• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

UTAMADUNI WA WANAUME WA KIGOMA MAARUFU “KUHANZURA” UNAATHIRI WANAWAKE WA MKOANI KIGOMA,women celebration

Posted on: March 5th, 2020

Kongamano la kuhitimisha wiki ya maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani Manispaa ya Kigoma/Ujiji limefanyika leo march 5, katika ukumbi  wa Redcross uliopo katika Manispaa hiyo

Kongamano hilo limefanyika likianza kwa maandamano ya wanawake wakianzia  Ofisi  kuu ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kupitia barabara ya Lumumba , Maweni , kituo cha Polisi hadi ukumbi wa Redcross wakiwa na ujumbe wa kuhamasisha usawa na haki sawa kwa wote

Katika kongamano hilo Wanawake wameaswa kuwa katika haki wanazopata isiwe nafasi ya kuweza kuwagandamiza wanaume katika familia zao bali ikawe mwanzo wa kufungua fursa za kiuchumi ili kuleta ustawi wa kifamilia katika Nyanja tofauti tofauti

Akihutubia katika kongamano hilo Mgeni Rasmi Bi. Frida Chinuka amepongeza jitihada  zilizofanyika Nchini  na zinazoendelea kufanyika  kuinua uchumi kwa wanawake kupitia asasi na  Mashirika mbalimbali ya Serikali na yasiyo ya Serikali

Katika hotuba yake amewataka Wanawake kuendelea kufanya shughuli mbalimbali za uzalishaji mali pasipo kujinyanyapaa huku wakiamini kuwa wanawake wanaweza na jamii inapaswa kuwapa nafasi  ili waweze kuachana na utegemezi wa kifikra na uchumi pia

Ameipongeza Halmashauri ya Manispaa kwa kuhamasisha na kuunda vikundi 65 vya Wanawake wajasiliamali na kuwawezesha kupata mikopo kutoka katika mikopo ya wanawake , vijana na walemavu inayotolewa na Manispaa ya Kigoma/Ujiji mara kwa mara huku akisisitiza Manispaa hiyo kuendelea kuwainua na kuwaendeleza wanawake kiuchumi

Naye Mkuu wa idara ya Maendeleo ya jamii, Jinsia, Vijana , Wazee na Watoto Ndugu. Jabiri Majid akieleza mafanikio ambayo Manispaa hiyo imeweza kufikia katika kuwainua wanawake amesema Manispaa imekuwa ikitoa elimu ya kijinsia , na kupambana na vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa wanawake na watoto

Ameendelea kusema Manispaa imeunda kamati za ulinzi za kupambana na ukatili na kuleta usawa wakinjisia , kamati hizi zimeundwa kwa kata kumi na tisa (19) zote za manispaa ya Kigoma/Ujiji na kutengeneza mazingira ya kibiashara kwa wanawake kwa kuanzisha soko la usiku la Mwanga

Jeshi la polisi kupitia dawati la jinsia na watoto Mkoani Kigoma limesema limekuwa likipambana na vitendo vya kiutali vinavyofanywa na jamii huku wakiipongeza jamii kwa kutoa ushirikiano mara kwa mara licha ya baadhi ya watu wachache kuwaficha waharifu na wengine kutotoa ushahidi wa waharifu

Afisa kutoka Jeshi la Polisi akitoa tawimu amesema kwa mwaka 2018 watu waliolipotiwa kubaka walikuwa watuhumiwa 22  huku kwa mwaka 2019 wakiongezeka na kufikia watuhumiwa 23, na vitendo vya ulawiti vilivyolipotiwa ni matukio mawili (2) tangu mwezi januari 2020 huku matukio ya kujaribu kubaka yakiwa mawili(2)

Amehitimisha kwa kuitaka jamii kuendelea kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi katika kulipoti vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto , na wale wanaoficha waharifu kwa kigezo cha kuwa ni ndugu au kuogopa kutoa ushirikiano kuacha tabia hiyo ili kuweza kumaliza vitendo vya ukatili vinavyofanyika ndani ya jamii

Naye mwakilishi kutoka Shirika la kuhudumia viwanda vidogo(SIDO) Bi. Mwaselembe amewapongeza wanawake wote wajasiliamali wadogo na wakubwa kwa kuendelea kujiinua kiuchumi huku akiwataka wanawake wote kuungana pamoja katika shughuli zao na kuanzisha viwanda vidogovidogo

Amewataka wanawake kujenga tabia za kushindana katika bidhaa zao na kuwa wabunifu ili kuleta mvuto tofauti tofauti kwa wateja wao na wanawake hao kuzalisha kulingana na mahitaji ya jamii ili kuweza kufurahia biashara ambazo wanazifanya

Naye Afisa Masoko kutoka Benki ya NBC Bi. Janeth Chacha ameendelea kutoa pongezi kwa wanawake kuendelea kuona fursa  za mikopo zinazokuwa zikitolewa katika benki mbalimbali , huku akiwataka wanawake kujenga tabia ya kuweka akiba katika uzalishaji wao wanaoufanya

Akiongea katika kongamano hilo Bi. Chausiku Mgahula amesema zipo mila za wanawake wa kigoma zinazowaathiri ambazo mila hizo ni wanaume kuwa na tabia ya kusafiri kwenda mikoa mingine kutafuta pesa maarufu “Kuhanzura “ na kuwaachia watoto bila matunzo yeyote jambo linalowathiri wanawake katika malezi ya familia kutokana na vipato vidogo wanavyovipata huku akiwaasa wanaume wanaposafiri kwenda mikoani kuzikumbuka familia zao katika mahitaji ya kila siku

Kongamano hilo la wanawake limefanyika ikiwa ni katika kuelekea kilele cha siku ya wanawake Duniani ambapo huazimishwa March 1-8 kila mwaka, ambapo maadhimisho ya mwaka huu yakiwa na kauli mbiu ya “Kizazi cha usawa kwa maendeleo ya Tanzania ya sasa nay a baadae” na kwa mwaka huu  Kitaifa maadhimisho hayo yakihitimishwa mkoani Simiyu

Maadhimisho haya ya Siku ya wanawake Duniani yalianzishwa mwaka 1911 huko nchini Marekani ambapo wanawake wafanyakazi wa viwandani walikuwa wakinyanyaswa na kuamua kuanzisha siku hii ili kudai haki sawa kwa wote na Nchini Tanzania maadhimisho hayo yalianza mwaka 1997


Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • WAJASIRIAMALI WAENDELEA KUFIKIWA NA WATAALAMU KIGOMA UJIJI. Social services

    May 30, 2025
  • UGAWAJI WA VYANDARUA BURE UNAENDELEA KWENYE VITUO KIGOMA UJIJI. Health protection

    May 29, 2025
  • WAJASIRIAMALI KIGOMA UJIJI WATEMBELEWA NA WATAALAMU.

    May 28, 2025
  • RC ANDENGENYE AZINDUA ZOEZI LA UGAWAJI VYANDARUA MKOA WA KIGOMA. Malaria protection

    May 28, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa