• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MEYA WAMANISPAA YA KIGOMA UJIJI HUSSEIN RUHAVA AFANYA KIKAO NA WAMILIKI WA BAJAJI NA BODABODA, ATATUA CHANGAMOTO INAYOWAKABILI. MAYOR

Posted on: January 19th, 2019

Afisa biashara Festo Nashoni akieleza namna stika itakavyokuwa inafanya kazi na kukomboa mda kwa madereva tofauti na ushuru wa awali.


                                          wamiliki wa bajaji na bodaboda katika kikao na Meya wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji


Na mwandishi wetu.

Meya wa manispaa ya Kigoma/Ujiji Hussein Ruhava jana January 18, amefanya kikao na wamiliki wa bajaji na bodaboda katika ukumbi wa manispaa na kutokana na malalamiko aliyoyapokea ofsini kwake.

Meya huyo akifungua kikao na wamiliki hao mara baada ya kukaribishwa na Afisa biashara wa manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa niaba ya Mkurugenzi Ndugu Festo Nashoni alisema ofsi yake ilipokea malalamiko namna dereva wa bajaji wanavyopoteza mda wakiwa kazini pindi wanapotozwa ushuru wa siku kutokana na kusimama kwa mawala pindi wanapokata risti.

Aliendelea kusema katika kutatua changamoto hiyo aliituma timu ya wataalamu katika kufatilia namna gani wanaweza kutatua changamoto hiyo na kuhakikisha mapato hayapotei, jambo lililofanya wataalamu hao kupitia ofsi ya Mkurugenzi kuja na wazo la kukata stika kwa mwezi kwa lengo la kuleta ufanisi katika kuongeza mapato ya halmashauri na kuwanufaisha madereva na wamiliki wa vyombo hivyo.

Aliendelea kusema  “utaratibu huo wa stika kwa kila mwezi tumeanza nao kuutumia January 2 mwaka huu kwa wamiliki wa bajaji na bodaboda kulipia shilingi za kitanzania elfu kumi na tano (15000/=) na tutahakikisha tunadhibiti watu wote wanalipia stika hizo jambo litakaloondoa usumbufu kwenu ninyi wamiliki na madereva wenu”.

Nao  wamiliki wa vyombo hivyo waliweza kueleza changamoto zinazowakabili , mmoja wa wamiliki na kiongozi wao Ndugu Jumanne Gange alisema wanazo changamoto nyingi pindi wanapokuwa barabarani kwa kudhibitiwa na Askari wa ulinzi na usalama barabarani katika maeneo wanayopakilia abiria jambo linalosababisha kushindwa kufikia malengo yao na kusema kiwango cha ushuru kilichowekwa kwa mwezi ni kikubwa sana kwani sio mara zote madereva wanakuwa barabarani wakifanya kazi hiyo na mara nyingi bajaji hizo hupelekwa katika matengenezo(service).

Naye katibu wa wamiliki wa bajaji na bodaboda maarufu kwa jina la Kibopa alisema hakubaliani na ushuru huo wa Tsh 15000/= kwa mwezi na kutaka ushuru uendelee kutozwa wa Tsh 500/= kwa siku jambo lilioleta majadiliano na mvutano mkubwa katika kikao hicho.

Akitoa ufafanuzi katibu wa kikao hicho na Afisa biashara aliwataka wamiliki na viongozi hao kukubaliana na utaratibu uliowekwa wa kutumia stika kwa mwezi kwani tayari walikuwa wameshakutana na viongozi wao na kuweza kukubaliana na viongozi hao kulidhia utaratibu wa stika jambo linaloleta mvutano kwa viongozi nhao kutokuliana katika kikao hicho.

Naye mmoja wa wajumbe wa kikao hicho mmiliki na dereva  aliyejulikana kwa jina moja Mussa alipongeza jitihada za halmashauri katika kujali na kuweka mzingira mazuri japo alisema kiwango hicho ni kikubwa na kuomba kupunguziwa ushuru huo.

Naye meya wa halmashauri ya manispaa ya Kigoma ujiji alitoa tamko kwamba kuanzia mwezi February wamiliki wa vyombo hivyo watalipia Tsh 13000/=kama msimamo wa halmshauri na kusema kiwango hicho kimezingatia hata siku za matengenezo (service).

Alihitimisha kikao hicho kwa kuwashukuru na kuwapongeza wamiliki hao na kusema wataendelea kukaa pamoja katika kuhakikisha hata baadhi ya changamoto zinatatuliwa  na kuwataka kutii kanuni na sheria za nchi katika uendeshaji wa vyombo hivyo vya moto.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa