• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

UKAGUZI WA VYOO NYUMBA KWA NYUMBA WAANZA MANISPAA YA KIGOMA UJIJI KATA YA BANGWE, WASIO NA VYOO WATOZWA FAINI NA KUFUNGULIWA MASHITAKA.INSPECTION

Posted on: January 24th, 2019

Moja ya mkazi wa Bangwe aliyebainishwa kwa kutokuwa na vyoo kabisa akianza taratibu za ujenzi baada ya kukutana na maafisa afya nyumbani kwake


Kaimu mkuu wa idara ya usafi, afya na mazingira manispaa ya Kigoma Ujiji akikagua moja ya choo kilichopo katika mtaa wa kamala Kata ya Bangwe


Zoezi la ukaguzi kwa watu wasio na vyoo manispaa ya Kigoma Ujiji laanza katika kata ya Bangwe leo January 24, kwa kutoza faini kutokana na agizo la Waziri mkuu Kassimu Majaliwa kila nyumba kuwa na choo bora.

Agizo hilo lililotolewa na kiongozi huyo mwishoni mwa mwaka 2018 ikiwa ni kuleta uimarishaji wa afya za Watanzania, kutokana na agizo hilo manispaa ya Kigoma Ujiji kupitia kitengo chake cha Usafi na Mazingira chini ya kaimu mkuu wa kitengo hicho Ndugu. Bakari A. Bakari imefanya oparesheni kwa kutembea nyumba kwa nyumba na kubaini na watu wasio na vyoo.

Akizungumuza kaimu mkuu wa kitengo hicho Manispaa ya Kigoma/Ujiji amesema oparesheni hii itafanyika katika nyumba zote zilizo katika kata 19 zilizobainishwa kutokuwa na vyoo na mawakala wa kuleta mabadiliko ya jamii (CCA).

Ameendelea kusema katika ukaguzi huo unafanyika ni pamoja na kutoa elimu namna vyoo bora vinatakiwa viwe kwa kuhakikisha vyoo vinakuwa na shimo la pembeni lililojengewa, lenye paa, na kuwa mlango na kuwa na vibuyu chirizi na sabuni ili kuimarisha usafi wa mikono na mwili mara baada ya kujisaidia.

Katika ziara hiyo Shilingi elfu hamsini zimekusanywa kutokana na faini ya mtu mmoja ambaye hakuwa na choo na wengine zaidi ya kumi na tano kupewa masaa ishirini na nne kulipa faini hiyo katika ofsi ya kata na kuhakikisha vyoo vinajengwa ndani ya siku saba.

Naye kiongozi wa mawakala wa kuleta mabadiliko katika jamii(CCA) Bi. Yasinta Vitusi amesema tayari wamebaini nyumba 98 zilizopo katika manispaa ya Kigoma Ujiji ambazo hazina vyoo kabisa na zingine kutokuwa na vyoo bora.

Ameendelea kusema katika ukaguzi huo wameendelea kutoa elimu juu na umuhimu wa vyoo kwa kuwataka wakazi wa manispaa ya Kigoma Ujiji kuimarisha afya zao kupitia kampeni ya “nyumba ni choo” ili kuepuka magonjwa ya kipindupindi na tumbo.

Nao baadhi ya wananchi waliobainishwa kwa kutokuwa na vyoo waliweza kuelezea zoezi hilo, Bi. Raila Habibu mkazi wa kata ya Bangwe anasema zoezi hilo ni zuri kwani linawaepusha na kuwapa elimu namna ya kuepukana na magonjwa na kuahidi choo chake kukishughulikia ndani ya siku saba alizopewa.

Naye mzee Amiri Barakiliza aliyebainika kwa kutokuwa na choo amesema changamoto ya wakazi wa kata hiyo kutokuwa na vyoo ni uzembe hali inayoweka afya zao katika mazingira hatarishi kwa kukumbwa na magonjwa ya milipuko kama vile kipindupindu na kuahidi na kuchimba choo ndani ya siku saba katika kaya yake.

Akihitimisha zoezi hilo kaimu mkuu wa kitengo cha Usafi na Mazingira Ndugu. Bakari A. Bakari amesema zoezi hilo ni endelevu na wataendelea kulifanya kwa kata zote ambazo wakazi ambao tayari wameshabainishwa kutokuwa na vyoo kwa kushirikiana na wataalamu kutoka ofsi ya Mkurugenzi wa halmashauri, watendaji kutoka katika kata na mawakala wa kuleta mabadiliko ndani ya jamii.

PICHA ZAIDI INGIA KATIKA MAKTABA YA PICHA



Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • WAJASIRIAMALI WAENDELEA KUFIKIWA NA WATAALAMU KIGOMA UJIJI. Social services

    May 30, 2025
  • UGAWAJI WA VYANDARUA BURE UNAENDELEA KWENYE VITUO KIGOMA UJIJI. Health protection

    May 29, 2025
  • WAJASIRIAMALI KIGOMA UJIJI WATEMBELEWA NA WATAALAMU.

    May 28, 2025
  • RC ANDENGENYE AZINDUA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA MKOA WA KIGOMA. Malaria protection

    May 28, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa