• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

MWAILWA ASEMA “UJENZI WA VYOO SHULE YA MSINGI KAGERA UANZE MARA MOJA” NA MACHINJIO YA KIBIRIZI KUANZA KUFANYA KAZI WIKI IJAYO. Municipal Director

Posted on: February 3rd, 2020

Mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Mwailwa Pangani  leo januari 3, amewasili katika shule ya msingi Kagera iliyopo katika halmashauri hiyo kwa lengo la  kuona changamoto ya ukosefu wa vyoo inayoikabili shule hiyo

Akiwasili katika shule hiyo akiwa na wataalamu wake Mkurugenzi huyo alipewa taarifa na mwalimu mkuu wa shule hiyo Ndugu. Faustino Satula na kusema  shule hiyo ina jumla ya matundu mawili (2)  ya vyoo huku jumla ya wanafunzi waliopo shuleni hapo wakiwa ni wasichana 634 na wavulana  569 na kufanya jumla ya wanafunzi  1203 sawa na uwiano wa tundu moja kwa wanafunzi 601

Ameendelea kusema upungufu wa vyoo hivyo unafanya uchafuzi wa mazingira kwa baadhi ya wanafunzi kujisaidia ovyo katika maeneo yasiyo sahihi  huku wanafunzi wengine wakienda kujisaidia katika nyumba jirani za wananchi wanaoizunguka shule hiyo  na kuleta kero kwa wakazi hao

Mwalimu mkuu hiyo ameendelea kutoa taarifa kuwa hali ya miundombinu ya shule hiyo ni mibovu na ya zamani, hali ambayo haiwavutii wanafunzi ili waweze kuendelea kujifunza katika mazingira hayo huku akimuomba Mkurugenzi huyo aipe kipaumbele katika ukarabati wa miundombinu ya shule hiyo

Naye mkurugenzi wa halmashauri hiyo akiwa katika shule hiyo amesikitishwa na miundombinu ya shule hiyo  na ukosefu wa vyoo huku akimuagiza Mhandisi wa halmashauri siku ya kesho kumpeleka fundi ujenzi ili kutathimini gharama za ujenzi wa choo kipya chenye matundu kumi ili wanafunzi waweze kusoma katika mazingira salama

Mkurugenzi huyo amesema “Mhandisi nakuagiza kesho mlete fundi ,watathimini ujenzi wa choo kipya chenye matundu kumi ya kuanzia , maana mahitaji yote ya hapa kama ni mchanga,tofali na fedha iko ndani ya uwezo wetu na kufikia siku ya jumatano ujenzi uanze mara moja “

Mkurugenzi huyo ameendelea kumtaka  mhandisi huyo kufanya tathimini ya ukarabati wa majengo , kutokana na uchakafu wa sakafu madarasani, na uchakavu wa mabati ya shule hiyo ili kuweza kuboresha mazingira ya walimu na wanafunzi katika mchakato wa ufundishaji na ujifunzaji

Mkurugenzi huyo ameahidi kupeleka tofali, simenti na fedha ili kuanza na ujenzi wa choo hicho haraka, na kusema katika ukarabati wa madarasa hayo itafanyika tathimini kutoka katika taarifa ya mhandisi kwa lengo la kuangalia mahitaji ya kuingiza katika bajeti ili majengo ya shule hiyo yaweze kuboreshwa

Akiwa katika ziara hiyo shuleni hapo ameongea  na walimu na wanafunzi wa shule hiyo, maeneo mengine aliyofanya ziara ni katika bwawa la Katosho ambapo imeanzishwa kitalu cha miche ya kisasa ambapo jumla ya miche elfu nane ipo tayari huku lengo likiwa ni miche elfu thelathini

Aidha ameendelea na ziara yake katika machinjio ya kibirizi ambapo machinjio hayo  kwa mwaka 2013 yalifungwa na mamlaka ya vyakula na dawa (TFDA) kutokana na kutokidhi vigezo , ambapo mkuu wa Idara ya Uvuvi na Mifugo Ndugu. Edmund Kajuni ameeleza machinjio hayo yamekamilika katika ukarabati huku akisema kwa sasa yako tayari katika kuanza kutumika kuchinjia wanyama

Ameendelea kusema machinjio hiyo ipo tayari kuanza kutumika kutokana na vigezo iliyofungiwa vyote kurekebishwa na kusema kwa wiki ijayo matarajio ya kuanza kwa machinjio hayo ni makubwa sana na wanatarajia kuanza kuchinja Ng’ombe kumi na tano (15) hadi kumi na tisa (19) kwa siku.

Mkurugenzi huyo amehitimisha ziara yake katika shule ya sekondari Rubengera(tarajiwa) awali iliyokuwa shule ya Msingi Kigoma ili kukagua ukarabati wa majengo unaoendelea na kuwakuta mafundi wakiendelea na kazi huku akiwataka kufanya kazi usiku na mchana ili mapema mwezi march wanafunzi wakidato cha kwanza waweze kuanza masomo yao.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa