Na Mwandishi Wetu
Wakuu wa Idara na Vitengo Manispaa ya Kigoma/Ujiji wakishirikiana na Wataalamu wa Benki ya CRDB Tawi la Kigoma Mjini wamefanya ziara ya Kutembelea na kukagua Shughuli na miradi ya vikundi vya Wajasiriamali.
Ziara hiyo ilianza Jana May 28, 2025 kwa kupita katika maeneo yao ya miradi kwa lengo la kuwapatia Ushauri wa Kitaalamu kwa miradi wanayoitekeleza na Maandalizi ya Utoaji wa Mikopo ya Wanawake, Vijana na Watu wenye ulemavu Awamu ya pili Robo ya Nne 2025.
Vikundi vya Wajasiriamali vilivyotembelewa vinajihusisha na Shughuli mbalimbali ikiwemo Usafirishaji Abiria (Bodaboda), Uuzaji wa Chakula, Ufugaji Kuku na Nguruwe, Ufumaji na Uuzaji wa Shuka,Utengenezaji wa Sabuni.
Zaidi bofya www.kigomaujijimc.go.tz
Manispaa ya Kigoma Ujiji
Sanduku la Posta: S.L.P 44
Simu: +255 28 2802535
Namba ya Simu: +255765660847
Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz
Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa