• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

KATIBU TAWALA ATOA AGIZO KWA WATAALAMU KUJA NA ANDIKO LA KUANZISHA SHULE AU KITUO CHA MICHEZO MKOANI KIGOMA, Sports

Posted on: June 9th, 2021

Na Mwandishi wetu

Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Ndugu.  Rashidi Mchatta leo June 9, 2021 amefungua Mashindano ya michezo kwa Shule za Sekondari (Ummiseta) yaliyoanza kwa ngazi ya mkoa katika Uwanja wa chuo cha walimu kasulu


Akifungua Mashindano hayo Katibu Tawala huyo amewaagiza wataalamu wa Mkoa huo kuja na andiko la  kuanzisha shule au kituo cha  michezo (Centre of Sports Academy) na baada ya miezi mitatu wataalamu hao wawe wamewasilisha majibu ofisini kwake juu ya utekelezaji wa agizo Kwa lengo la kukuza vipaji vilivyopo Mkoani hapo


Amewapongeza Wakurugenzi wa Halmashauri, Maafisa Elimu, Maafisa Michezo ,Walimu wa Michezo na Wanamichezo wote tangu walipoanza Mashindano kwa ngazi ya Shule, Kata hadi ngazi ya Wilaya na sasa kushiriki katika Mashindano ngazi ya Mkoa


Aidha amewataka Walimu na wakufunzi wa michezo kuchagua wana michezo bora katika kuunda timu ya Mkoa   watakaoleta ushindi kwa Mkoa wa Kigoma kwa michezo yote na kutozingatia usawa wa kuchagua wachezaji kutoka katika kila Halmashauri

Akihutubia katika uwanja huo amesema wanamichezo wana nafasi kubwa katika kufanya vizuri katika masomo ya darasani huku akiwataka wanafunzi hao wa Shule za  Sekondari kuzingatia pia masomo huku wakikuza vipaji walivyonavyo


Afisa elimu Mkoa wa Kigoma Ndugu. Omary Mkombole Awali akimkaribisha Mgeni Rasmi alisema wapo wanamichezo mia saba (700) wanaoshiriki  kutoka katika Halmashauri nane (8) za zinazounda Mkoa huo ,huku akisema wanaimani watapata wachezaji bora watakaoishiriki ngazi ya Taifa na kuiletea ushindi Mkoa wa Kigoma


Mashindano hayo ya ngazi ya Mkoa yenye lengo la kupata timu bora zitakayoshiriki kwa ngazi ya Taifa  katika Michezo mbalimbali yatafanyika  kwa siku nne (4) ambapo yanatarajia kukamilika June 11, 2021 na Michezo itakayofanyika ni pamoja na Mpira wa Miguu, Mpira wa Pete, Mpira wa Mikono, Mpira wa Wavu, Mpira wa Kikapu, Riadha na Mashindano ya fani za ndani yaani Kwaya na Ngoma na Kitaifa Mashindano haya yanatarajiwa kufanyika Mkoani Mtwara

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa