• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

“TUTAJENGA MADARASA 38 KWA NGUVU YA WANANCHI” WASEMA WENYEVITI WA MTAA KIGOMA/UJIJI CONSTRUCTION OF CLASSES

Posted on: December 19th, 2019

Wenyeviti wa Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji wameahidi kutatua changamoto ya wanafunzi kukosa nafasi ya kujiunga na kidato cha kwanza  kwa mwaka mwaka 2020 kutokana na upungufu uliopo katika halmashauri hiyo wa vyumba vya madarasa 38 kwa kuwashirikisha wananchi

Wameyasema leo Desemba 19, katika ukumbi wa halmashauri baada ya wenyeviti wa mitaa 68, watendaji wa kata na mkurugenzi wa halmashauri kukutana kwa lengo la kunusuru wanafunzi  1753 waliofaulu na kukosa nafasi ya kujiunga na kidato cha kwanza kutokana na upungufu wa madarasa katika shule za upili.

Akitoa ufafanuzi katika kikao hicho Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Ndugu. Frednand Filimbi amesema  wanafunzi waliofaulu  mtihani wa darasa la saba  kwa mwaka 2019 ni wanafunzi  Elfu tatu mia tisa kumi na nane (3918) sawa na 85% ya waliofanya mtihani, waliochaguliwa kujiunga na na kidato cha kwanza kwa shule zilizopo ni wanafunzi  Elfu mbili mia moja sitini na tano (2165) ambapo wanafunzi waliofaulu na kukosa nafasi kutokana na Upungufu wa  vyumba vya madarasa ni  wanafunzi  Elfu moja mia saba hamsini na tatu (1753) na kufanya kuwa na upungufu wa  vyumba vya  madarasa thelathini na nane(38) kwa sasa ili wote waweze kujiunga na kidato cha kwanza

Ameendelea kusema tayari halmashauri imechukua hatua kukabiliana na tatizo hilo kwa kuanza mchakato wa ununuzi wa tofali na kukutana na baadhi ya Taasisi za serikali na binafsi kama vile Benki ya NMB  ili kuweza kusaidia katika kuhakikisha halmashauri inaondokana na upungufu  huo wa vyumba vya madarasa

Naye Kaimu Afisa Elimu Sekondari Ndugu. Yaragwila Gwimo amesema halmashauri ina shule 18 za kutwa, na shule 1 ya Bweni ambapo shule 8 hazina upungufu wa madarasa na shule 10 kuwa na upungufu wa madarasa

Ameendelea kusema kata ya Gungu inaongoza kwa kuwa na wanafunzi  mia nne hamsini na mbili (452) waliokosa nafasi ya kujiunga na kidato cha kwanza sawa na vyumba vya madarasa tisa (9) vinavyohitajika  ikifatiwa na kata ya Mwanga kaskazini yenye wanafunzi  mia tatu sabini na mbili (372) waliokosa nafasi sawa na vyumba vya madarasa saba(7)

Naye Afisa Tarafa wa Kigoma Kaskazini Ndugu. Maxmilliani Ngasa  amepongeza kikao hicho kilichoandaliwa na ofisi ya Mkurugenzi wa halmashauri huku akiwataka watendaji wa kata, wenyeviti wa mitaa hiyo kwenda kulifanyia kazi kwa kuliweka kuwa agenda za kata na kufanya mikutano na wananchi kwa lengo la kutatua tatizo la upungufu wa vyumba vya madarasa

Nao baadhi ya watendaji wa kata akiwemo  Wamesema ujenzi wa vyumba vya madarasa wameupokea kwa uzuri na kuahidi kulifanyia kazi kwa kufanya mikutano na wananchi , na kusimamia shughuli ya ujenzi itakayokuwa ianendelea ili kuhakikisha wanafunzi waliokosa nafasi wanaanza masomo yao kabla ya mwezi februali

Nao baadhi ya wenyeviti wa mitaa akiwemo Ndugu Azizi Ibrahimu (myenyekiti wa mtaa wa Mgeo,Buhanda) na Bakari Songolo (Mwenyekiti wa mtaa wa Taifa, Rusimbi) wameipongeza halmashauri ya Manispaa kwa kuja na mpango mkakati wa ujenzi wa madarasa kwa kushirikiana na nguvu ya  wananchi  kuweza kufanya wanafunzi walifaulu wanapata nafasi ili kuweza kuendelea na masomo ya upili

Naye mwenyekiti wa mtaa wa Kasulu Ndugu. Mlekwa Mfaume ameendelea kupongeza halmashauri kuja na mpango wa wanafunzi waliokosa nafasi ili wapate fursa ya kujiunga na masomo hayo ya upili huku akishauri halmashauri iandae mkakati wa kujenga nyumba vya madarasa mapema kabla ya wanafunzi kukosa nafasi na kuchelewa kuanza masomo yao

Naye Kaimu Mkurugenzi amehitimisha kwa kuwashukuru Wenyeviti wa mtaa, na watendaji  wa kata kuitikia wito na kuonesha nia ya kuweza kujenga vyumba vya madarasa kwa kushirikiana na nguvu ya wananchi ili kuweza kurithisha elimu katika kizazi kilichopo, na kusema serikali ya awamu ya tano ipo pamoja na wananchi kuhakikisha elimu  inakuwa urithi kwa watoto wa Kitanzania na kusema Manispaa ya kigoma/Ujiji  ilishika nafasi ya 1 kimkoa na ya 72 kitaifa kwa ufaulu wa asilimia 85% katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba 2019

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa