• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

KATIBU TAWALA MKOA WA KIGOMA AWATAKA WAKAZI WA MKOA HUO KUTUMIA SIKU 3 ZILIZOONGEZWA KUJIANDIKISHA KATIKA DAFTARI LA ORODHA YA WAPIGA KURA.Regional Administration secretary

Posted on: October 14th, 2019

Katibu tawala wa mkoa wa Kigoma Ndugu. Rashid K. Mchata  amewataka wakazi wa mkoa wa Kigoma kutumia fursa ya siku tatu  zilizoongezwa kwenda kujiandikisha katika daftari la orodha ya wapiga kura  ili kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa November 24

Aliyasema hayo jana October 13 katika ziara yake aliyoifanya ya kutembelea halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji na halmashauri ya Kigoma vijijini(kigoma dc) kukagua namna zoezi linavyofanyika katika vituo vya kujiandikishia

Akiwa katika halmashauri ya Kigoma vijijini msimamizi wa uchaguzi  wa serikali za mitaa Bi. Petronila B. Gwakila alitoa taarifa na kusema uandikisha unaendelea  vizuri ambapo hakuna changamoto yeyote iliyokwisha jitokeza katika uandikisha na maafisa uandikishaji walipata semina namna watakavyofanya kazi kwa kushirikiana na mawakala wa vyama vya siasa

Naye msimamizi wa uchaguzi  manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Emmanuel Katemi akitoa taarifa wakiwa katika halmashauri hiyo alisema uandikishaji unaendelea vizuri na watu wamejitokeza kwa kiasi kikubwa  ambapo alisema katika kituo cha kata ya ofisi ya kitongoni uandikishaji uko kwa asilimia 92 kwa makisio ya wapiga kura na kituo cha shule ya msingi Bangwe kikiwa na asilimia ya 60 ya makisio ya wapiga kura.

Nao baadhi ya wananchi waliojitokeza kujiandikisha katika daftari la orodha ya wapiga kura Ndugu. Hamza Yassini na Bertha Musa wameweza kumpongeza katibu tawala huyo kwa ufuatiliaji anaoufanya na kusema wao tayari wamejiandikisha na wapo tayari kusubilia ratiba nyingine inayofuata na kueleza watashiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa kwa kuchaguz na kugombea nafasi za uongozi.

Naye Katibu Tawala huyo amewapongeza wananchi kwa kujitokeza katika uandikishaji huo na kuwataka wananchi kuweza kujitokeza zaidi katika zoezi hilo kutokana na kuongezewa siku na waziri mwenye dhamana katika uandikishaji huo.

Aliwaasa waandishi na mawakala kutomkatilia mtu yeyote katika kujiandikisha katika daftari la orodha ya wapiga kura kutokana na kuwa takwa la kikatiba kwa kila raia mwenye umri wa miaka 18 ila ni kufuata hatua za pingamizi kwa mtu anayetiliwa mashaka pindi uandikishaji huo utakapomalizika.

Alihihitimisha kwa kuipongeza wilaya ya Kakonko kwa kufikia asilimia sitini (60%) ya wapiga kura wote ambao wameshaandikwa katika daftari hilo la orodha ya upigaji kura na  kuwataka wasimamizi hao wa uchaguzi kubuni mbinu bora za kuwafikia wananchi na uboreshaji wa matangazo ya sauti  yanayokuwa yakipita mtaani katika kuwaelimisha wananchi

Uandikishaji huo wa orodha ya wapiga kura uchaguzi wa serikali za mitaa ulianza October 8 ambapo ulitarajiwa kuhitimishwa oktoba 14 lakini kutokana na sababu zilizoelezwa na waziri wa TAMISEMI Mhe. Sulemani Jafo  mikoa mingi nchini Tanzania mvua kunyesha kwa kiasi kikubwa na watu kushindwa kwenda kujiandikisha na sababu nyingine wananchi kuwa na dhana potofu ya mtu aliyejiandikisha katika daftari la kudumu la mpiga kura kutojiandikisha tena katika uchaguzi huo wa serikali za mitaa jambo ambalo sio sahihi.

Waziri hyo wa TAMISEMI ameongeza siku tatu (3) Kutokana na sababu hizo na kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa za Mwaka 2019 na matangazo ya Serikali Na 371,372,373 na 374 ya Mwaka 2019 Waziri mwenye dhamana na Serikali za mitaa ana mamlaka ya kutoa miongozo mbalimbali kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

picha zaidi ingia katika maktaba ya picha

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa