• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

NAIBU WAZIRI WA AFYA AHUTUBIA BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI, AELEZA FEDHA ZA AWALI ZA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA, Hon.

Posted on: January 26th, 2022

Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel leo January 26, 2022 amehutubia Baraza la Madiwani Manispaa ya Kigoma/Ujiji huku akieleza Utekelezaji unaoendelea kufanywa na Serikali ya Awamu ya sita katika  Manispaa hiyo na Mkoa wa Kigoma katika sekta ya afya

Akihutubia Baraza hilo amesema Serikali ya Awamu ya Sita tayari imeleta fedha zaidi ya Billion 16 Mkoani Kigoma  kwa ajili ya kuimarisha miundo mbinu ya afya na vifaa tiba na tayari Wilaya zote za Mkoa huo ujenzi unaendelea  

Amesema fedha za awali kwa ajili ya Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kigoma Tsh Million 500   tayari zimetolewa huku akilitaka Baraza hilo la Madiwani kufanya uamuzi wa haraka wa eneo ambapo Hospitali hiyo itajengwa

Ametaja Ujenzi unaoendelea katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma (Maweni)  ikiwa ni Ujenzi wa jengo la damu salama kwa gharama  ya  fedha Kitanzania Million 428, Ujenzi wa Jengo la Mapokezi na Mochwali kwa gharama ya fedha za Kitanzania Billion 2.8 ,  Ujenzi wa Jengo la wagonjwa Mahututi na jengo la dharura  kwa gharama ya fedha za Kitanzania Billion 1.2  huku akisema tayari fedha za ununuzi wa siti scan Billion 1.6 imetolewa kwa ajili ya Hospitali hiyo

Ameendelea kusema Maboresho na Ujenzi wa Hospitali hiyo ni kwa lengo la kuokoa fedha za  Wagonjwa  ambao wamekuwa wakipatiwa rufaa za kwenda katika Hospitali zenye huduma za Kibigwa kama vile Bugando, na Mhimbili

Aidha amesema kukamilika kwa Ujenzi huo kutaleta mabadiliko ya  huduma za kiafya ikiwemo huduma za Kibigwa kupatikana na kuwahudumia watu wengi zaidi wakiwemo wa Mataifa jirani huku akisema baadhi ya Madkatri Bigwa watahamishiwa katika Hospitali hiyo na wataalamu wengine wakipelekwa masomoni

Amehitimisha kwa kuwataka Madiwani na  wataalamu  kushirikiana na Mbunge wa Jimbo hilo katika ufuatiliaji wa fedha  wa Ujenzi wa kituo cha afya kipya katika Manispaa hiyo

Awali Meya wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Mhe. Baraka Naibuha Lupoli akimkaribisha Naibu Waziri aliipongeza Serikali ya Awamu ya Sita katika jitihada za kuwahudumia Wananchi  huku akimuomba  kiongozi huyo kuleta fedha kwa ajili ya Ujenzi wa kituo cha Afya ili kupanua huduma za afya na kuwa na vituo vya afya vya kutosha na kuendelea kuongeza upatikanaji wa vifaa tiba na dawa katika Hospitali na Zahanati za Serikali zilizopo katika Manispaa hiyo


Naye Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini Mhe. Shabani Ng'enda Kilumbe akitoa salamu amesema asubuhi amepokea vifaa tiba vitakavyotumika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kigoma (Maweni)  vilivyogharimu kiasi cha fedha za Kitanzania Million 105 ikiwa ni jitihada za Serikali  na fedha  kutoka kwa wafadhili huku akiipongeza  Serikali kwa kuanzisha kambi  za kutoa huduma za Kibingwa katika Hospitali  hiyo huku akisema tayari Wananchi 914 wamepata huduma za Kibigwa

Kwa taarifa zaidi tembelea, picha na video kuhusu taarifa hiyo tembelea www.kigomaujijimc.go.tz




Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • WAJASIRIAMALI WAENDELEA KUFIKIWA NA WATAALAMU KIGOMA UJIJI. Social services

    May 30, 2025
  • UGAWAJI WA VYANDARUA BURE UNAENDELEA KWENYE VITUO KIGOMA UJIJI. Health protection

    May 29, 2025
  • WAJASIRIAMALI KIGOMA UJIJI WATEMBELEWA NA WATAALAMU.

    May 28, 2025
  • RC ANDENGENYE AZINDUA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA MKOA WA KIGOMA. Malaria protection

    May 28, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa