• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MKUU WA WILAYA YA KIGOMA NDUGU SAMSONI ANGA AUNDA KAMATI YA KUFUATILIA NA KUONA MPAKA UNAOTENGANISHA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI NA HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA, AWATAKA WANANCHI KUFUATA MAAMUZI YALIYOPITA NA KUHESHIMU SHERIA YA NCHI.

Posted on: November 16th, 2018

Mkuu wa wilaya Ndugu Samsoni Anga juzi ameunda kamati ya kufuatili mpaka unaotenganisha halmashauri ya manispaa ya kigoma ujiji na halmashauri ya wilaya ya Kigoma ili kuondoa migogoro na minongono baina ya viongozi wa halmashauri hizo.

Ameyasema hayo katika kikao cha kamati  ya ushauri wa wilaya (DCC) uliofanyika juz nov 14, katika ukumbi wa halmashauri ya manispaaya Kigoma Ujiji ambapo alikuwa amezikutanisha halmashauri zote mbili , hoja hiyo iliwasilishwa na ofsi ya Mkurugenzi halmashauri ya wilaya ya Kigoma kama agenda katika kikao hicho.

Akisoma taarifa hiyo mkurugenzi wa halmashauri hiyo Ndugu. Upendo anasema  “kwa mda mrefu halmashauri ya wilaya ya Kigoma imeendelea kufahamu kwamba mpaka unaototenganisha Halmashauri ya Kigoma na manispaa ya Kigoma/Ujiji sehemu ya mwandinga unaopita mto ntovye na kuvuka barabara ya Kigoma-kasulu na kuendelea mto huo hadi relini kasha kufuata reli kuelekea mashariki.”

Aliendelea kuzungumzia chanzo cha mgogoro huo alisema  “upimaji uliofanyika awali  kisheria ulikosewa kwa kutaja mpaka unaotenganisha halmashauri ya  wilaya ya Kigoma na halmashauri ya manispaa ya Kigoma/ Ujiji ni eneo la mwandinga unafuata mto Ntovye na kwenda hadi barabara ya Kigoma-Uvinza, kisha kuelekea mashariki kufuata barabara hiyo ya Kigoma-Uvinza hadi kwenye daraja la mto Mugonya kuelekea kusini kufuata mto mungonya .”

Katika kikao hicho Mkuu wa wilaya aliuliza Naibu meya Athuman Juma Athumani kama mgogoro huo anaufahamu jambo alililosema mgogoro huo haujui na halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji haina mgogoro wowote na Halmashauri ya wilaya ya Kigoma, lakini mipaka iliyodhibitishwa kisheria ndio sahihi na ndio halmashauri inaitambua.

Wakichangia baadhi ya wajumbe katika kikao hicho juu ya mgogoro huo baadhi ya wajumbe akiwemo Frank Ruhasha anasema  “mgogoro huo haupo halmashauri  ya wilaya ya Kigoma ndio inayoibua mgogoro huo na sharti sheria ifuatwe kama maamuzi ya  awali yaliyoamuliwa  licha ya watu kuwa na historia tofauti tofauti.”

Naye mkuu wa wilaya akizungumzia mgogoro huo aliwajulisha wajumbe wa kikao hicho kwamba mwenye ardhi ni serikali na serikali imeshatoa maamuzi hivyo wajumbe wote na wakazi wa halmashauri zote mbili waheshimu sheria ambayo tayari imetumika kufanya maamuzi.

Katika hitimisho la mgogoro huo alioufanya aliweza kuunda kamati ya watu 17 kwa ajili ya kufuatilia na kuona mpaka huo kwa makubaliano ya meya na mwenyekiti wa halmashauri hizo mbili ambapo alitaja wajumbe watakao husika katika mpaka huo ni pamoja na Meneja TARURA 1 kutoka katika kila halmashauri, meneja TANROAD 1,Meya wa manispaa ya kigoma ujiji, Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kigoma, wakurugenzi wa halmashauri zote, viongozi wa mipango miji kutoka kila halmashauri, kiongozi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) mmoja na wawakilishi wa wananchi 2 kutoka katika kila halmashauri.

Katika kikao hicho cha mashauri agenda zingine zilizowasilishwa kutoka katika halmashauri zote mbili ni pamoja na Taarifa za mapato ya ndani, miradi iliyotekelezwa, ambapo kwa manispaa miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa matundu ya vyoo shule ya msingi kibirizi iliyogharimu Tsh million 50,  ujenzi wa madarasa tisa na matundu ya vyoo katika shule ya msingi kigoma iliyogharimu Tsh milioni 200, na ujenzi wa madarasa shule ya msingi airport uliogharimu Tsh millioni 60, agenda zingine zilizowasilishwa ni utekelezaji wa kunusuru kaya masikini (TASAF).

Akihitimisha kikao hicho alizitaka halmashauri zote kufanya na kuweka  mikakati ya kukuza mapato ya halmashauri ili kuweza kusuka gurumu la maendeleo kwa wakazi wa Kigoma na aliendelea kuwataka watumishi  wote kuwa waadilifu katika shughuli za kila siku.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa