• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

NAIBU KATIBU MKUU TAMISEMI AKAGUA MIRADI YA LOCAL INVESTMENT CLIMATE ILIYOFADHILIWA NA UBAROZI WA DERNMARK MANISPAA YA KIGOMA UJIJI, AAGIZA CHANZO CHA MAPATO MWALO WA KIBIRIZI UKAGULIWE KILA MARA,DEPUTY SECRETARY GENERAL OF TAMISEMI ISSUED INSTRUCTIONS.

Posted on: November 11th, 2018

Naibu katibu mkuu wa TAMISEMI  Tixon Nzunda juzi nov 9 alitembelea miradi wa Local Investment Climate(LIC) inayofadhiliwa na ubarozi wa Dernmark na kuagiza chanzo cha mapato cha mwalo wa kibirizi kikaguliwe kila baada ya miezi mitatu ili kudhibiti na kuboresha upoteaji mapato katika halmashauri ya manispaa ya Kigoma/Ujiji.

Naibu katibu mkuu huyo alitembelea miradi mitatu ambapo mradi wa kwanza alitembelea eneo la soko la jioni eneo la Mwanga center  lililojengwa kwa ufadhili wa ubarozi wa Dernmark  afisa biashara wa halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji  ndugu. Festo  Nashon alitoa taarifa ya namna soko hilo jinsi litakavyokuwa likifanya kazi kwa kusema asubuhi eneo hilo litatumika kama barabara inapofika majira ya jioni barabara hiyo itakuwa ikifungwa pande zote mbili na wakazi wa eneo hilo kuendelea na biashara na aliendelea kusema mwitikio wa wananchi katika kulipokea soko hilo ni mzuri na tayari limekamilika kwa kiasi kikubwa likiwa na miundombinu ya vyoo pia.

Baada ya ukaguzi wa mradi wa soko msafara uliendelea hadi mwalo wa kibirizi ampapo kiongozi huyo alipewa taarifa na Afisa uvuvi ndugu.Azizi namna mwalo huo ulivyoboreshwa ambapo ufadhili huo wa Dernmark uliweza kujenga  majengo ya stoo ya kuhifadhia mazao ya samaki na dagaa,kufadhili chanja za kisasa za kuanikia samaki na kujenga pavement ya eneo la mwalo huo na eneo la soko la dagaa na samaki eneo la kibirizi, akiwa katika eneo hilo aliendelea kutembelea makampuni ya usafirishaji ya mazao ya samaki na dagaa, na  mitambo ya kuzalishia barafu .

Kiongozi huyo alifanikiwa pia kutembelea kituo cha biashara kilichopo katika manispaa hiyo na kutolewa ufafanuzi na afisa biashara namna kinavyofanya kazi , namna wanafohakikisha ukusanyaji mapato hayapotei  na namna wanavyotoa lesseni kwa wafanyabiashara.

Baada ya ziara hiyo Naibu katibu mkuu huyo aliweza kuongea na wataalamu wa manispaa ya Kigoma Ujiji na wa halmashauri ya wilaya ya Kigoma (wakuu wa idara) katika ukumbi wa manispaa ya Kigoma/ Ujiji, ambapo aliwapongeza wakurugenzi wa halmashauri zote mbili kwa kufanikisha ziara hiyo.

Aliendelea kusema miradi yote aliyotembelea imejengwa kwa viwango vinavyohitajika na kuwataka wataalamu kuiendeleza miradi hiyo kwa ushirikiano mkubwa na kuagiza kituo cha biashara kilichojengwa manispaa ya Kigoma Ujiji kiendelee kufanya kazi na wafanyabiashara kuendelea kuja kupata elimu juu ya masuala ya kibiashara.

Naye katibu mkuu huyo alipongeza ubunifu uliofanyika katika manispaa hiyo katika kuhakikisha vyanzo vipya vya mapato vinapatikana kama ujenzi wa soko la jioni katika manispaa hiyo, amewataka wataalamu kuendelea kuboresha eneo hilo la soko la jioni ili kuleta ufanisi mkubwa katika upatikanaji wa mapato.

Lakini pia alitaka mwalo huo kuendelea kujengwa zaidi ili kufanikisha wavuvi wanapoleta mazao yao nchi kavu na kuwataka wataalamu wa manispaa chini ya mkurugenzi kutafuta wafadhili zaidi wa kujenga eneo la kupakulia mazao hayo ya ziwani  kama vile TARURA na wengine wengi.

Naibu katibu mkuu huyo akizungumzia suala la changamoto za vifaa vya kuzalishia barafu, ambapo kuna mashine tatu na mbili zikiwa mbovu amewataka makampuni ya kibiashara yaliyoko hapo kufanya ufadhili ili mashine hiyo zitengemae na kuendeleza ufanisi wa kazi wa kila siku.

Aidha naibu katibu mkuu huyo aliweza kuhoji fedha za mradi wa  EQUIEP zilizoweza badilishiwa matumizi halmashauri ina mpango gani wa kuzirejesha, naye mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndg. Mwailwa S. Pangani alisema fedha hizo tayari wameanza kuzirudisha kwa vyanzo vya mapato ya ndani na fedha zinazotolewa kuendeshea idara.

Naibu katibu mkuu alimalizia kwa kuzitaka halmashauri zote kufanya maandalizi mazuri ya uchaguzi wa serikali za mitaa kwa mwaka 2019 na kuwataka wakuu wa idara kufanya kazi kwa ushirikiano , kusimamia sheria, kanuni na maadili bila kupatikana na vitendo viovu kama vile rushwa na kuzitaka halmashauri hizo kuendelea kubuni miradi ya kiuchumi,huduma za jamii kama vile shule na zahanati kuzipa kipaumbele.

Naye mkurugenzi wa halmashauri wa manispaa ya Kigoma/Ujiji aliweza kushukuru kiongozi huyo kwa ziara aliyoifanya katika manispaa hiyo na kusema maagizo aliyoyatoa na ushauri alioutoa utafanyiwa kazi ili kuleta ufanisi mzuri wa utendaji kazi na kuendelea kubuni vyanzo vya mapato vipya na kuhakikisha wanasimamia kwa uzuri suala la ukusanyaji mapato.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa