• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MWAILWA AFANYA ZIARA YA KUSHUGHULIKIA MALALAMIKO YA WANANCHI , AFIKA HADI DARAJA LA MTO KATANDARA-BUSHABANI, Grievances solution

Posted on: April 14th, 2020

Mkurugenzi wa manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu  Mwailwa Pangani leo April 14, 2020 amefanya ziara katika manispaa hiyo katika kutatua malalamiko ya wananchi katika mitaa na makazi yao

Amefanya  ziara baada ya kupokea malalamiko ya wananchi wanaoingiliwa na maji na kuharibu miundombinu ya barabara za mitaani kutokana na wingi wa mvua inayoendelea kunyesha maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Kigoma

Akiwa katika Mtaa wa Matofalini kata ya Kasingirima ambapo wananchi walikuwa na malalamiko ya kuharibika kwa barabara kutokana na wingi wa maji ya mvua amekutana na mwenyekiti wa mtaa huo Mhe. Abdallah  Almas Mhuza na kumueleza  namna wananchi wanavyopata shida kutokana na uharibifu wa barabara hiyo

Mkurugenzi  huyo ameahidi barabara hiyo kujengwa kama nyongeza baada ya kuanza ujenzi  wa  barabara ya Kasulu-Ujiji   kwa lengo la kuendeleza standi ya ndogo iliyopo katika eneo hilo na kusema  barabara hiyo ipo tayari katika bajeti ya miradi itakayoanza baada ya mwezi July

Aidha mkurugenzi huyo ametembelea mtaa wa Airport ambapo ofisi  ilipokea malalamiko ya ubovu wa barabara ya mtaa huo  Airport -Mwasenga ambapo pia  ametembelea barabara iliyoharibiwa na maji ya mtaa wa Masanga Kabingo ambapo maji yanawaathiri wananchi wa mtaa huo

Hata hivyo katika ziara hiyo  Mkurugenzi huyo ametembelea  daraja la Mto Katandara lililopo eneo la Bushabani kutokana na athari za mmomonyoko katika daraja hilo  zilizojitokeza baada ya wananchi wa eneo hilo kuwa na tabia ya kuchimba mchanga

Mkurugenzi ameagiza wananchi kuacha tabia ya kuchimba mchanga katika eneo hilo kutokana na athari za mmonyoko ambazo zinaweza kuathiri makazi ya wananchi wa eneo hilo na kuathiri miundombinu ya barabara na daraja  huku akimupigia simu Mhandisi wa TARURA kumtaka aje aone nakushughulikia haraka ili kuepuka kukatika kwa barabara hiyo

Katika ziara hiyo mkurugenzi amefika katika soko la samaki Kibirizi ambapo amekuta kilio cha wanawake wafanyabiashara wa Unga kuingiliwa na maji kutokana na kuongezeka kwa maji katika  ziwa Tanganyika na kuathiri eneo wanalofanyia biashara ambapo mkurugenzi wa huyo amemtaka Mhandisi wa Manispaa hiyo Eng. Wilfred Shimba kusimamia ujazaji wa kifusi katika njia inayoleta maji na maji yaliyopo katika eneo hilo kuondolewa

Wanawake hao wafanyabiashara akiwemo Mama Tatu wamemshukuru Mkurugenzi huyo kwa ziara aliyoifanya na kujionea shida wanayokuwa wanaipata kutokana na maji hayo kujaa na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa kulipa ushuru wa kila siku

Mkurugenzi huyo amehitimisha ziara yake kwa kutembelea ujenzi wa wodi ya Wazazi, na jengo la upasuaji unaoendelea katika  kituo cha afya Gungu ambapo serikali imeingiza zaidi ya shilingi Milioni 200, katika uboreshaji wa kituo hicho, na kutembelea ujenzi unaoendelea wa ofisi ya kata ya Kitongoni  ambapo kiongozi huyo amefanya ziara yake akiwa na Mchumi na Mhandisi wa Ujenzi wa Manispaa hiyo

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa