• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MADIWANI WAPITISHA BAJETI YAO YA MWISHO KATIKA UONGOZI WAO 2019/2020 ”WAWAONYA WATENDAJI KUTOWAONA MAZEZETA” ASEMA NAIBU MEYA BUDGET

Posted on: February 11th, 2019


Na mwandishi wetu.

Baraza la madiwani la manispaa ya Kigoma/Ujiji juzi ijumaa February 8, liliweza kupitisha bajeti ya mwaka wa fedha 2019/2020 kiasi cha  Tsh 35,175,030,076.00.

Katika baraza hilo lililoanza majira ya saa nne asubuhi chini ya mwenyekiti na Meya wa manispaa hiyo Hussein Rihava na katibu Kaimu Mkurugenzi manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Bennert Ninalwo, ambapo mwenyekiti alianza kwa kuwakaribisha wajumbe wa kikao hicho na kuwa na ushirikiano kwa kuhakikisha wanatoa mapendekezo yatakayo saidia katika utekelezaji wa bajeti.

Akiwasilisha bajeti hiyo hiyo kwa baraza hilo la madiwani Mchumi wa Mipango,Uchumi na Takwimu Ndugu. Filimbi(kwa jina moja) alitoa mchanganuo wa bajeti akisema kiasi cha shilingi 2,042,533,234.00 ikiwa ni mapato ya ndani (OS), shilingi 923,934,000.00 ni ruzuku toka Serikali kuu , shilingi 24,941,741,000.00 ni ruzuku ya Mishahara, na shilingi 7,266,781,842.00 ni fedha za miradi ya maendeleo kwa fedha za ndani na wafadhili, huku akimtaka Mwenyekiti wajumbe wake kuridhia kiasi hicho cha bajeti.

Nao madiwani walipata wasaa wa kujadili bajeti hiyo, moja ya mjumbe na Diwani wa Kata ya Kibirizi mhe. Ruhomvya akijadili bajeti hiyo aliweza kutoa mapendekezo kwa kueleza ili bajeti iweze kutekelezwa ni lazima makusanya ya mapato ya ndani yakusanywe ipasavyo na watumishi wa halmashauri na hasa katika minara ya makampuni ambayo ipo katika maeneo ya halmashauri huku akitaka bajeti hiyo inatoa kipaumbele kwa kutenga fedha kwa sekondari ya ya Upili Kasingirima na kuwa na madarsa ya kidato cha tano na sita.

Naye mwenyekiti wa kamati ya Elimu uchumi na Afya na diwani wa kata ya Kigoma mjini Mhe. Hussein Kariango, akichangia bajeti hiyo alisema Manispaa kupitia  wataalamu wake waweke mipango dhabiti ya kuhakikisha chanzo cha mapato cha vibali vya ujenzi kinasimamia kwa uzuri katika kuongeza fedha za ndani kwa lengo la kutekeleza bajeti hiyo  huku akiwataka wataalamu kuendeleza vyanzo vingine vya mapato kwa soko la Mwasenga, soko la Ujiji na Standi ya Ujiji kwa kuweka mazingira na miundombinu inayofaa huku akikumbusha fedha zinazodaiwa na madiwani wa halmashauri hiyo.

Baada ya kujadili bajeti hiyo madiwani waliweza kupitisha bajeti hiyo na mwenyekiti wa kikao hicho akitoa nafasi kwa Kaimu Mkurugenzi wa manispaa alieleza kuwa wataalamu wamepania katika kukusanya fedha na kuhakikisha madeni yote yanalipwa “milioni 30 zimetengwa kwa ajili ya madiwani tutahakikisha tunalipa madeni yote labda shetani atupitie” alisema Kaimu Mkurugenzi huyo.

Naye Naibu meya wa manispaa hiyo Athumani Athumani aliwataka wataalamu kuhakikisha wanasimamia mapato na kuhakikisha wanatoa taarifa ya madiwani ambao sio waaminifu katika kuingilia na kukwamisha ukusanyaji wa mapato huku akiwataka pia wataalamu kutowaona madiwani kama mazezeta.

Naye mwenyekiti wa kikao hicho na meya wa manispaa aliwashukuru madiwani kwa michango yao katika kujadili bajeti na kueleza bajeti hiyo ni mwisho katika uongozi wao kabla ya kuelekea katika uchaguzi mkuu 2020 akiwataka madiwani kusimamia miradi mbalimbali ya maendeleo katika kata zao na halmashauri kwa ujumla.


PICHA ZAIDI INGIA KATIKA MAKTABA YA PICHA

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa