• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

KITUO CHA AFYA KILICHOJENGWA KWA FEDHA ZA TOZO, CHAANZA KUTOA HUDUMA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI Health Centre

Posted on: November 9th, 2022

Na Mwandishi Wetu  

Kituo cha afya kipya cha Buhanda kilichopo Manispaa ya Kigoma/Ujiji kilichojengwa kwa fedha za tozo (kodi) ya miamala ya simu Jana Novemba 08, 2022 kilifunguliwa kwa lengo la kuanza kutoa huduma za afya kwa Wananchi

Kituo hicho kilifunguliwa na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Bi. Ester Alexander Mahawe   ambapo aliwataka Wananchi kutunza miundombinu ya kituo hicho ili  kuwanufaisha Watu wengi

Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Athuman Msabila alisema ujenzi wa Kituo hicho uliohusisha Jengo la Wagonjwa wa nje, Maabara na kichomea taka umegharimu kiasi cha fedha za Kitanzania Millioni Mia tano (Tsh 500, 000, 000/=) ikiwa ni fedha kutoka Serikali kuu iliyotokana na kodi za miamala ya simu

Alisema Serikali inaendelea kutekeleza miradi ya afya katika  Manispaa hiyo na inatarajia  kupokea kiasi cha fedha za Kitanzania Million mia tano (Tsh 500, 000, 000/=) kutoka Serikali Kuu  kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya itakayojengwa Kata ya Kagera  

Mkurugenzi  huyo alisema kwa sasa ujenzi wa  jengo jingine la  upasuaji na wodi ya wazazi unaendelea kwa fedha za Kitanzania Million mia mbili hamsini (Tsh 250, 000, 000/=) kutoka Serikali Kuu   katika kituo hicho cha afya

Naye Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo Dr. Hashimu Mvogogo alisema tayari wahudumu wa Afya watano (05) na Mganga wa Kituo hicho wamepangwa  na huduma zitakazoanza kutolewa ni pamoja na huduma kwa wagonjwa wa nje (OPD) pamoja na kupumzisha, huduma za dharura, huduma za kimaabara huku akisema kukamilika kwa miundombinu inayoendelea kujengwa kutaanza kutolewa kwa huduma ya upasuaji na huduma ya baba,Mama na mtoto

Naibu Meya wa Manispaa hiyo Bi. Mgeni Kakolwa aliwataka wahudumu wa Afya kufanya kazi kwa weredi kwa kuzingatia misingi ya kazi na upendo kwa Wananchi wanaowahudumia huku akiipongeza Serikali kwa uboreshaji wa miundombinu unaoendelea  katika Manispaa hiyo

Diwani wa Kata ya Buhanda Mhe. Gilberth Kilahumba aliishukuru Serikali kwa kuendelea kujenga, kuboresha na kusogeza huduma mbalimbali kwa Wananchi kama vile Ujenzi wa Madarasa na  miradi ya Afya katika Kata hiyo

Kukamilika kwa ujenzi wa kituo hicho cha afya cha Buhanda kunafanya Manispaa hiyo kuwa na jumla ya idadi ya vituo vya afya Vitatu (03)   ikiwemo  kituo cha afya cha Ujiji na kituo cha Afya Gungu


Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa