• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

KAMATI YA WILAYA YA MPANGO WA TAIFA WA KUTOKOMEZA UKATILI WANAWAKE NA WATOTO (MTAKUWWA) YAKUTANA KWA MARA YA KWANZA, YAWEKA MAAZIMIO TISA (9) YATAKAYOTEKELEZWA. DISTRIC COMMITTE OF MTAKUWWA MEETS FOR THE FIRST TIME,IMPOSES RESOLUTIONS

Posted on: December 7th, 2018


Kamati ya wilaya ya mpango wa Taifa wa kutokomeza ukatili wa wanawake na watoto (MTAKUWWA) kwa mara ya kwanza jana Desemba 5, ilikutana katika ukumbi mdogo wa halmashauri ya manispaa ya Kigoma Ujiji  kujadili na kuweka mikakati na maazimio ya kuhakikisha vitendo hivyo vinatoweka.

Akifungua kikao hicho kaimu mkurugenzi wa manispaa ya Kigoma Ujiji Ndugu. Berneth Ninalwo aliwataka wajumbe wote waliohudhulia kikao hicho kuhakikisha inawekwa mipango thabiti kukahakikisha vitendo hivyo vinatoweka na kuwa agenda ya kudumu katika kupinga vitendo vya ukatili kuanzia ngazi ya familia.

Katika kikao hicho wajumbe waliweza kusomewa majukumu ya kamati hiyo na katibu wa MTAKUWWA wilaya Bi. Agnes Sanga  ikiwa ni pamoja na kamati kutekeleza mpango kazi wa kitaifa wa kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto, na kuhamasisha na kutoa elimu juu ya kutokomeza ukatili wa wanawake na watoto.

katika kikao hicho mwenyekiti aliweza kukaribisha wajumbe na wadau mbali mbali kutoa taarifa namna wanavyofanya kazi katika kuhakikisha vitendo vya ukatili  wa wanawake na watoto vinatoweka katika wilaya na halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji.

Akitoa taarifa Afisa wa Polisi dawati la kupinga ukatili wa wanawake na watoto Bi. Mary Paul aliweza kueleza majukumu yanayotekelezwa na jeshi la Polisi ikiwa ni kupokea taarifa za ukatili mbali mbali ikiwa ni pamoja na ubakaji, kupigwa , kuchomwa moto kwa watu wanaofanya vitendo hivyo vya ukatili.

Aliendelea kutoa taarifa kuwa kwa mwaka huu mpaka sasa wamepokea kesi 20 za kubaka, kesi 1 ya kupapaswa kwa mtoto wa kike na dereva bajaji, kesi 15  za migogoro ya kifamilia ikiwemo kutelekezwa kwa wanawake na watoto na tayari zimeshafikishwa Mahakamani na dereva bajaji amehukumiwa miaka 5 jera, na hadi hivi sasa wanaendelea kutoa eli mu juu ya kupinga na kutokomeza vitendo vya Ukatili wa wanawake na watoto  mashuleni ikiwa ni pamoja na shule ya msingi ya Bangwe, shule ya msingi ya  Muungano, shule ya upili ya Kitwe, shule ya upili ya Mlole na shule ya upili ya St. James huku akieleza changamoto ni watu wengi kutoripoti vitendo hivyo vya ukatili na kuamuliwa ngazi ya familia.

Naye  kiongozi kutoka taasisi ya Living Soul Foundation inayojishughulisha na u na ulinzi wa watoto na kupinga ndoa za utotoni  Bi. Happines Nkorogo akitoa taarifa za taasisi yake alisema wameweza kufanya uelimishaji wa wanafunzi mashuleni vya kuhakikisha vitendo hivyo vya ukatili kwa  wanawake na watoto vinatoweka kabisa baahi ya shule ni pamoja na shule ya upili ya Kichakachui, shule ya upili ya Katubuka, kitongoni na shule ya upili ya Kitwe.

Aliendelea kusema lengo kubwa ni kuhakikisha mtoto na mtoto wa kike wanakuwa salama na kufikia ndoto zake licha ya changamoto ambayo watoto wa kike ni kupewa kazi nyingi za nyumbani tofauti na watoto wa kiume na wazazi wanapongombana watoto hutelekezwa na kubaki na malezi yasiyo ya wazazi wote.

Wadau wengine waliotoa taarifa ni pamoja na Kenneth Hageze kutoka taasisi ya Sanganigwa ya kulea watoto yatima, Betrida Buhaga mratibu wa taasisi ya MAPAO inayojishughulisha na usaidizi wa kisheria , elimu na utatuaji wa migogoro,  kiongozi kutoka ofsi za Uhamiaji ndugu. Ally Hadivumi  wakiwemo wataalamu kutoka ofsi ya mkurugenzi.

Baada ya kuwasilisha taarifa za utendaji kazi kutoka kwa wadau mbalimbali  kamati iliweza kujadili na kuweka maazimio ya utekelezaji katika shuguli za utekelezaji ikiwa ni pamoja na taarifa za wadau na wataalamu kuhakikisha zinawasilishwa zikiwa na takwimu halisi kutoka katika maeneo wanayofanyiwa kazi,na kuhakikisha wadau hao wanapofanya kazi kushirikisha vyombo vya habari ili kuhakikisha elimu inawafikia wananchi kwa urahisi zaidi.

Kikao hicho kilichoanza majira ya saa nne asubuhi kiliweza kufungwa na mwenyekiti wa kikao hicho kwa kuwashukuru wote waliohudhuria na kuwataka wadau wote kushirikishana katika shughuli wanazokuwa wanazifanya kila siku na kuendelea kuhamasisha wananchi kuhakikisha wanaripoti na kutoa taarifa vitendo vya ukatili katika mamlaka husika pindi vitendo hivyo vinapotokea.


Picha zaidi za habari hii nenda katika maktaba ya picha.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa