• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MKUU WA MKOA WA KIGOMA MHE. EMMANUEL MAGANGA AMEWAAPISHA WAKUU WA WILAYA YA BUHIGWE NA KASULU, AWAOMBA WANASIASA WANAOKWAMISHA UKUSANYAJI MAPATO MANISPAA YA KIGOMA UJIJI KUACHIA MADARAKA.

Posted on: August 6th, 2018

Mkuu wa mkoa mhe. Emmanuel  Maganga amewataka madiwani wa halmashauri ya manispaa ya kigoma ujiji wanaoshindwa kufanya kazi kwa weledi kuachia madaraka kutokana  kulalamikia masuala ya posho.

Ameyasema hayo leo August 6 katika hotuba aliyoitoa baada ya kumwapisha mkuu wa wilaya ya Buhigwe mhe. Kanali Simon Mahenge  na mkuu wa wilaya ya Kasulu mhe. Luteni Kanali Michael Masala katika eneo  la mikutano mkoani hapo. Amesema mapato ya halmashauri ya manispaa yapo chini kwa asilimia 43% jambo ambalo ni hatari na kusema wanaokwamisha ni madiwani wanaoleta migogoro na marumbano wanayoyafanya kwa wataalamu waliopo.

Katika sherehe hizo za kuwaapisha wakuu wa wilaya ya Buhigwe na Kasulu,  amewataka pia wakuu wote wa wilaya zote za mkoa wa Kigoma kuwashugulikia  kisheria wale wote wanaokwamisha shuguli za ukusanyaji mapato  wakiwemo wanasiasa.

Lakini pia amewakumbusha viongozi hao na viongozi wengine wajibu wa kiongozi ikiwa ni pamoja na kukubaliana na mazingira, kuwapenda wananchi , na kutompuuza mtu yeyote ikiwa ni pamoja na kuwa tayari kuwasikiliza wananchi na kutatua changamoto zao .

Ameendelea kuwataka viongozi hao walioapishwa kuwa watiifu kutokana na kiapo na tamko walilosaini mbele ya wakazi wa mkoa wa Kigoma, huku akisema wenye mamlaka kubwa ni wananchi katika eneo lakini pia ndio wasimamizi wakubwa wa katiba,

“msifanye kazi kwa maonyesho bali fanyeni kazi kwa mjibu wa katiba, sheria,na miongozo, msifanye kazi kwa woga , hakuna mtu yeyote mkubwa zaidi yako wewe mkuu wa wilaya, simameni imara, ila sio kwa ubavu bali kwa kufuata taratibu” ameyasema mkuu wa mkoa katika kusisitiza utekelezaji wa majukumu kwa wakuu wa wilaya hao.

Katika hotuba hiyo mkuu wa mkoa amewataka viongozi na wananchi kuendelea kusimamia kila mmoja majukumu yake katika masuala ya usafi wa mazingira,kuendelea kufanya shuguli za kilimo, biashara wakitumia fursa za masoko yaliyopo nchi jirani Burundi na Rwanda.

Mkuu wa mkoa huyo amepongeza suala la ulinzi na usalama wa mkoa licha ya kusema kuna mapungufu madogo ya mauaji yanayoendelea ya mtu mmoja mmoja huku akiwataka viongozi wa  kamati ya ulinzi na usalama mkoa kusimamia na kufanya msako wa wahamiaji haramu, na akiwataka wakazi wa mkoa wa Kigoma kutowahifadhi wahamiaji ambao wanaingia nchini kinyume cha utaratibu.

Akizungumzia suala la vitambulisho vya kitaifa mkuu huyo wa mkoa wananchi wameandikishwa lakini si kila aliyeandikishwa anaweza kupata kitambulisho hicho kutokana na lindi kubwa la wahamiaji haramu na kusema mtu asiyepata kitambulisho na arijiandikisha ajiandae kurudi alipotoka.

Kabla ya hotuba hiyo ya mkuu wa mkoa katibu tawala mkoa ambaye ni mgeni mkoani hapo alijitambulisha kwa wote waliohudhulia sherehe hizo na kumshukuru Rais wa jamhuri ya muungano wa  Tanzania kwa kumteua katika nafasi hiyo na kuahidi kuifanyia kazi kwa weledi na kuomba ushirikiano mkubwa kwa viongozi na wananchi.

Katibu tawala huyo amejitambulisha na kusema  yeye ni mtaalamu wa masuala ya mawasiliano na mifumo lakini pia akiwa na uzoefu wa miaka 18 katika usimamizi wa mambo ya kifedha pamoja na mabenki, Amemaliza kwa kuahidi kufanya kazi kwa weledi kwa kusimamia sheria, sera na katiba.

Nao wakuu wa wilaya wakiongea baada ya kuapishwa, mkuu wa wilaya ya Kasulu  mhe. Luteni Kanali Michael Masala ameahidi kutoa ushirikiano kwa wananchi na kuwataka wananchi nao kumpa ushirikiano.

Naye mkuu wa wilaya ya Buhigwe  mhe. Kanali Simon Mahenge ameahidi ushirikiano wa wananchi wa wilaya hiyo na kuahidi kuwa wazi katika kuijenga wilaya hiyo.

Naye mkuu wa mkoa amehitisha amehitimisha kwa kuwashukuru wote waliohudhulia katika sherehe hizo,na kuwataka kila mmoja kwa nafasi kufanya juhudi kwa kuendeleza mkoa wa Kigoma. 

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • WAJASIRIAMALI WAENDELEA KUFIKIWA NA WATAALAMU KIGOMA UJIJI. Social services

    May 30, 2025
  • UGAWAJI WA VYANDARUA BURE UNAENDELEA KWENYE VITUO KIGOMA UJIJI. Health protection

    May 29, 2025
  • WAJASIRIAMALI KIGOMA UJIJI WATEMBELEWA NA WATAALAMU.

    May 28, 2025
  • RC ANDENGENYE AZINDUA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA MKOA WA KIGOMA. Malaria protection

    May 28, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa