• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MGANGA MKUU WA MKOA ASEMA “VYUO NA SHULE MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI VINAFATA HATUA NA TAHADHARI YA KUJIKINGA NA COVID-19” Regional Medical Officer

Posted on: June 2nd, 2020

Na Mwandishi wetu

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dr. Saimon Chacha leo june 2, amefanya ziara katika shule na vyuo vilivyo anza masomo  Manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa lengo la kukagua kama hatua za kujikinga na ugonjwa wa Covid-19 zinachukuliwa kwa walimu na wanafunzi

Mganga mkuu huyo akiwa katika ziara hiyo amesema kwa Mkoa wa Kigoma hakuna Mgonjwa wa Covid-19 huku akiwataka wanafunzi na walimu kutokuwa na hofu katika suala la ujifunzaji na ufundishaji bali waendelee kuchukua tahadhari ya kujikinga na ugonjwa huo

 Akiwa katika chuo cha Uuguzi Maweni amepongeza uongozi wa chuo hicho kwa hatua walizozichukua katika kuhakikisha kila mtu anayeingia na kutoka anahakikisha anapimwa joto la mwili wake na kunawa huku katika madarasa yao wakikaa kwa hatua ya mita moja moja ili kuepukana na msongamano darasani

Aidha Mganga Mkuu ameendelea kuwasisitiza wanafunzi na wanachuo kuepuka suala la kukumbatiana na kubusiana kutokana na wanafunzi na wanavyuo kuwa na mazoea hayo mara wanapokutana mara kwa mara kama marafiki , kunawa maji safi yanayotiririka kwa sabuni na kuvaa barakoa kila mara wanapokuwa darasani

Naye Afisa Elimu Taaluma Mkoa wa Kigoma Ndugu. Omari Mkombole amewataka walimu wanapokuwa wakifundisha  darasani  kuingiza na mada mtambuka kila mara namna ya kujikinga na ugonjwa wa Covid-19 huku wanafunzi wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari Kigoma na Buronge wakiaswa kutumia mda mfupi uliobaki kuelekea mitihani kuutumia kwa usahihi ili kuweza kufanya vizuri katika ufaulu wa  mitihani

Kaimu mkuu wa chuo cha Uhasibu (TIA) Tawi la Kigoma Ndugu. Charles Merengo amesema  tayari wanachuo wa chuo hicho wamepatiwa mafunzo ya kujikinga na ugonjwa wa Covid-19 na wanafunzi wote na walimu hupimwa joto la mwili kila  wanapoingia katika chuo hicho , ameendelea kusema kwa sasa ratiba ya masomo imerekebishwa awali ratiba iliishia saa nane na kwa sasa ratiba mwisho saa kumi na mbili jioni  kutokana na kupunguza idadi ya  wanafunzi darasani kwa wakati mmoja

 Mwanachuo wa chuo cha Uuguzi Maweni Bi. Jackie Kazinga amesema wao kama wanachuo wanachukua tahadhari ya kujikinga na ugonjwa wa Covid-19 kwa kunawa maji safi yanayotiririka, kuvaa barakoa na kukaa darasani kwa umbali unao takiwa

Pia   mwanachuo wa Chuo cha Uhasibu (TIA)  Ndugu. Hassan Kigongo amesema tayari masomo yameanza chuoni hapo na wanachukua tahadhari zote katika ujifunzaji kwa kuhakikisha wanachukua tahadhari ya kujikinga na Ugonjwa wa Covid-19 na tabia za kukumbatiana na kubusiana kama zilivyokuwa awali

Mei 21,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli alisema vyuo vikuu vyote vitarejea katika hali yake ya kawaida ya kuendelea na masomo kuanzia June mosi baada ya kujiridhisha kutokana na maambukizi ya virusi vya Ugonjwa wa Covid-19 kupungua Nchini Tanzania

 

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa