Na Mwandishi Wetu
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bw.Kenani Kihongosi Leo Februari 21, 2026 amekagua maendeleo ya ujenzi wa Soko la Mwanga lililopo Manispaa ya Kigoma/ Ujiji.
Akikagua ujenzi huo unaoendelea amewapongeza Wataalamu na mafundi kwa usimamizi wa ubora wa Jengo huku akiendelea kusistiza usimamizi madhubuti na akimtaka Mkandarasi kukamilisha ujenzi huo kwa wakati kwa mjibu wa mkataba.
Amesisitiza kuhakikisha Wafanyabiashara wa awali pindi soko litakapokuwa limekamilika kupewa kipaumbele na kufanya biashara ili kuinua uchumi wa mji huo.
Naye, Mhandisi wa Ujenzi kutoka Kampuni ya ujenzi ya Asabhi contractor Company Ltd in Jv with Pioneers Builders Limited Eng. Joseph Marando amehakikisha kuwa mradi huu wa ujenzi upo katika hatua za mwisho na kukamilika ifikapo Aprili Mwaka huu.
Manispaa ya Kigoma Ujiji
Sanduku la Posta: S.L.P 44
Simu: +255 28 2802535
Namba ya Simu: +255765660847
Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz
Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa