• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

RAIS SAMIA AMWAGA FEDHA KWA MARA NYINGINE TENA UJENZI WA MADARASA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI construction

Posted on: October 17th, 2022

Na Mwandishi Wetu

Manispaa ya Kigoma/Ujiji imepokea kiasi cha fedha za Kitanzania Billion moja na milion mia moja arobaini na Sita (Tsh 1, 146, 000, 000/=)  kutoka Serikali  Kuu  ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  chini ya Rais Mhe. Samia Suluhu Hassani   kwa lengo la Ujenzi wa vyumba vya madarasa hamsini na saba (57)  ikiwa ni Maandalizi na Mapokezi ya Wanafunzi wa kidato cha kwanza kwa Mwaka 2023

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Bi.  Ester Alexander Mahawe Leo October 10, 2022 amefanya kikao   na Viongozi na Wasimamizi wa miradi ya elimu kwa lengo la kuweka mikakati  namna utekelezaji na ujenzi wa madarasa hayo kwa viwango  vilivyo bora

Mkuu huyo wa Wilaya amewataka Wakurugenzi, Watendaji Kata, na Wakuu wa Shule kuzingatia weredi katika kuchagua Mafundi watakaoomba kazi hizo za Ujenzi wa madarasa  na kuepuka Mafundi wasio kuwa waadilifu

Aidha amewataka Wahandisi kusimamia mpango wa Ujenzi (BOQ) na Maafisa manunuzi kuhakikisha mipango ya manunuzi haicheleweshi utekelezaji na ujenzi wa madarasa hayo

Aidha amewataka Waheshimiwa Madiwani wenye miradi kutambulisha miradi hiyo kwa Wananchi kwa kufanya mikutano ili kuwa na uelewa juu ya miradi inayotekelezwa katika maeneo yao

Naibu Meya wa Manispaa ya Kigoma /Ujiji  Mhe. Mgeni Kakolwa ameipongeza Serikali kwa kuendelea kuleta fedha za Maendeleo katika Manispaa hiyo   kwa lengo la kuboresha miundombinu  na jukuza taaluma

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Ndugu. Evansi Mdee amesema Manispaa ya Kigoma/Ujiji tayari imeshafanya vikao na Wakuu wa idara wanaohusika na ujenzi wa Madarasa hayo wakiwemo Maafisa elimu, Wahandisi na Maafisa manunuzi kwa lengo la kuhakikisha miundombinu itakayojengwa inakuwa bora na kuwa na Usimamizi na ufautiliaji wa mara kwa mara

Kikao hicho kimehudhuriwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama,  Katibu Tawala wa Wilaya, Naibu Meya na Mwenyekiti wa Halmasharuri ya Wilaya,  Viongozi wa Chama cha Mapinduzi,  Waheshimiwa Madiwani, Wakuu wa idara na Vitengo, Watendaji Kata, Waratibu elimu Kata na Wakuu wa Shule

Kwa Mwaka wa fedha 2020/2021 Manispaa ya Kigoma/Ujiji ilitekeleza Ujenzi wa Vyumba vya Madarasa arobaini na nane (48) yaliyogharimu  kiasi cha fedha za Kitanzania Million mia tisa sitini (Tsh 960,000,000/=) ikiwa ni fedha zilizotoka Serikali Kuu

Kwa taarifa zaidi endelea kutembelea www.kigomaujijimc.go.tz na mitandao yetu ya kijamii ili kupata taarifa zaidi       

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa