• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

USAFI WA MJI NA MAZINGIRA KUWA AGENDA YA WAKAZI WOTE WA KIGOMA/UJIJI, sanitation

Posted on: April 1st, 2021

Na Mwandishi wetu

Watendaji wa kata za Manispaa ya Kigoma/Ujiji wametakiwa kuzijengea uwezo Asasi za kijamii (vikosi kazi) zinazojihusisha na shughuli za usafi wa Mji katika mitaa mbalimbali ili ziweze kujitegemea na kujiendesha kifedha

Yamesemwa hayo leo April 1, 2021  na Mtaalamu wa udhibiti taka ngumu na Mazingira Ndugu. Patrick Matandala wakati akihitimisha mafunzo yaliyofanyika kwa  siku mbili kwa Watendaji Kata  katika ukumbi wa Hoteli ya Greenview katika kuwajengea uwezo wa kuhakikisha mji unakuwa safi

Mtaalamu huyo amewataka watendaji kata kuhakikisha wanazishauri asasi za kijamii (vikosi kazi) zinazojishughulisha na usafi kwa kuhakikisha zinajiendesha ikiwa ni pamoja na ununuzi wa vifaa na  ukusanyaji wa pesa za uzoaji taka ili ziweze kukua na kufikia hatua ya Makampuni ya usafi

Ameendelea kusema kuwa ipo haja ya asasi hizo kusajiliwa na kupewa mikataba ya usafi ili iweze kuwalinda katika shughuli wanayoifanya na kusajiliwa huko kutasaidia asasi hizo kuwa na uwezo wa kukopeshwa katika taasisi mbalimbali za kifedha  au makampuni kwa kuwezeshwa vifaa vya usafi

Amesema asasi hizo za kijamii kama zitawezeshwa na kujengewa uwezo zitakuwa na uwezo wa kuchakata baadhi ya taka ili zitumike kama bidhaa zingine na utengenezaji wa mbolea za mboji(recycling and re-use) ambapo amesema vikundi vingine vimeanza kukusanya taka za plastiki na kuzisaga na kuzisafirisha kwenda viwandani

Kaimu Mkuu wa idara ya Usafi na Mazingira Ndugu. Elishaphati Rusemvya amewapongeza watendaji hao kwa mafunzo ya kujengewa uwezo waliyoyapata ili kuhakikisha wanakuza asasi za kijamii na kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika kuhakikisha mji unakuwa safi na taka nyingi kukusanywa ili kuepuka madhara yatokanayo na kusambaa kwa taka katika jamii

Mkuu huyo wa idara amewakaribisha wadau mbalimbali wa kufanya  usafi wa mji kutokana na fursa za kujiingizia kipato,  na upungufu wa asasi za usafi na kwa  sasa vikundi vilivyosajiliwa ni vikundi ishirini na mbili(22) tu vitakavyofanya usafi kwa mitaa hiyo ishirini na mbili(22) licha ya Manispaa hiyo kuwa na mitaa sitini na nne(64)

Amesema kwa mjibu sheria ndogo za Manispaa hiyo suala la uchimbaji wa shimo majumbani ili kuwekewa taka ni kosa kisheria hivyo wakazi,taasisi na wafanya biashara wanawajibu wa kukusanya taka wanazozizalisha na asasi za kijamii zinazojishughulisha na usafi kuzichukua na kuzipeleka katika maeneo yaliyopangwa kwa ukusanyaji wa taka kwa kila mtaa

Mtendaji wa kata ya Rubuga Bi. Asha Mrisho amesema mafunzo hayo waliyoyapata yamewajengea uwezo wa kuhakikisha wanazisaidia asasi za kijamii zinazojishughulisha na usafi wa mji kwa kila mtaa, na wao watahakikisha wanashiriki kuzikuza huku agenda za usafi wa mazingira kuwa suala mtambuka kwa  mwananchi wote  na kuhakikisha wanashiriki katika kutoa ada za ukusanyaji wa taka hizo

Mafunzo hayo yaliyofanyika ikiambatana na ziara  ni mwendelezo wa kujengea uwezo wa wataalamu ambapo awali yalifanyika kwa Wakuu wa idara na Vitengo na yanatarajiwa kuendelea kwa wadau mbalimbali ikiwemo asasi za kijamii(vikosi kazi vya usafi) zinazoshighulisha na usafi wa mji ili kuhakikisha zinakuwa na uwezo wa kujiendesha

Na ikumbukwe Manispaa ya Kigoma/Ujiji inazalisha tani mia moja na arobaini (140) kwa siku ambapo inakadiriwa kila mkazi wa Manispaa hiyo kwa siku anazalisha kilogram 0.5 kwa siku na hali hiyo inatokana na ukuaji na ongezeko la watu

 Picha na video zaidi ingia katika maktaba ya picha katika tovuti yetu  www.kigomaujijimc.go.t

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa