• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

KATIBU MKUU WIZARA YA AFYA DKT CHAULA, AMTAKA MKURUGENZI WA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI KUTENGA ENEO LA MAKABURI KWA WATU WANAOFARIKI KWA MAGONJWA YA MLIPUKO, official visit

Posted on: February 11th, 2020

Katibu mkuu wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainabu Chaula jana februali 10, amemtaka mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji kutenga maeneo maalumu ya kuzika watu wanaokufa kutokana na magonjwa ya mlipuko

Katibu mkuu huyo ametoa tamko hilo ikiwa ni katika kukabiliana na magonjwa ya mlipuko yanayoendelea kuathiri baadhi ya Nchi  Duniani, ambapo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo  inameathiriwa na Ugonjwa wa Ebola huku Nchi ya China ikiendelea kuathiriwa na  vifo kutokana na ugonjwa wa Corona

Katibu Mkuu alisema lengo la ziara yake ni kukagua namna huduma za afya zinavyotolewa kwa Wananchi  na kuangalia namna Mkoa na Halmashauri zilivyojiandaa katika kukabiliana na wagonjwa wa magonjwa hayo yamlipuko kutokana na kuwa pembezoni na mipakani ya nchi jirani

Akiwa katika zahanati ya Bangwe ambapo ndipo kituo cha kuwahudumia wagonjwa wa Ebola na Corona  endapo watabainika kuwepo, alisomewa taarifa ya Utendaji kazi wa Zahanati hiyo ambapo kwa mjibu ya Sensa ya Mwaka 2012 eneo hilo lina jumla ya wakazi elfu kumi na tisa (19,000) na Zahanati hiyo inapokea wagonjwa  wa nje sitini (60) kwa siku , na kutoa huduma ya Kliniki ya baba, Mama , na watoto  huku ikiwa na watumishi kumi na moja (11)

Katibu mkuu huyo aliendelea na ziara yake hadi katika Zahanati ya Kigoma ambapo alisomewa taarifa na Mganga Mfawidhi wa kituo hicho Ndugu. Godlove Myinga kuwa Zahanati hiyo inahudumia wakazi wa Kata ya Kigoma  yenye wakazi 21577 kwa mjibu ya Sensa ya mwaka 2012 na kusema  zahanati hiyo ina watumishi 22 ambapo inahudumia wagonjwa wan je elfu moja (1000)kwa mwezi, wastani wa wanawake 30 hujifungua kwa mwezi,huku huduma zingine za upimaji wa VVU hutolewa, upimaji wa saratani ya Shingo ya Kizazi na huduma ya uzazi wa mpango hutolewa

Mganga mfawidhi  huyo aliendelea kueleza mafanikio ya zahanati ya Kigoma kuwa hadi hivi sasa imeweza kupanda kutoka nyota moja hadi kufikia nyota mbili, na kusema huduma ya wanawake ya kujifungua inatolewa huku akisema uboreshaji wa mazingira kwa kupanda miti na utengenezaji wa bustani unaendelea ili kuwa kivutio na faraja kwa wagonjwa wanaofika kupata huduma

Alisema licha ya mafaniko hayo zipo changamoto ambazo zinapaswa kutatulia kwa zahanati hiyo kuwa na eneo dogo ukilinganisha na idadi kubwa ya wateja wanaofika kupata huduma huku akiomba kuongezewa kwa eneo lililokuwa ofisi ya Halmashauri ya Kigoma kabla ya kuhama ofisi hizo na kuomba majengo ya Sandra yanayomilikiwa na halmashauri ya Uvinza

Naye katibu mkuu amepongeza shughuli zinazofanywa  na watumishi wa Zahanati zote mbili kwa kuwahudumia wananchi na wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji huku akiwataka kuendelea kufanya kazi kwa kuendelea kuboresha huduma zinazotolewa

Alisema katika zahanati ya Bangwe huduma zinazotolewa ziendelee kutolewa  kwa wagonjwa wa kawaida na endapo wagonjwa wa magonjwa ya mlipuko watabainika(kugundulika) kuwepo kutokana na dalili za magonjwa  ya Ebola na Corona huduma zitasitishwa kwa wagonjwa wakawaida na kuhamia zahanati ya Kigoma

“hadi hivi sasa hakuna mgonjwa aliyebainika kuwepo Nchini wa magonjwa haya ya Ebola na Corona inayoendelea kuwatesa wenzetu Wachina, tayari tumeshachukua tahadhari katika maeneo yetu ya Mipaka, Bandarini na Viwanja vya Ndege, wapo watu wanaendelea kuchunguza na wanavifaa maalumu kwa hiyo Watanzania wasiwe na wasiwasi waendelee kufanya kazi lakini pia lazima tuchukue tahadhari katika kuhakikisha magonjwa haya hayaingii nchini na endapo mgonjwa atabainika tujue namna ya kumhudumia na wapi huduma hizo zinaweza kutolewa” alisema katibu Mkuu huyo

Alihitimisha kwa kuwataka watumishi wa afya kufanya kazi kwa kujiwekea malengo ili kutoa huduma zilizo bora na kumtaka mkurugenzi wa halmashauri hiyo kufatilia majengo hayo yanayomilikiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma na Uvinza kwa kufanya mazungumzo ili kupata Majengo hayo kwa lengo la zahanati hiyo kuipandisha hadhi kuwa kituo cha afya

Naye mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Ndugu. Mwailwa Pangani alimpongeza Katibu mkuu huyo kwa kufanya ziara katika Manispaa hiyo na kuahidi kutenga eneo la makaburi la kuzika  watu wanaofariki kwa magonjwa hatari na ya mlipuko huku akiahidi kufatilia majengo yanayomilikiwa na Halmashauri jirani katika Manispaa hiyo

.Maambukizi ya ugonjwa wa Ebola, yalionekana kuongezeka mwaka jana 2019 Mashariki mwa Demokrasia ya Congo, baada ya kuzuka kwa ugonjwa huu hatari ambapo hadi hivi sasa inasemekana kasi ya maambukizi ya  Ugonjwa huu umepungua nchini humo

Watu zaidi ya 1,800 walipoteza maisha na wengine zaidi ya 2,000 kuambuakizwa virusi vya ugonjwa huo, kwa mujibu wa shirika la Afya Duniani (WHO),

Wakati nchi ya China ikiendelea kupambana na ugonjwa wa Corona watalaamu walieleza  watu zaidi ya 75,000 wanaweza kuwa na maambukizi ya virusi vya corona, katika mji wa Wuhan, huku vifo hadi kufikia jana vikiwa vifo 908 vilivyotokana na ugonjwa huo kwa mjibu wa vyombo vya habari vya kimataifa

Picha na video zaidi ingia katika maktaba ya picha www.kigomaujijimc.go.tz

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa