• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI YAKABIDHI VIFAA VYA USAFI VYA TSH MILLION 83, KWA VIKOSI KAZI, Sanitation

Posted on: March 5th, 2021

Na Mwandishi wetu

 Manispaa ya Kigoma/Ujiji leo march 5, 2021 imekabidhi vifaa vya Usafi vilivyogharimu kiasi cha fedha za Kitanzania Million themanini na tatu (83,000,000/=)  kwa vikosi kazi vya Usafi ishirini na mbili (22) ili kuhakikisha  mji unakuwa katika hali ya usafi


Vifaa hivyo vimekabidhiwa kwa vikosi kazi vya usafi vya mitaa vilivyoundwa na wataalamu ngazi ya kata wakishirikiana na wenyeviti wa mitaa ili kuhakikisha mji unakuwa safi kupitia Usafi utakaofanyika na kuchangia tozo za uzoaji wa taka hizo


Akikabidhi vifaa hivyo kwa niaba ya Mkurugenzi, Mganga Mkuu wa Manispaa Dr. Sebastian Siwale amewataka watendaji kata na mitaa kuhakikisha wanasimamia vikosi kazi vya usafi katika mitaa yao ili kuhakikisha mji unakuwa safi wakati wowote


Aidha Mganga Mkuu huyo amevitaka vikosi kazi vya usafi kufanya kazi hiyo kwa uaminifu kwa kukusanya taka katika barabara za mji, Makazi na Taasisi mbalimbali za Serikali na zisizo za Serikali kwa wakati ili kuepuka mrundikano wa uchafu unaoweza kusababisha magonjwa ya mlipuko kwa binadamu  kutokana na kukabidhiwa kwa vifaa vitakavyorahisisha shughuli hiyo


Kaimu Mkuu wa idara ya Usafi na Mazingira Ndugu. Elishaphati Rusemvya amesema  kwa sasa Manispaa ya Kigoma/Ujiji inazalisha tani mia moja hamsini na mbili (152)kwa siku  ambapo taka hizo husafirishwa kwenda dampo la Kisasa lililopo Msimba linalomilikiwa na Manispaa hiyo


kiongozi huyo amewataka wakazi wa Manispaa  kuachana na tabia ya kulima katika hifadhi za barabara na kuacha tabia za upandaji wa mazao marefu na kufanya hivo ni kinyume na sheria ndogo hali inayoweza kusababisha mwananchi kushitakiwa kwa kuvunja sheria hiyo, Aidha amehitimisha kwa kuzitaka Taasisi mbalimbali na wananchi kutoa ushirikiano kwa kufanya Usafi wa Mazingira na kuhakikisha taka hizo zinafikishwa katika vizimba vilivyowekwa mtaani kupitia vikosi kazi


Mtendaji wa Kata ya Kigoma Ndugu. Kasimu Nyamkunga amesema wao kama wataalamu watahakikisha wanasimamia vikosi kazi vya usafi ili kuhakikisha mji unakuwa safi katika mitaa mbalimbali na makazi ya watu  


Katika shughuli zinazofanywa na vikosi hivyo ni pamoja na usafi wa barabara za mji, uzoaji taka kwa makazi na Taasisi ambapo kila kaya hulipia kiasi cha fedha za Kitanzania Tsh 1000/=  na taasisi kuanzia elfu thelathini hadi laki mbili (30,000/= hadi 200,000/=) kwa mwezi kutokana na ukubwa wa Taasisi na uzalishaji taka


Vifaa hivyo vya Usafi vimekabidhiwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kutokana na msaada uliotoka kwa kampuni ya Belgium Development Agency inayojishughulisha na uchakataji wa taka na kufadhiliwa na Umoja wa Ulaya , vifaa hivyo vilivyokabidhiwa ni pamoja na Troli kubwa 44, Troli ndogo 44, Mifagio 220, reki 220,   rain boot(Gambuti) 220, gloves 220, na Koreo 220


Kampuni hiyo inayojishughulisha na uchakataji wa taka Makao Makuu yao yapo Mji Mkuu wa Bunjumbura Nchini Burundi ikiwa inafanya kazi Nchi tano (05) za Tanzania,  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Zambia , Burundi na Rwanda



Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • WAJASIRIAMALI WAENDELEA KUFIKIWA NA WATAALAMU KIGOMA UJIJI. Social services

    May 30, 2025
  • UGAWAJI WA VYANDARUA BURE UNAENDELEA KWENYE VITUO KIGOMA UJIJI. Health protection

    May 29, 2025
  • WAJASIRIAMALI KIGOMA UJIJI WATEMBELEWA NA WATAALAMU.

    May 28, 2025
  • RC ANDENGENYE AZINDUA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA MKOA WA KIGOMA. Malaria protection

    May 28, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa