kuendelea kutatua kero za wananchi


Aidha  Miradi mingine iliyotembelewa ni pamoja na ukamilishaji wa maabara mbili (2) za masomo ya Sayansi shule ya sekondari Kichakachui wenye thamani ya fedha za Kitanzania Million sitini (Tsh 60,000,000/=), Ujenzi wa Bweni moja wenye thamani ya fedha za Kitanzania Million themanini (80,000,000/=) ujenzi wa madarasa mawili yenye thamani ya fedha za Kitanzania Million arobaini (Tsh 40,000,000/=) maabara mbili (2) yenye thamani ya fedha za Kitanzania Million sitini (Tsh 60,000,000/=) katika shule ya Sekondari Kasingirima, Ujenzi wa Bweni Shule ya Sekondari Buronge yenye thamani ya fedha za Kitanzania Million themanini (Tsh 80,000,000/=) ,Ujenzi wa Machinjio ya Ujiji Kisasa wenye thamani ya Fedha za Kitanzania Million mia moja na themanini na mbili (Tsh 182,913,668/=) na kutembelea kitalu cha miche ya Michikichi ya kisasa kilichopo eneo la Katosho





Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa