• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MAPATO YA NDANI YANAVYOTOA TABASAMU KWA WAKAZI WA KIGOMA UJIJI, ZAHANATI NYINGINE MPYA YAFUNGULIWA. New dispensary

Posted on: December 21st, 2023

Na Mwandishi Wetu

Mbunge wa Kigoma Mjini Mhe. Kilumbe Shabani  Ng'enda Leo Desemba 21, 2023 amezindua Zahanati mpya iliyojengwa kwa mapato ya ndani Kata ya Machinjioni Manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa lengo la kuanza kutoa huduma kwa Wananchi.


Akihutubia Wananchi waliohudhuria uzinduzi huo amesema Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kutoa fedha katika kuboresha na kusogeza huduma za afya karibu na Wananchi wa Manispaa hiyo.


Amesema Serikali ya Awamu ya Sita ilitoa kiasi cha fedha za Kitanzania Million Mia tano (Tsh 500, 000,000/=) kwa lengo la upanuzi Kituo cha afya cha Gungu,  Million Mia tano (Tsh 500, 000, 000/=) Ujenzi wa Kituo cha afya cha Buhanda,  Million Mia mbili (Tsh 200, 000,000/=) kukamilisha Ujenzi wa Zahanati ya Kamala ,Kibirizi na Kitongoni na Kiasi cha zaidi ya Billion Moja (Tsh 1, 300, 000, 000/=) kwa Ujenzi wa Hospitali ya Manispaa unaoendelea Kata ya Kagera.


Aidha ameipongeza Halmashauri kwa kuendelea kutekeleza miradi kupitia Makusanyo yake ya ndani ambapo Zahanati imejengwa kwa  fedha za Kitanzania zaidi ya Millioni Mia moja thelathini na nne (Tsh 134,000,000/=), Mapato ya ndani yakiwa ni zaidi ya Million mia moja na ishirini (Tsh 123,000,000/=) na Fedha kutoka Mfuko wa Jimbo Million kumi na Moja ( Tsh 11, 000, 000/=) na Vifaa tiba vikigharimu kiasi cha Million Hamsini (Tsh 50, 000, 000/=).


Akiongea Katika Mkutano huo Meya wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Mhe. Baraka Naibuha Lupoli amesema Baraza la Madiwani limeendelea kutekeleza na kusimamia Miradi ya Maendeleo kupitia Mapato ya ndani kwa kujenga Ofisi za Kata, Uzalishaji Miche ya Michikichi ya Kisasa na Ujenzi wa Zahanati katika kata mbalimbali.


Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Bi. Mwantum Mgonja amesema kuzinduliwa kwa Zahanati hiyo kumefanya Manispaa hiyo kuwa na Zahanati tisa (09) huku akiahidi kusimamia nidhamu ya Watumishi kwa kutoa huduma bora na kuwataka Wanachi kutunza miundombinu iliyopo.


Zaidi endelea Kubofya www.kigomaujijimc.go.tz



Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa