• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MANISPAA YA KIGOMA UJIJI YAUNGANA NA HALMASHAURI ZINGINE TANZANIA NA DUNIA KUADHIMISHA WIKI YA UNYONYESHA, WANAWAKE WASEMA WATAENDELEA KUNYONYESHA HAWATAOGOPA KUTEPETA KWA MAZIWA.

Posted on: August 10th, 2018

Wakazi  na wanawake wa manispaa ya kigoma ujiji siku ya jumanne august 7,wameahidi  kunyonyesha watoto kila inapohitajika na kuachana na tabia za kuogopa kutepeta kwa maziwa ili waweze kuondoa suala la udumavu na kukuza afya za watoto kimwili na kiakili.

Wameyasema hayo katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji  duniani ambapo huadhimishwa tarehe 1-7 august kila mwaka,  na kwa manispaa ya Kigoma/Ujiji yamefanyika katika kata ya businde ikihudhuliwa na wanawake pamoja na wanaume katika ukumbi uliopo jirani na zahanati ya kata hiyo maarufu kama ukumbi wa Rich.

Katika ukumbi huo semina na mafunzo ya unyonyeshaji yaliyofanyika yakiongozwa na Afisa lishe manispaa ya Kigoma/Ujiji bi. Naomi Rumenyera wanawake wamekili kuendelea kunyonyesha kwa wakati na kila mara mtoto anapo hitaji kunyonya, akichangia mada mama aliyejitambulisha kama mama Suzi makala, amesema limekuwepo tatizo kubwa la unyonyeshaji la akina mama kutokana na harakati na shuguli za maisha huku wengine wakiogopa kuwa endapo wangenyonyesha matiti yangeanguka, kulala na kutepeta jambo linalofanya baadhi ya wanaume kutowapenda tena na wengine kukosa wanaume wa kujenga nao mahusiano mengine.

Katika semina hiyo iliyoongozwa na Afisa lishe bi.Naomi Rumenyera  akiwa na kaimu Afisa chanjo  manispaa, afisa maendeleo ya jamii na wadau wengine waliojitokeza akiwemo afisa kutoka taasisi  na asasi ya Ndela iliyopo katika manispaa hiyo, afisa lishe huyo amesisitiza kwa kueleza  umuhimu wa wa maadhimisho hayo na malengo ya siku hiyo ikiwa ni pamoja na uhusiano uliopo baina ya lishe bora,uhakika wa chakula, kupunguza umasikini na unyonyeshaji, unyonyeshaji kama msingi wa maisha lakini pia afisa lishe huyo aliendelea kuonesha umuhimu wa kunyonyesha maziwa ya mama pekee chini ya  kabla ya miezi sita.

Aliendelea kusema unyonyeshaji wa maziwa ya mama ni jukumu la watu wote katika jamii kuhusika ikiwa ni pamoja na wakuu wa masuala ya ulishaji wa watoto wachanga na wadogo, watunga sera, vyombo vya habari, wanawake na watoto, familia na jamii kwa ujumla , kwa kusema watu wote hao watakapohusika suala la udumavu kwa watoto litakungua kwa kiasi kikubwa na kuzuia aina zote za utapiamlo kwa watoto pamoja na wazazi ,lakini pia kuondoa na kupunguza hali ya umasikini kwa kusema kama watoto watanyonya kwa utaratibu watakuwa na akili nzuri ambazo zitawafanya kufikiri na kuwa wabunifu jambo litakalo fanya kuondoka na kupungua kwa umasikini kutokana na ubunifu na akili zinazofikiri.

Afisa lishe huyo akiendelea kutoa semina hizo aliongea na wanaume waliohudhulia katika ukumbi huo kwa kuwataka kuhakikisha kuna mazingira rafiki katika unyonyeshaji kama kutoleta migogoro majumbani kwa wanyonyeshaji jambo linalosababisha  mawazo na kusababisha maziwa kutoweka na kutotoka kutokana na migogoro jambo ambalo ni hatari kwa afya ya mtoto.

               mwanamke alipokuwa akinyonyesha katika ukumbi wa kata ya Businde maarufu kwa jina la ukumbi wa Rich katika maadhimisho ya                       kilele cha wiki ya unyonyeshaji duniani august 1-7.


Lakini pia aliendelea kuwataka wanaume hao kuhakikisha uwepo wa chakula cha kutosha kwa mama mnyonyeshaji ili maziwa yaweze kuzalishwa kwa wingi na kufanya kuimarika kwa afya ya mama na mtoto na kufanya kuwa na kizazi imara kwa mstakabali wa maendeleo ya manispaa na taifa kwa ujumla.

Naye baba aliyejitambulisha kwa jina moja Ndugu. Shabani akiwa na uzoefu wa miaka arobaini katika malezi ya watoto amesema zipo changamoto kadhaa zinazojitokeza  kwa akina baba , baadhi ikiwa ni pamoja na migogoro ya kifamilia jambo ambalo  linaathiri afya kwa akina mama na watoto kwa ujumla katika kipindi cha unyonyeshaji ambapo amekiri na kuwataka wanaume waliohudhulia semina hizo kufanya mabadiliko na kuwa mawakiri kwa wanaume wengine lakini pia kwa kuwataka wanaume kujibidisha katika uzalishaji ili kuweza kuleta matoke chanya ya kifamilia kwa kuhakikisha uwepo wa chakula ili kuimarisha afya ya mama mnyonyeshaji na afya ya mtoto.

Akiendelea kutoa semina hizo Afisa lishe bi. Naomi Rumenyera ametoa takwimu kutokana na Utafiti wa Hali ya Afya  na Demografia wa  mwaka 2015/2016 amesema tafiti hizo zilionesha kati ya wanawake10 wanaonyonyesha , wanawake 5 tu ndio hunyonyesha watoto wao katika saa moja ya mwanzo na wanawake 6 kati ya 10 huendelea kunyonyesha maziwa ya mama ya mama pekee katika miezi sita ya mwanzo.  Na kuwataKa wafanyie kazi kile kinachopaswa katika unyonyeshaji.

Naye afisa maendeleo manispaa ya Kigoma Ndugu. Jabiri Majidi katika semina hizo ameeleza faida za unyonyeshaji na hasara za kushindwa kunyonyeza maziwa pekeeya mama  mtoto miezi sita ya mwanzo na athari zinazotokana na mtoto kupewa chakula kabla ya miezi sita ya mwanzo

Moja ya athari alizozieleza afisa maendeleo huyo mama anaposhindwa kunyonyesha huweza kuleta athari hasi kwa mama hata kwa mtoto pia kama vile kupata saratani ya matiti kwa mama, kutungwa kwa mimba mapema katika umri mdogo wa mtoto aliyezaliwakutokana na kurudi siku zake mapema baada ya kujifungua na athari alizozieleza ambazo mtoto anaweza kupata pindi atakaposhindwa kunyonya maziwa ya mama katika miezi sita ya awali ikiwa ni pamoja na magonjwa kwenye njia ya hewa, kuharisha, kiribatumbo pamoja na kisukari.

Katika uelimishaji na semina hizo zilizofanyika kwa lengo la kilele cha maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji  afisa lishe aliwataka waliohudhulia wote kuhakikisha kuyafanyia kazi na hata ujumbe huo kuwafikishia wanaume  na wazazi wengine hawakupata elimu kwa kuhakikisha kila mmoja anauwa balozi kwa mwenzake  katika kutoa uelimishaji huo. Baada ya kutoka kata ya Businde maafisa hao na wataalamu hao wameenda kutoa uelimishaji huo katika kata ya Rusimbi kwa kukutana na vikundi mbalimbali vya wanawake wakiwemo wajasiliamali ambapo semina hizo zilifanyika katika shule ya msingi Kipampa.Na kitaifa maadhimisho hayo yalifungulia august 1, 2018 na mgeni rasmi akiwa ni waziri wa  afya, maendeleo ya jamii,jinsia, wazee na watoto mhe. Ummy Mwalimu.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa