• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

Wadau wa Usafi na Mazingira wakutana Manispaa ya Kigoma/Ujiji, strategic of environment safety

Posted on: December 29th, 2020

Na Mwandishi wetu

Wadau wa Usafi na mazingira leo  Desemba 29, wamekutana na Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji katika Ukumbi wa Manispaa hiyo kwa lengo kuweka mikakati ya kufanikisha Mji unakuwa safi

Wadau hao waliofika katika Ukumbi wa Manispaa ni Watendaji wa Kata, wenyeviti wa serikali za Mitaa, kamati za Usafi ngazi ya Mtaa, Viongozi wa Dini, na vikosi kazi vya usafi vilivyosajiliwa ngazi ya mtaa wakiongozwa na Wataalamu kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo

Mkuu wa idara ya  Mipango na Uchumi Ndugu. Frednand Filimbi Akiwasilisha kwa niaba ya Mkurugenzi amesema lengo la kuwaita wadau hao ni kuweka  mikakati imara ya kuendeleza Usafi wa Mazingira kwa Mitaa 68 ya Manispaa na kuhakikisha mji unakuwa safi kwa kutumia vikosi kazi  

Mkuu huyo wa idara ameendelea kusema ni wajibu wa vikosi kazi vilivyoundwa ngazi ya mtaa kuendelea kufanya usafi katika maeneo yao ambapo watakuwa wakikusanya taka katika maeneo maalumu yaliyotengwa huku Magari ya Manispaa yakiondoa taka hizo kwa kuzipeleka  dampo la kisasa eneo la Msimba

Aidha Mkuu huyo wa idara amesema kwa mjibu wa sheria ni wajibu watu wote kuchangia tozo za kuondoa taka Mjini na katika Makazi ya watu kutokana na kila mmoja kuwa chanzo cha uzalishaji taka,  na tozo hizo hutolewa kwa kila kaya, taasisi za Serikali na zisizo za Serikali kwa kila mwezi

Suala la kuzagaa kwa mifugo ya Mbuzi katika ya mji ni moja ya jambo ambalo limejadiliwa kwa kina ambapo imeonekana kuwa Mifugo hiyo imekuwa mingi katika  Manispaa hiyo na kuzagaa ovyo ambapo Mkuu huyo wa idara amepiga marufuku na kuwaonya wafugaji huku akisema  kwa mjibu wa sheria ni marufuku kufuga Mifugo mjini inayozagaa ovyo mtaani hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa wafugaji na Mifugo hiyo kupigwa mnada  

Mkuu huyo amehitimisha kwa kuwataka watendaji wa Kata na Mitaa kusimamia vikosi kazi hivyo vya Usafi  kwa kila mtaa huku wenyeviti wa mitaa na kamati za Usafi katika mitaa zikitakiwa kuwa hamasa kwa jamii ili kuendeleza Usafi wa mji na kuepuka na milipuko ya Magonjwa yatokanayo na uchafu

Naye Mjumbe wa kamati ya Usafi mtaa wa Uwanja wa Ndege Bi. Donatila Mzaira amepongeza kuandaliwa kwa kikao hicho kwa lengo la kujadili Usafi wa mji huku akisema yupo tayari kuihamasisha jamii kwa ajili ya kuhakikisha mji unakuwa safi na kutekeleza sheria za Usafi katika jamii inayomzunguka

Mwenyekiti wa Mtaa wa Kisangani Abdallah Kimenya amesema tayari kikosi kazi katika mtaa wake  kipo tayari kikiendelea kwa Usafi ambapo kila kaya hutoa fedha za Kitanzania kila mwezi Tsh 1000/= na hadi sasa mtaa huo umekuwa safi licha ya Changamoto za uwali za  taka kuwa nyingi mtaani  huku akiomba Ofisi ya Mkurugenzi kuongeza kizimba cha kukusanyia taka

Naye kiongozi wa dini na Mchungaji  Linus Simoni ameipongeza Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa jitihada za kuendeleza Usafi wa mji huku akisema wao kama viongozi wa dini wapo tayari kuhamasisha waumini na washirika wa imani zao ili kushiriki katika Usafi wa mji na kuhamasisha vijana na makundi mbalimbali kuchukua fursa ya kujiajiri  kupitia Ukusanyaji taka katika Manispaa hiyo

Aidha wadau hao wamekubaliana kwenda kuanza shughuli ya kukusanya taka kwa kuishirikisha jamii, taasisi za Serikali na zisizo za Serikali  ambapo vikosi kazi hivyo vya Usafi kuchukua asimilia sitini(60%) ya Makusanyo huku Ofisi ya Mkurugenzi ikibaki na asilimia arobaini (40%) ya Makusanyo hayo  na wadau hao wamepanga kukutana kwa kikao kingine cha tathimini mapema Mwezi Marchi 2021

Picha zaidi bofya http://www.kigomaujijimc.go.tz/sinlge-gallery/kikao-cha-wadau-wa-usafi-watendaji-kata-mitaa-kamati-za-usafi-mitaa-na-viongozi-wa-dini-ukumbi-wa-manispaa-ya-kigomaujiji-desemba-292020


Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa