• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

KAMATI ZA KUTOKOMEZA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO MANISPAA YA KIGOM A/UJIJI NA HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA ZAFUNDWA, ZATAKIWA KUIBUA VITENDO VYA UKATILI VISIVYORIPOTIWAYOLIPOTIWA NDANI YA JAMII, Regional Commitee

Posted on: September 15th, 2020

 Na Mwandishi wetu

Kamati  zinazoshughulika na kutokomeza Ukatili wa dhidi ya Wanawake na Watoto(MTAKUWWA) Manispaa ya Kigoma/Ujiji  na Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma zatakiwa kuibua mbinu za uibuaji matukio ya Ukatili yanayofanyika Ndani ya Halmashauri hizo

Kamati hizo za Halmashauri zilitakiwa hivo Jana Septemba 14, katika Ukumbi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji zilipotembelewa na Kamati ya kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) ngazi ya Mkoa ikiongozwa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Kigoma Ndugu. Moses Msuluzya ikiwa na lengo la kukagua namna kamati za Halmashauri zinavyofanya kazi

Akiongea na Kamati hizo Kaimu Katibu Tawala huyo alisema kwa sasa Katika Mkoa wa Kigoma unachangamoto ya Vitendo vya ukatili vinavyofanya kutolipotiwa na badala yake  kusuluhishwa ndani ya Jamii na familia hali inayofanya kuathirika kwa wahanga na jamii kukithiri na kuongezeka kwa vitendo hivyo

Katibu Tawala huyo  aliitaka Kamati hiyo kuibua mbinu mpya kwa kuendelea kutoa elimu ndani ya  jamii katika maeneo ambayo vitendo hivyo vya ukatili vimekithiri na kutoa mawasiliano kwa maafisa Ustawi wa Jamii na Dawati la Jeshi la Polisi ili vitendo hivyo kuweza kuripotiwa

Aliendelea kusema elimu na kujitambua kwa jamii ndicho kitu kitakacholeta mabadiliko makubwa ndani ya Jamii huku akizitaka kushirikiana na idara zingine kama idara ya Elimu Msingi na Sekondari katika kuhakikisha vitendo vya ukatili vinapungua na kuisha katika Halmashauri zote mbili


Awali akisoma taarifa ya namna Kamati ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji inayoshughulikia Kutokomeza, vitendo vya Ukatili wa  Wanawake na Watoto  Afisa Ustawi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji  Bi. Agnes Punjila alisema Jamii na wakazi wa Manispaa hiyo wamekuwa wakipata elimu ya namna kupinga Ukatili wa Wanawake na Watoto huku jamii hiyo ikatakiwa kutoa taarifa ya kuripoti kwa wakati vitengo hivyo vya ukatili  

Akitoa takwimu za vitendo walivyoshughulikia katika Manispaa hiyo  kwa kipindi cha Januari hadi June 2020 alisemà vitendo vilivyolipotiwa vya ukatili ni Watoto mia moja arobaini na moja (141) wakitelekezwa na wazazi wao,  huku Watoto wanaofanya kazi mtaani wakiwa ni watoto wa kike 44 , mtoto wa kiume akiwa mmoja     ukatili wa Kimwili ikiwa ni pamoja na Kipigo na kuchomwa na vitu vyenye Ncha kali wanawake nane (08),  huku wanaume wawili (02) wakifanyiwa ukatili huo

Aliendelea kutoa takwimu za mashauri ya  ukatili dhidi ya Wanawake yaliyoshughulikiwa ni pamoja na matunzo ya watoto  mia moja arobaini na moja (141),  Utatuzi wa migogoro ya Ndoa thelathini na tano (35), kuripotiwa kwa Mimba nane (08) za wanafunzi, kesi za watoto zilizopo Gereza la Bangwe zikiwa kesi  tatu (03), huku kesi zilizopo katika mahakama ya Watoto  zikiwa kesi nane (08)

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Bi. Zilipa Kisonzera Akitoa takwimu za Hali ya ukatili kwa kipindi cha Januari hadi Juni 2020 na namna walivyoshughulikia alisema jumla ya Mashauri dhidi ya watoto yaliyofanyiwa  kazi  kwa miezi sita yalikuwa 121 huku mashauri dhidi ya wanawake 22 yakishughulikiwa na Watoto walioathirika  na vitendo výa ukatili yaliyoshughulikiwa wakiwa  wavulana 47,  Wasichana 74 na wanawake 22

Aidha wawasilishaji wote wa Halmashauri hizo walisema kwa sasa wanakumbana na changamoto  ni Jamii kutotoa ushirikiano pindi kesi hizo za vitendo vya ukatili zinapopelekwa Mahakamani hasa kesi za ubakaji na ulawiti, changamoto nyingine ikiwa ni kukosa kituo cha pamoja (One stop Centre) kwa ajili ya kuharakisha kesi za ukatili  

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu Mwailwa Pangani akizungumza katika kikao hicho  aliishukuru  kamati hiyo ya MTAKUWWA ngazi ya Mkoa kwa kutembelea kamati hizo za Halmashauri Mbili huku akiwaahidi kuendelea kuimarisha kwa kamati ya MTAKUWWA Manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa kuiwezesha kupambana na vitendo vya ukatili kwa kupatiwa mafunzo na kuendelea kuelimisha jamii kuachana na vitendo hivyo vya ukatili kutokana na athari zake  

Picha na video zaidi ingia Maktaba ya picha www.kigomaujijimc.go.tz


Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa