• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MSIMAMIZI WA UCHAGUZI WA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI AANZA KAZI KWA KISHINDO BAADA YA KUAPISHWA, ATOA TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MITAA KATIKA HALMASHAURI YAKE. Election leader

Posted on: September 13th, 2019

Msimamizi  wa uchaguzi wa serikali za mitaa halmashauri ya manispaa ya Kigoma/Ujiji ndugu. Emmanuel Katemi jana September 12, mara baada ya kuapishwa kushika wadhifa huo alikutana na watendaji wa kata na watumishi wa ofisi kuu ya mkurugenzi wa halamshauri  katika ukumbi wa halmashauri hiyo.

Msimamizi huyo wa uchaguzi wa serikali za mitaa alikutana nao akiwa na mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Mwailwa Pangani kwa lengo la kumtambulisha kwa watendaji hao wa kata na watendaji wengine wa ofisi kuu ya mkurugenzi huyo

Mara baada ya kutambulishwa na mkurugenzi wa halmashauri hiyo aliongea  na watendaji hao wa serikali kwa  lengo la kuwakabidhi tangazo la majina  na  mipaka ya mitaa iliyopo katika halmashauri hiyo kwa lengo la kuifikisha katika ofisi za kata ambapo tangazo hilo wataliotoa leo September 13 kwa mjibu wa ratiba.

 Msimamizi wa uchaguzi huo alisema amefanya hivo kwa kuwa ni majukumu yake chini ya kanuni ya 5 ya kanuni za uchaguzi wa mwenyekiti wa mtaa na wajumbe wa kamati ya mtaa, Tangazo la serikali Namba 372 la tarehe 26/2/2019  pamoja na kanuni za uchaguzi wa mwenyekiti wa kijiji, wajumbe wa Halmashauri ya kijiji  na mwenyekiti wa kitongoji katika mamlaka za miji, tangazo la serikali Namba 374 la Tarehe 26/4/2019 na kwa kuzingatia orodha  ya mitaa, vijiji na vitongoji vilivyotangazwa  kwenye  gazeti la serikali namba 536 la tarehe 19/7/2019.

Aliendelea kuwataka watumishi hao  watakaoshiriki katika baadhi ya shughuli hizo za uchaguzi  wa serikali za mitaa kumpa ushirikiano  na kuwa waadilifu katika utumishi wao na kuzingatia kanuni na miongozo ya uchaguzi wa serikali za mitaa  na kila jambo kufanyika kwa wakati kwa kutokana na ratiba iliyopangwa.

Naye afisa uchaguzi wa manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Mrisho Bukuku alisema tayari maandalizi yako vizuri kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na baadhi ya vifaa vipo na kwa ajili ya shughuli hiyo huku akisema atawakabidhi watendaji wa kata gundi ya kubandikia tangazo hilo alilolitoa msimamizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa.

Aliendelea kusema vituo vya kupigia kura vitakuwepo katika taasisi za umma katika mitaa iliyopo huku akisema maeneo ambayo yatawekwa vituo yasiyo na taasisi za umma itakuwa jukumu la kushauriana baina ya msimamizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa na vyama vyote vya siasa vitakavyoshiriki uchaguzi huo.

Nao baadhi ya watendaji kata waliokabidhiwa tangazo la majina na mipaka ya mitaa Ndugu. Amesema  wamempongeza msimamizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa kwa kuteuliwa huku akisema wapo tayari kumpa ushirikiano katika shughuli hiyo itakayofanyika na kumuahidi kufanya kazi hiyo kwa uadilifu.

Msimamizi huyo wa uchaguzi wa serikali za mitaa ameteuliwa kati ya wasimamizi 184 waliochaguliwa nchi nzima kwa mjibu kwa mujibu wa Kifungu 201A, cha Sheria za Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya), Sura 288 zikisomwa pamoja na Kanuni ya 3 na 6(6) ya Kanuni za Uchaguzi wa Viongozi na Mitaa za Mwaka 2019 zilizotolewa kwa Tangazo la Serikali Namba 371, 171 na 374 ya mwaka 2019.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa