• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MILLION 960 ZA RAIS SAMIA, NAMNA ZITAKAVYOWANUFAISHA WAKAZI WA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI, Buildings

Posted on: October 21st, 2021

Na mwandishi wetu

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan imeendelea kutekeleza mipango na mikakati mbalimbali  katika Sekta ya Afya na Elimu Mkoani Kigoma ambapo jumla ya fedha za Kitanzania Shilingi billion kumi na tano million mia nane themanini ( 15,880,000,000/=) zimetengwa katika ujenzi wa Miradi hiyo

Manispaa ya Kigoma/Ujiji tayari imepokea fedha za Kitanzania Shilingi million mia tisa sitini (960,000,000/=)  ikiwa ni fedha kutoka Serikali Kuu na ni mpango wa Rais wa Tanzania kuinua Uchumi wa Watanzania kutokana na athari za Uviko-19 zilizojitokeza duniani kote

Kiasi cha fedha hicho kinatarajia kutumika katika Ujenzi wa Madarasa arobaini na nane (48) kwa shule kumi na sita (16)  za sekondari zilizopo Manispaa ya Kigoma/Ujiji ambapo jamii itahusika katika ujenzi wa madarasa hayo

Fedha hizo zilizotolewa zinatarajia kuleta manufaa  kwa Wananchi na  Wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji ambapo miongoni mwa faida zinazotarajia kupatikana ni pamoja na;-

Ajira kwa Wananchi na wakazi wa Manispaa ya Kigoma, zaidi ya ajira mia tisa sitini (960) zinatarajiwa kuzalishwa katika kipindi chote cha  ujenzi wa madarasa utakapokuwa ukiendelea ambapo kwa kila darasa linatarajia kugharimu kiasi fedha  Million ishirini (20,000,000/=) na kuzalisha  ajira ya watu Kumi na tano hadi ishirini(15-20)

Kuongezeka kwa mzunguko wa fedha,  ununuaji na usambazaji wa  bidhaa mbalimbali kama vile ununuzi wa mawe, Mchanga, kokoto, cementi, mbao, mabati, na vifaa vingine vya ujenzi  unatarajia kuongezeka kutokana na kuhitajika katika ujenzi huo  ikiwa ni pamoja na upakiaji, upakuaji na usafirishaji wa vifaa hivyo na kufanya uwepo wa mzunguko wa fedha kwa haraka

Kukua kwa Uchumi wa Wananchi na Wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji, katika kipindi chote cha ujenzi ajira mbalimbali zitazalishwa ambapo idadi kubwa itakuwa ikijishughulisha kufanya kazi ambapo makundi mbalimbali kama vile, mafundi uashi, Ujenzi, Vibarua na mama/Baba lishe watajiongezea kipato na kufanya uchumi wa mtu mmoja mmoja, familia na hata jamii kukua

Kuboreshwa kwa miundombinu ya Kujifunzia na Kujifunzia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati akizungumzia usimamizi wa fedha hizo  aliwataka wataalamu kusimamia miundombinu ya ujenzi  katika viwango vinavyofaa ambapo alitamka kuwa hatakuwa na huruma kwa mtu atakaye tumia fedha hizo kwa kujenga katika viwango vya chini , hivyo tunatarajia miundombinu itakayokuwa katika viwango vinavyokubalika na kuwa kivutio kikubwa kwa wanafunzi na walimu katika tendo la ufundishaji na Ujifunzaji

Idadi kubwa ya wanafunzi kupata nafasi ya Kujiunga na elimu ya upili, kumekuwa na ongezeko la ukuaji wa ufaulu kwa mitihani ya mwisho kwa wanafunzi wa darasa la saba kutoka ufaulu wa asilimia themanini (80%)  kwa mwaka 2016 hadi ufaulu wa asilimia themanini na sita (86%)  kwa mwaka 2021 hivyo ujenzi wa miundombinu hiyo itakuwa chachu ya idadi kubwa ya wanafunzi kujiunga na elimu ya upili kutokana na uwepo wa miundombinu bora

Kiwango cha elimu na ufaulu kwa wanafunzi wa shule za Upili kuongezeka, katika madarasa yatakayojengwa Manispaa ya Kigoma/Ujiji wanafunzi watakuwa wakijifunza katika mazingira bora kwa kiwango kinachofaa kama vile ukaaji darasani hivyo kufanya wanafunzi kujifunza katika mazingira yatakayofanya kupata kiwango kikubwa cha elimu na kuleta matokeo chanya kwa jamii na hata kukua kwa ufaulu wa wanafunzi katika mitihani yao

Kuwa na jamii kubwa iliyoelimika, kukamilika kwa ujenzi ya madarasa hayo kutafanya idadi kubwa ya wanafunzi wa wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji kujiunga na masomo ya upili na kuwa na idadi kubwa ya watu walioelimika na elimu hiyo kuitumia katika maisha ya kila siku na kufanya kuwa na jamii iliyoendelea katika nyanja mbalimbali

Madarasa hayo yanatarajia kujengwa kwa shule za Sekondari Buteko, Kitwe, Buhanda, Buzebazeba, Gungu, Buronge, Bushabani, Kigoma-Ujiji,Kitongoni, Kichakachui, Kirugu, Katubuka, Masanga, Mwananchi, Rubuga, na Shule ya sekondari Rusimbi

Taarifa zaidi endelea kufuatilia taarifa zetu kupitia  www.kigomaujijimc.go.tz

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa