• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MKURUGENZI WA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI NDUGU. MWAILWA PANGANI AELEZA MAKUBWA YALIYOFANYWA NA SERIKALI YA AWAMU YA TANO KATIKA MANISPAA HIYO, 5 YEARS

Posted on: August 28th, 2020

Na Mwandishi Wetu

Katika kipindi cha miaka mitano inayoongozwa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dr. John Pombe Magufuli ameweza kufanya miradi mingi katika kuboresha miundombinu  ndani ya  Manispaa yetu, hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu Mwailwa Pangani mapema wiki hii alipokuwa akifanya mahojiano na wandishi wa habari

Akiiongea kwa ujumla wake Mkurugenzi huyo alisema Serikali ya Awamu ya Tano imefanya mabadiliko ya kiutendaji katika kuhakikisha maadili ya wafanyakazi  yanaimarishwa, kusimamia miradi katika hali ya viwango na kupinga na kukataa Rushwa hali iliyofanya kukua na kuendelea kuboreshwa kwa miundombinu na kuweka mazingira mazuri katika shughuli za biashara, Kilimo na hata ufugaji katika Manispaa hiyo

Mkurugenzi huyo aliendelea kusema katika kipindi cha Miaka Mitano, Serikali ya Awamu ya Tano imeweza kuboresha  katika sekta ya Afya ambapo upatikanaji wa huduma za dharura zimeendelea kutolewa katika vituo vya afya ambapo katika kituo cha Afya cha Ujiji huduma ya Upasuaji imeendelea kutolewa huku kituo cha Afya cha Gungu ukarabati na ujenzi wa jengo la Upasuaji na Wodi ya wazazi ukiendelea kukamilika kwa fedha zilizotolewa na serikali hiyo kiasi cha Tsh Million mia mbili(200,000,000/=) huku wakazi wa Manispaa hiyo 448 wakiunganishwa na CHF iliyoboreshwa ambapo wanaweza kutibiwa katika vituo vyote vya Mkoa Mzima ukilinganisha na kwa Mwaka 2015 ambapo wanachama wa bima walitibiwa katika kituo cha afya au zahanati walizokatiwa bima hizo

Akitoa takwimu za uboreshaji katika sekta ya Elimu Mkurugenzi huyo alisema kwa kipindi cha serikali ya awamu ya tano Jumla ya madarasa sabini na tatu(73) , matundu ya vyoo mia moja ishirini na tano (125),Bwalo moja (1), na  nyumba za walimu 4,  ujenzi wa maabara 11 zikikamilika na maabara 46 zikiendelea kukamilishwa  huku  baadhi ya nyumba za walimu zilizopo shule ya Msingi Mgumile zikiunganishwa na mfumo wa umeme wa jua kwa upande wa Elimu Msingi ambapo jumla ya Billion 2,877,671,370.00/= zilitumika huku Jumla ya Tsh Million 250,959,030.00/= zikitumika upande wa Elimu Sekondari

Aidha aliiendelea kusema idadi ya wanafunzi wa awali walioandikishwa katika kipindi cha Awamu ya Tano imeongezeka kwa asilimia 124%  kutoka wanafunzi 4000 kwa mwaka 2015 hadi kufikia  wanafunzi 4949  mwaka 2020 na jumla ya wanafunzi 3288 walijiunga na  kidato cha kwanza kwa mwaka 2020 sawa na ongezeko la asilimia 83 ukilinganisha  mwaka 2015 ambapo wanafunzi 1732 sawa na asilimia 60 ndio waliojiunga na kidato cha kwanza

 Akieleza miundombinu ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami alisema serikali imeweza kuboresha mitandao ya barabara  za mitaani kwa kiwango cha lami ambapo jumla ya Km 13.75 zimejengwa  kwa Gharama ya Tsh Billion 20.02/= ukilinganisha kwa kipindi cha awamu zingine zilizopita  huku akiendelea kusema  Serikali inaendelea kutekeleza ujenzi  wa barabara za mitaani katika kata zote kumi na tisa chini ya mamlaka ya TARURA ili kuweza kuboresha miundombinu na makazi ya wakazi wa Manispaa hiyo

 Katika kuboresha  sekta ya Mifugo na Uvuvi, Serikali ya awamu ya Tano imeweza kuboresha miundombinu katika Mwalo wa Kibirizi ambapo jumla ya Fedha za Kitanzania Jumla ya Tsh Million 447,292,077.00/= zimetumika katika ujenzi wa soko la kuuzia samaki, kuongeza chanja za kuanikia samaki na dagaa , mitamboo ya kuzalishia barafu kwa ajili ya kutunzia dagaa pamoja na ujenzi wa vyumba vya kuchakatia samaki kwa ajili ya usafirishaji ndani na nje ya Nchi  ikiwa ni pamoja na ukarabati na uboreshaji wa Machinjio ambapo Jumla ya Tsh Million Hamsini (Tsh 50,000,000/=) zilitumika katika ukarabati huo

Alisema katika kuboresha maisha ya  Wakulima Serikali imeanzisha sera ya uzalishaji wa Mbegu za Kisasa la Zao la Mchikikichi na kulitangaza kuwa zao la Kimkakati Nchini ambapo miche ya kisasa imeendelea kuzalishwa na kugawiwa kwa wakulima bure na jumla ya Miche Elfu thelathini (30,000) tayari imezalishwa na huku lengo likiwa ni kuzalisha miche Million moja kwa bajeti ya Tsh Million 300/=  

Aidha Mkurugenzi huyo aliendelea kusema Serikali ya Awamu ya Tano imeendelea kuboresha maisha ya makundi maalumu yanayopatikana katika jamiii na  jumla ya vikundi 955 vilitambuliwa kufikia mwaka 2020 na kuwezeshwa mikopo isiyokuwa na riba na kukopeshwa Kiasi cha Fedha Tsh Million 267,777,500/= ukilinganisha kufikia mwaka 2015 ambapo vikundi vilikuwa vimekopeshwa kiasi cha Tsh Million 36,500,000/=

Aliendelea kusema mfuko wa maendeleo ya vijana umeongezeka kutoka Tsh Million 52,000,000/= kwa mwaka 2015 hadi kufikia Tsh Million 352,800,000/= kwa mwaka 2020 huku wanawake wakikopeshwa Tsh Million 164,900,000/= kwa vikundi 66 vya wanawake ukilinganisha na fedha iliyotolewa hadi kufikia mwaka 2015 ambapo ilikuwa kiasi cha Tsh million 22,400,000/= kwa vikundi 23 vya wanawake huku Wazee  4207 wameendelea kutambuliwa na kupewa matibabu bure katika  vituo vya kutolea huduma za afya

 katika kuboresha miundombinu ya viwanda na biashara masoko katika Manispaa hiyo yameendelea kujengwa huku mazingira ya kufanyia biashara kwa wajasiliamali na wanawake yakiboreshwa ambapo kiasi Cha Tsh Million 115,915,200.00/= zilitumika kujenga soko la samaki la jioni ambapo zaidi ya wafanyabiashara mia sita (600) wananufaika na uwepo wa soko hilo ukilinganisha kwa mwaka 2015 ambapo wafanyabiashara na  wajasiliamali 350 walikuwa wanauzia bidhaa zao maeneo ambayo siyo rasmi

Jumla ya hekta 491 zimetengwa kwa ajili ya wawekezaji wa viwanda vikubwa na vidogo eneo la KIZES ambapo miundombinu ya umeme na barabara zinatarajiwa kuboreshwa kwa kiwango cha lami na hati 2,380 tayari zimeandaliwa na kutolewa kwa wananchi

Mkurugenzi huyo alihitimisha kwa kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli  na  Serikali ya awamu ya Tano kwa kuonesha upendo wake kwa vitendo kwa Watanzania na Wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa kuendelea kuwapigania na kuboresha maisha yao kwa kipindi chote cha Awamu ya Tano huku mkurugenzi huyo akisifia suala la kukua na kuongezeka kwa makusanyo na mapato ya Manispaa hiyo.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa