• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI YAKUTANA NA UONGOZI WA SHIRIKA LA RELI TANZANIA (TRC) KUTATUA MGOGORO WA KUVUNJIWA MAKAZI WAKAZI WA ENEO LA KATOSHO GUNGU. land conflict

Posted on: October 11th, 2019

 Halmashauri ya manispaa ya Kigoma/Ujiji leo October 10, imefanya ziara katika eneo la Katosho kata ya Gungu na uongozi wa Shirika la reli Tanzania(TRC)  katika kutatua mgogoro wa kuvunja makazi ya wananchi wa eneo hilo  kwa madai kuwa ni eneo la shirika hilo.

Ziara hiyo imefanyika katika eneo hilo ikiwa ni sera ya serikali ya awamu tano wananchi kutosumbuliwa katika makazi  yao kama watakuwa hawaja vunja sheria za nchi  ambapo eneo hilo lina zaidi ya nyumba za makazi 25 na viwaja vya wananchi 12.

Katika ziara hiyo wataalamu, madiwani wa manispaa hiyo pamoja na wataalamu wa shirika la reli (TRC) wameweza kujilizisha kwa kuchukua vipimo vya eneo la shirika la reli ambapo imebainika kuwa awali eneo la katosho ndio ilikuwa eneo la kituo cha treni(Stesheni)  ambapo vipimo vinakuwa tofauti na eneo la njia ya reli ya kawaida kuwa na vipimo vya mita 30 kutoka katika njia hiyo kwa pande zote mbili.

Katika eneo hilo lililopimwa vipimo vilivyochukuliwa ni mita 90, mita 112, mita 156 kutoka usawa wa eneo la reli ambapo baadhi ya nyumba zimeonekana kuwa katika eneo la vipimo hivyo licha ya sheria ya awali ya shirika hilo kuwa mita 30 kutoka reline kwa pande zote mbili

Akiongea katika ziara hiyo Mkurugenzi wa manispaa ya Kigoma/Ujiji  Ndugu. Mwailwa Pangani amesema shirika la reli linalo wajibu wa kuomba ardhi kwa halmashauri kama shirika hilo litakuwa na uhitaji jambo ambalo halmashauri haikuwahi kupokea maombi hayo na shirika la reli kutoweka mipaka ya eneo linalodaiwa kuwa la shirika hilo .

Ameendelea kusema eneo hilo linalodaiwa na shirika la reli limepimwa na halmashauri mwaka 2002 na kugawiwa kwa wananchi, ambapo ni miaka zaidi ya kumi na mbili (12) wananchi wakiishi katika eneo hilo na  kisheria makazi hayo ni halali kwa wakazi wa eneo hilo.

Naye Afisa  wa ardhi wa shirika la reli(TRC) Ndugu. Fredrick Kusekwa amesema maeneo yanayomilikiwa na shirika hilo yanawekewa alama na yanalindwa na kuna makazi yamewekwa kando ya reli na yanayokaliwa na wataalamu wa shirika hilo kwa lengo la kulinda maeneo hayo ambapo amesema katika kushughulikia mgogoro huo wa ardhi ni muhimu taasisi hizo kukaa pamoja katika mazungumzo ambayo hayatoathiri upande wowote wa taasisi na athari kwa wananchi.

Naye afisa wa dawati la malalamiko manispaa ya Kigoma ujiji Ndugu. Melleji Mollel amesema halmashauri imekuwa ikitatua malalamiko ya wananchi na mgogoro huo wa wakazi wa eneo hilo la katosho kando ya reli hatimaye unaelekea kupata suluhu kutokana na taasisi hizo mbili kuwa na lengo moja la kutowaathiri na kuwasumbua wakazi wa maeneo hayo.

Naye katibu wa wahanga hao wa eneo la katosho  Bi. Emelda Albeto ameipongeza halmashauri  ya manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa jitihada na ukaribu ambao wamekuwa wakiuonesha kwa wahanga hao na kusema ujio wa viongozi kutoka shirika la Reli inaonesha ni namna gani tatizo hilo linaenda kuisha na wanaamini taasisi hizo zitazingatia maslahi ya wananchi hao.

Akihitimisha katika ziara hiyo iliyofanyika naibu meya wa halmashauri hiyo Mhe. Athumani Athuman  amesema taasisi hizo mbili zitakaa pamoja na andiko litakwenda kwa mkurugenzi mkuu wa shirika hilo la reli(TRC)  la kuwataka wakazi hao kutovunjiwa  na endapo shirika litahitaji matumizi ya eneo hilo iweze kuwalipa wananchi wa eneo hilo.

picha zaidi ingia katika maktaba ya picha

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa