• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MKUU WA MKOA WA KIGOMA MHE. THOBIAS ADENGENYE AFANYA ZIARA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI, AWATAKA WATUMISHI YA UMMA KUWA WAAMINIFU NA WAADILIFU, Regional Commisioner

Posted on: September 9th, 2020

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe.Thobias Andengenye  amewataka watumishi wa serikali waliopo Mkoani hapo kutatua matitizo ya wananchi na kusimamia miradi inayoendelea kujengwa kwa waledi

Ameyasema hayo leo Septemba 9,2020 alipokuwa katika ziara aliyoifanya Manispaa ya Kigoma/Ujiji na kufanya kikao na watumishi wa Manispaaa hiyo pamoja na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

Akiwa katika Manispaa hiyo ametembelea miradi miwili Mradi wa Ujenzi wa Chanzo cha Maji na Mradi wa Ujenzi wa jengo la upasuaji na wodi ya wazazi kituo cha Afya cha Gungu ambapo amejionea hatua za ujenzi wa miradi hiyo ilipofikia

Akiwa katika Mradi wa Ujenzi wa Chanzo cha maji Mkurugenzi wa Maji safi na Maji Taka(KUWASA) Manispaa ya Kigoma/Ujiji Eng. Jonas Mbike akitoa  taarifa ya  Amesema ujenzi wa   Mradi huo  umekamilika kwa asilimia tisini na tatu (93%) ambapo una uwezo wa kuhudumia wakazi 384,501 ambapo kwa sasa kadrio la wakazi wa Manispaa hiyo ni Watu 254,368

Ameendelea kusema mradi huo  umeanza kufanya kazi ambapo tayari matanki mapya  sita (6) na matanki matatu (3) yaliyokuwepo(zamani)  yanaendelea kufanya kazi huku uzalishaji ukiwa ni Lita Million kumi na nane (18,000,000) kwa siku na mahitaji kwa wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji yakiwa ni Lita Million ishirini na tatu (23,000,000) kwa siku

Mkurugenzi huyo amesema kwa sasa maeneo mengi ya Mji maji yanapatikana kwa kiwango kikubwa katika maeneo ya makazi ya watu, na kufikia mwezi Oktoba mwaka huu tatizo la maji litakuwa limeisha kutokana na uzalishaji utakao kuwa ukiendelea kwa kuzalisha Lita Million mia moja arobaini na mbili (142,000,000) na mahitaji yakiwa Lita Million ishirini na tatu (123,000,000) ambapo wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma wataanza kunufaika na mradi huo pia

Aidha Mkuu wa Mkoa huyo akipokea taarifa ya Ujenzi wa Jengo la Upasuaji na wodi ya wazazi katika kituo cha afya cha Gungu, Msomaji wa taarifa hiyo na Mtendaji wa Kata ya Gungu Bi. Mwavita Lusovu amesema mapema Mwezi Desemba, 2019 Serikali Kuu ilileta fedha Tsh million Mia mbili (200,000,000)/= kwa ajili ya ukarabati wa Majengo yaliyopo katika kituo hicho cha Afya ambapo Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo iliona inafaa katika ujenzi wa majengo mapya hayo

Ameendelea kusema  katika ujenzi huo mradi huo umefikia Asilimia Sabini na Tano (75%) ambapo mradi huo unatarajia kugharimu kiasi cha Fedha Tsh Million 263,135,180/= hadi kukamilika kwake, na kiasi cha Tsh Million 63,135,180/= kinatarajiwa kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo

Naye Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Ndugu. Mwailwa Pangani Amesema kukamilika kwa ujenzi wa  Jengo la wodi ya wazazi na Jengo la Upasuaji kutaondoa usumbufu na ukosefu wa majengo hayo hali itakayosaidia akina Mama kuhudumiwa pindi wanaposhindwa kujifungua kwa njia ya Kawaida

Naye Mkuu wa Mkoa huo amepongeza jitihada na usimamizi uliofanyika katika kusimamia miradi hiyo itakaoweza kuwa manufaa kwa wananchi na Wakazi wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma na Manispaa ya Kigoma/Ujiji huku akiwataka Viongozi na Watumishi wa Serikali kuendelea kusimamia miradi kwa weledi

Mkuu huyo wa Mkoa amehitimisha kwa kuendelea kuwataka watumishi wa Umma kuwa waaminifu na waadilifu katika kuwatumikia wananchi na kujenga taswira chanya kwa kupenda shughuli na maeneo wanayofanyia kazi

Mkuu huyo wa mkoa yupo katika ziara ya kutembelea wilaya na Halmashauri zote akiambatana na kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa  ambapo anafanya ziara yake akiwa katika Mavazi yake ya Askari ambapo awali alikuwa katika utumishi katika idara hiyo


Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa