• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MKURUGENZI MPYA WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI AONGEA NA WATUMISHI WOTE WA OFSI KUU KWA MARA YA KWANZA, AWATAKA WATUMISHI KUTII SERIKALI ILIYOPO MADARAKANI.

Posted on: August 31st, 2018

Mkurugenzi mpya wa halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji Ndugu. Mwailwa S. Pangani ameongea leo August 31, na watumishi wote wa ofsi kuu katika ukumbi wa halmashauri huku akiwataka watumishi wote kufanya kazi kwa waledi ikiwa ni pamoja na kuheshimu serikali ya tano iliyoko madarakani.

Ameyasema hayo katika mkutano wa watumishi akiwa na wakuu wa idara wakiongozwa chini ya Afisa Utumishi  Ndugu. Berneth Ninalwo ambapo mkurugenzi huyo amesema lengo kuu ni kufahamiana na watumishi wote na kuzungumzia namna ya utendaji kazi katika halmashauri.

Mkurugenzi huyo ameendelea kuwataka watumishi kutoa ushirikiano katika shuguli zinazofanyika kila siku na kuzifanya kazi kwa weledi mkubwa ili kuweza kuondokana na tatizo la kupata hati chafu kwa miaka mitatu mfululizo jambo ambalo linatia aibu kwa halmashauri zingine nchini.

Akizungumzia changamoto inayozungumzwa ya hati chafu ikiwa ni mwingiliano wa wanasiasa na wataalamu amesema tatizo sio wanasiasa tu lakini pia wataalamu wamekuwa ni tatizo kubwa kutokana na namna wanavyofanya kazi kwa uzembe na kufika kazini kwa mda wanavyotaka jambo ambalo ni hatari kwa maendeleo ya manispaa hiyo, mkurugenzi huyo anasema “wanasiasa sio tatizo sana hata ninyi wataalamu mnasababisha, kwani suala la mapato wanasiasa ndio wanaokusanya?, hivyo nawaomba tufanya kazi kwa weredi”.

Akiendelea kuongea amewataka watumishi hao kuitii serikali iliyoko madarakani hata kama mtumishi atakuwa na itikadi tofauti kwa kuwataka watumishi kuwahi kazini kwa wakati na kuondoka kwa wakati kutokana na sheria na kanuni za utumishi wa umma zinavyotaka ikiwa ni pamoja na kuvaa mavazi ya heshima  kwa kila mtumishi ili kuleta ufanisi mzuri katika utendaji kazi.

Ameendelea kuwataka watumishi hao inapotokea tatizo la aina yeyote kufika ofsini na kutafuta namna ya kufanya utatuzi wa matatizo mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuacha majungu katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku.

Naye afisa utumishi Ndugu. Berneth Ninalwo katika mkutano huo amempongeza Mkurugenzi huyo kwa hatua nzuri aliyoanza nayo katika kuongea na watumishi wote kwa lengo la kuleta ufanisi katika kazi na afisa utumishi huyo amemuahidi mkurugenzi kutoa ushirikiano kwa watumishi wote waliopo chini yake na kusema kwa yale yote aliyoyaagiza yatasimamiwa ili kuleta ufanisi katika kazi.

Naye Ndugu Shabani mashaka na Meleji Mollel watumishi wa halmashauri hiyo wameweza kutoa pongezi kwa mkurugenzi huyo kwa kuteuliwa na Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kumtaka mkurugenzi huyo kushugulikia masilahi ya wafanyakazi, upotevu wa mapato, na masuala ya hati chafu jambo ambalo linaichafua halmashauri hiyo.

Naye mkurugenzi huyo amehitimisha kwa kuwashukuru watumishi wote hao kwa kuhudhulia katika mkutano huo na kusema maoni yaliyototewa atayafanyika kazi kadri ya uwezo wake na kuwataka kuwa na upendano pamoja na ushirikiano  katika majukumu ya kila siku ili manispaa iweze kusonga mbele.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa