• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

Manispaa ya Kigoma/Ujiji kugawa vifaa vya kujikinga na Covid-19 kwa Shule za Msingi na Sekondari shule mara zitakapofunguliwa

Posted on: June 25th, 2020

Na Mwandishi wetu

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Frednand Filimbi leo june 25 amesema Manispaa hiyo itagawa vifaa vya kujinga and Ugonjwa wa Corona Kwa shule zote za msingi na sekondari mara tu baada ya wanafunzi kufungua shule

Ameyasema hayo wakati akipokea msaada wa vifaa vya kujikinga na ugonjwa huo kutoka kwa taasisi ya Direct Aid Society vyenye thamani ya fedha za Kitanzania Shilingi Million saba (Tsh 7,000,000/=) inayojishughulisha na kutoa misaada kwa jamii za wahitaji

Kaimu Mkurugenzi huyo amesema kama Manispaa tayari wameweka mpango na vifaa ambavyo watasambaza Mashuleni mara tu wanafunzi watakapokuwa wameanza masomo yao huku akisema msaada huo walioupokea wa Barakoa, Sabuni ,vitakasa mikono, gloves na vipima joto vitaongeza nguvu kuendelea kusambaza katika taasisi za shule na vituo vya kutolea afya

Naye Mkurugenzi wa kampuni hiyo tawi la Kigoma Ndugu Mohamed Arab amesema katika kipindi cha ugonjwa wa Corona wamekuwa na utaratibu wa kuifikia jamii kutoa msaada wa vifaa vya kujikinga na ugonjwa huo ambapo mwezi May, Mwaka huu kampuni hiyo iligawa msaada wa vyakula katika vijiji vya Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma uliogharimu fedha za Kitanzania Shilingi Million ishirini (Tsh 20,000,000/=)

Mkurugenzi huyo amehitimisha kwa ķuishukuru Serikali kwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa misaada wanayokuwa wanaitoa ya kuihudumia jamii huku akisema wataendelea na ushirikiano kwa kufika katika maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji na maeneo mengine ya Mkoa wa Kigoma

Kaimu Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo Dr.Tibezuka Zinga amesema idara ya afya tayari iko tayari kwa ajili ya kutoa msaada wa Kisaikolojia kwa wanafunzi watakaoanza masomo yao siku ya Jumatatu june 29 kwa shule zote za Msingi na Sekondari zilizopo katika Manispaa hiyo

Ameendelea kuwasisitiza na kuwataka wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji kuchukua tahadhari ya kujikinga na Ugonjwa huo kutokana na kupungua Nchini  kwa kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima,  kunawa mikono kila mara , na kuvaa barakoa

March 17, Serikali ilitangaza kufungwa kwa shule na vyuo kutokana na idadi  maambukizi ya Virusi vya korona, kutokana na kampeni iliyoongozwa nchini ya Kuliombea Taifa na kampeni ya kujifukiza maarufu kwa jina la "Kupinga Nyungu" virusi vya corona vimeendelea kupungua Nchini ambapo June 16, Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dr John Pombe Magufuli akihutubia hotuba ya kulifunga Bunge la 11 alitangaza June 29 shule za Msingi na Sekondari kuanza Masomo yao

Rais Magufuli Alisema ''Namshukuru Mungu kwa kuliepusha taifa hili na virusi vya corona na nina washukuru viongozi wa dini kwa kuitika wito wa serikali kufanya maombi maalum ya kutuepusha na janga la corona.''

''Kutokana na kushuka kwa hali ya maambukizi ya ugonjwa wa corona napenda kutumia nafasi hii kutangaza kuwa shule zote zilizokuwa zimebaki zifungulliwe, lakini pia shughuli zote zilizokuwa zimezuiwa nazo ziendelee'', huku akiendelea kuwasihi Watanzania kuendelea kuchukua tahadhari kuepuka maambukizi ya virusi vya corona.



Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa