• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

WAKAZI WA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI WASEMA “ATAKAYEHARIBU BARABARA ZETU NA KUIBA TAA TUTAMTAFUTA POPOTE NA TUTAMPATA “

Posted on: January 21st, 2020

Wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji wameahidi kutowavumilia wale wote watakaokuwa waharifu wa miundombinu ya barabara iliyojengwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia chini ya mradi ya uendelezaji wa kimkakati wa miji na majiji  Tanzania (TSCP)

Wameyasema hayo katika mikutano tofautitofauti iliyofanyika na inayoendelea  katika kata zilizopitiwa na miradi hiyo ya barabara inayoendeshwa  na wataalamu kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa halmashauri hiyo juu ya uthamani, umiliki na utunzaji wa miundombinu hiyo

Akiongea katika mkutano uliofanyika jana Januari 20,  mmoja wa wananchi wa kata ya Kagera Ndugu. Emmanueli Kinyota alipongeza wafadhili wa miradi hiyo, Serikali ya awamu ya tano kwa kuidhinisha miradi hiyo kujengwa manispaa ya Kigoma/Ujiji huku akiwapongeza pia  wataalamu kwa kutoa elimu namna gani wanawanchi wataweza kutumia na kutunza miradi hiyo

“wakazi wa Kagera ni neema kwetu kwa mradi huu wa barabara na umeleta mabadiliko makubwa kwa mji wetu huu, kila siku tunapokea wageni kuja kutafuta ardhi,ni kwa mara ya kwanza daladala zinafika eneo letu hili, bajaji nazo zinafika huku, watu wanakuja kutafuta matunda kwa soko letu hilo, hivyo nasema tutapambana na watu wa kuiba taa, madereva wote wanaomwaga oili barabarani na dereva wa bodaboda wanaoburuza vyuma vyao na kupiga baruti, nasema tutawatafuta hadi uvunguni na tutawapata”

Naye Bi.Amina Mahelela alisema  “ Na sisi wanawake tutakuja kwa mtendaji kumtaarifu wale wote ambao ni waharibifu  wa barabara zetu, na tutakuwa tunawataja majina lakini na nyie mje mturudishie maji  mliyoyakata kipindi mnajenga”

Naye Afisa  Usafi na Mazingira wa Manispaa hiyo Ndg. Elishaphati Rusemvya  akitoa elimu hiyo kwa wakazi wa kata ya Kagera katika Ofsi ya Mtendaji wa Kata hiyo alisema wananchi wote wana wajibu wa kuilinda miundombinu ya barabara hiyo iliyojengwa na  kutambua barabara hizo ni miliki yao na endapo uhalibifu wowote utatokea atakayeathirika ni wananchi wanaotumia barabara hizo

Alisisitiza juu ya madereva kutumia barabara hizo kwa utaratibu ,kuendesha kwa kutoenda kwa kasi kubwa  na kutomwaga oili endapo atabainika mtu kwa mjibu wa sheria atalipa faini ya shilingi milioni moja(Tsh 1,000,000/=) lakini pia kuepuka utiririshaji wa maji machafu katika mitalo iliyojengwa na atakayebainika atalipa faini ya shilingi elfu hamsini (Tsh 50,000/=) na isiyozidi shilingi laki mbili (Tsh 200,000/=) huku  akisisitiza utunzaji wa miundombinu hiyo.

Naye Afisa Ustawi wa jamii Bi. Agnes Punjila akiwasilisha  mada katika mkutano huo alisema ujio wa barabara hizo ni maendeleo kwa wakazi wa eneo husika na katika matumizi ya miundombinu hiyo lazima tuzingatie usalama wa wanawake, watoto na wazee

Alisema “barabara hizi isiwe majanga na misiba kwa watoto wetu, jamii nzima ina wajibu wa kuwalinda watoto na kuwapa tahadhari namna ya kupita katika barabara hizi na kizuri zipo pia njia za watembea kwa miguu zimetengenezwa kando ya barabara kubwa hivyo lazima tuzingatie matumizi hayo pasipo mwingiliano lakini pia tukiangalia usalama wa wazee wetu na  madereva nawambia  muwe makini na makundi hayo”

Aliendelea kusema wanawake nao wapewe haki sawa na wanaume katika fursa zitokanazo na ujenzi wa barabara hizo kama vile kujenga mabanda ya biashara, na migahawa kando ya barabara hizo pasipo kubugudhiwa na familia zao na kuepuka ukandamizaji unaofanywa na wanaume kuwakandamiza wanawake katika kujitafutia vipato vya kuinua familia zao

Naye afisa anayeratibu Malalamiko Ndugu. Melleji  Molleli akiongea  na wananchi katika mikutano hiyo alisema  ofisi yake imepokea malalamiko ya wananchi wakilalamika kuhusu  vivuko vya barabara kubwa na vinavyoingia katika makazi ya watu, na kusema tayari mkandarasi analifanyia kazi kwa kuweka vivuko hivyo kwa kuanza na barabara ya Kagashe

Alihitimisha kwa kusema marekebisho kwa nyumba zilizoathirika umekuwa ukifanyika , na tayari wiki ijayo wataalamu kutoka ofisi ya Mkurugenzi watapita kujiridhisha athari zilizojitokeza kutokana na ujenzi wa barabara hizo kwa kata zote na watakuwa wakipiga picha nyumba zote na kulinganisha picha za awali za nyumba zilizopigwa kabla ya mradi kuanza kujengwa

Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji ni moja kati ya Miji saba (7) inayotekeleza mradi unaofadhiliwa na Benki ya Dunia(TSCP), miji hiyo ni Arusha, Tanga , Mwanza , Mbeya, Dodoma, Manispaa ya Mtwara Mikindani na Kigoma/Ujiji na barabara zinazojengwa ni barabara ya Kaaya –simu, Mwanga-kitambwe-Mwembetogwa, Kakolwa, Ujenzi-Nazarethi, barabara ya Kagashe, Barabara ya Wafipa-Kagera, Barabara ya Maweni-Burega na Barabara ya kuingia hospitali ya Mkoa ya Maweni, Ujenzi wa mfereji wa maji ya mvua ya Mlole na Katonyanga .

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa