• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

WADAU WA MAENDELEO MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI WAAHIDI KUCHANGIA FEDHA KUWEZESHA ZOEZI LA ANWANI ZA MAKAZI , Postcode

Posted on: March 3rd, 2022

Na Mwandishi Wetu

Wadau wa Maendeleo Manispaa ya Kigoma/Ujiji wameahidi kuunga mkono juhudi za Serikali katika zoezi la utambuzì na uwekaji wa anwani za makazi kwa kuchangia fedha za kuwezesha zoezi hilo

Wameyasema hayo Leo March 03, 2022 katika kikao kilichoandaliwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya  Kigoma/Ujiji kilichofanyika katika Ukumbi wa  Joy in the Harvest  kwa lengo la   kuwajengea ulewa wa  na kuwashirikisha katika  zoezi hilo

Mgeni rasmi wa kikao hicho Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Bi. Ester Alexander Mahawe amewashukuru wadau hao kwa kuonesha na kuahidi kutoa fedha zitakazosaidia ununuzi wa nguzo, vibao vya mabati, na fedha za uratibu wa zoezi hilo

Amesema michango itakayotolewa atahakikisha inafanya kazi iliyokusudiwa ili kuhakikisha kila Mwananchi na mkazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji  anakuwa na utambulisho wa mahali anapopatikana  huku akimtaka Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kufikisha barua na fomu za mchanganuo wa bajeti kwa wadau hao wa Maendeleo ili kuchangia Kadri ya uwezo wao

Katika hotuba yake amewataka Wananchi kuhakikisha wanasimia zoezi hilo na kulinda miundombinu kama vile nguzo na vibao vitakavyosimikwa ili kutambulisha makazi na majina ya barabara  

Aidha amesema kukamilika kwa zoezi hilo kutarahisisha Serikali kufikisha maendeleo kwa wananchi kwa urahisi kutokana na kujua miundombinu na huduma zinazopatikana kwa wananchi, upangaji wa bajeti, kuwezesha na kukuza Biashara Mtandaoni, upatikanaji kirahisi wa huduma za Jeshi la zima moto na Polisi    

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi( CCM) Wilaya ya Kigoma Alhaji Yassin Mtalikwa amesema Chama hicho kinalidhishwa na utekelezaji wa ilani  unafanywa na Viongozi wa Serikali ambapo pia amewataka wadau mbalimbali wa Maendeleo ikiwemo vyama vyote  vya Siasa kuunga mkono zoezi hilo litakalolsaidia kufikisha maendeleo kirahisi kwa Wananchi    

Nao baadhi ya wadau wa Maendeleo wakiwemo viongozi wa dini  Paroko wa Kanisa la Roman katoliki Kigoma Mjini Padre  Castus Rwegeshora na Mchungaji Eliudi  Katona wameipongeza Serikali katika utekelezaji wa mpango wa anwani za Makazi na kusema wao kama taasisi za dini watahamasisha waumini wao kushiriki kikamilifu katika zoezi hilo na kutoa fedha ili kutekeleza zoezi hilo

Naye mmoja kutoka katika Asasi za Kirai inayojishughulisha na msaada wa Kisheria Ndugu. Rufuano (kwa jina moja)  amesema anaamini zoezi hilo litafanyika pasipo kizuizi chochote huku akiwaka wananchi kuendelea kuelimishwa kwa ajili ya kufanikisha suala hilo

Wadau wa Maendeleo waliohudhuria katika kikao hicho ni pamoja na viongozi kutoka Ofisi na taasisi za Umma,  viongozi kutoka Mashirika ya Serikali na yasiyo ya Serikali, Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi, Vyama vya Siasa, Viongozi wa madhehebu ya Kidini, Watu Maarufu na Mashirika ya Kimataifa      


Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa