• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MICHE YA MICHIKICHI YA KISASA YAGAWIWA BURE KWA WAKULIMA, YAANZA KUPANDWA KANDO ZA BARABARA ZA MJI MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI , Palm tree

Posted on: November 25th, 2020

Na mwandishi wetu

Uzinduzi wa ugawaji miche ya michikichi ya kisasa kwa wakulima umefanyika leo Novemba 25, kwa kugawa bure miche elfu kumi na moja (11,000) kwa wanufaika na wakulima mia moja na hamsini huku zoezi la upandaji wa miche hiyo kando ya barabara za mji ukifanyika

Katika uzinduzi huo Mgeni Rasmi na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Mwailwa Pangani amewataka wakulima kuhakikisha wanaitunza miche hiyo na kuihudumia mashambani ili kuendeleza ubora wa uzalishaji wa mawese kwa kiwango cha juu na kuepukana na uagizaji wa mafuta ya mawese nje ya Nchi

Aidha mkurugenzi huyo amezitaka kaya na familia ambazo miche hiyo imependwa na itapandwa kando ya barabara za mji kuhakikisha miche hiyo inasitawi kutokana na gharama ya uzalishaji kuwa kubwa na sera iliyopo kuhakikisha Manispaa ya Kigoma/Ujiji inakuwa ya kijani kwa kustawisha zao hilo

Kaimu Mkurugenzi wa kituo cha utafiti wa kilimo Kihinga (TARI) Ndugu. Kuzenza Madili Amewataka wakulima kuhakikisha wanatunza miche hiyo ili kufikia lengo la uzalishaji wa mawese kwa kiwango cha juu huku akiwataka Maafisa Ugani kuwafatilia na kuwapa ushauri wakulima katika ukuzaji wa zao hilo

Naye Kaimu Mkuu wa idara ya Kilimo, Ushirika na Umwagiliaji Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Haruna Mtandanyi amesema Manispaa hiyo ina lengo la Kuzalisha miche Millioni Moja (1,000,000) ambapo kwa sasa tayari Miche Elfu thelathini (30,000) imeshazalishwa na utengaji wa bajeti ya uzalishaji wa miche iliyobaki umefanyika

Ameendelea kusema miche hiyo itagawiwa kwa awamu mbili ambapo kwa sasa wanufaika wengine ni pamoja na Taasisi tano (05) za serikali na barabara tatu(03) za mji za kiwango cha lami huku mwezi Februali 2021, ugawaji awamu ya pili miche elfu kumi na tisa(19,000) utafanyika na wakulima mia tatu na ishirini(320), taasisi tatu(03) na barabara nne (04) za lami za mji zikipandwa miche hiyo kando ya barabara

Bi. Shani Sasilo Mkulima wa bonde la Mto Ruiche ameipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuja na mkakati wa uzalishaji wa mafuta ya mawese kwa kiwango cha juu na kulifanya zao la michikichi kuwa la kimkakati huku akisem mpango huo wa Serikali utafanya wakulima kujikomboa kwa kupata mafuta yaliyobora kutokana na miche hiyo

Katika Hotuba ya Rais Dr. John Pombe Magufuli akifungua Bunge la kumi na mbili (12) alilitaja zao la Michikichi kama zao la kimkakati ambalo litasaidia uzalishaji wa mafuta ya mawese kwa kiwango kikubwa ,miche hiyo ya kisasa ikiwa na uwezo wa kuzalisha Tani 4.5 hadi Tani 5 kwa hekta kwa mwaka ambalo litapelekea kuepuka uagizaji wa mafuta hayo Nchini Malaysia na Nchini Burundi ambapo zaidi ya fedha za Kitanzania Billion 445 hutumika kila mwaka kuingiza mafuta hayo 

picha na video zaidi ingia maktaba ya picha www.kigomaujijimc.go.tz

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa