• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

WAKULIMA NA WANANCHI KANDA YA MAGHARIBI WATAKIWA KUCHAGUA VIONGOZI WANAOFANYA SIASA ZA MAENDELEO NA WALA SIO SIASA ZA VURUGU KATIKA UCHAGUZI MKUU WA MWEZI OKTOBA, KITAIFA SIKU MBILI ZA MAONESHO YA WAKULIMA NANE NANE ZAONGEZWA, Nane nane Ceremony

Posted on: August 5th, 2020

Na mwandishi wetu

Mkuu wa Mkoa  wa Tabora Dr. Philemoni Sengati amewataka wananchi na wakulima wa kanda ya Magharibi ya maonesho ya nane nane yanayojumuisha Mkoa wa Tabora na Kigoma kuchagua viongozi bora watakaofanya siasa za maendeleo na wala sio vurugu kwa kuhakikisha uchumi wa Watanzania na Taifa unaendelea kukua

Ameyasema hayo leo Agusti  5, katika viwanja vya Fatuma Mwasa  alipokuwa akizindua maonesho  ya nane nane katika kanda ya magharibi kwa kuwataka  wakulima na  wananchi wote kufanya uchaguzi sahihi wa kiongozi aliye bora katika kuwatumikia wananchi kwa kuhakikisha wanampima kwa kumsikiliza sera za maendeleo na sio siasa za kuleta vurugu ndani ya Jamii za Watanzania

Mkuu wa Mkoa huyo amesema Kauli Mbiu ya Maonesho ya nane nane kwa mwaka huu ndio umeleta taswira chanya kuwa ili kuwaeza kuleta maendeleo katika sekta ya Kilimo, Mifugo, na Uvuvi  ni lazima wananchi wafanye uchaguzi sahihi  wa viongozi watakaowatumikia wananchi ili wasimamie maslahi ya wakulima hao na wanaojali maisha ya wanyonge walio wengi

Aidha mkuu huyo wa Mkoa amesema serikali ya awamu ya tano imejipambanua katika kuwatumikia wananchi wote hususani kuboresha mazingira ya wakulima,  wavuvi, na wafugaji  huku kwa kanda ya Magharibi Mkoa wa Kigoma 2019/2020 ukipata lita 600 kwa ajili ya dawa ya Josho kwa Mifugo na Mkoa wa Tabora ukipata lita 905 kwa mwaka , huku majosho ya kuogeshea N’gombe Mkoani Kigoma yakikarabatiwa nane(8) na Mkoa wa Tabora yakiboreshwa majosho siti ni na moja (61) kutokana na kuwa na maeneo mengi ya ufugaji katika Mkoa huo

Ameendelea kusema mikoa ya Kanda ya Magharibi inaongoza kwa kuwa na mifugo mingi ya Kienyeji huku akiwataka wakulima hao kuendelea kuboresha mifugo hiyo ili iweze kuleta tija katika uzalishaji kwa kuwatumia wataalamu waliopo ili kuweza kuhawilisha kwa kutumia mbegu Dume za kisasa huku mifugo na mimea ikilindwa dhidi ya Magonjwa wanaoshambulia kwa kufuata utaratibu wa kitaalamu pia

Aidha mkuu huyo wa Mkoa amesema  kuanzia hivi sasa wakulima wa kanda ya Magharibi watakuwa wakifatwa na maafisa Ugani katika maeneo yao ya Ufugaji, kilimo na uvuvi kwa lengo kutatua changamoto zinazowakabiri na kumrahisishia mkulima na kumpunguzia adha ili kilimo hicho kikapate kuleta tija

Mkuu huyo wa Mkoa ameendelea kutaja mafanikio ya serikali ya awamu ya Tano kwa kupunguza migogoro baina ya wafugaji na wakulima zilizokuwa zikiendelea kwa kusema serikali ya awamu ya tano imeendelea kupunguza migogoro baina ya wakulima na wafugaji kutoingiliana  katika utendaji kazi wao kwa kutenga maeneo maalumu ya kilimo na ufugaji

Akizungumza kabla ya Mkuu wa Mkoa huyo wa Tabora Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Kigoma  Ndugu Rashidi mchata amewapongeza  wakuu hao wa mikoa wapya kwa kuchaguliwa na Rais kwa lengo la kuwatumikia wananchi huku akisema Mkoa wa Kigoma kufikia mwakani wamepanga wawe wamehitimisha ujenzi wa majengo ya Maonesho ya nane nane hayo kwa Halmashauri zote kutokana na changamoto wanayomkumbana nayo ya kutokuwa na majengo ya mda na imara

Naye Mwakilishi kutoka Wizara ya Kilimo akizunguza katika mkutano huo Paul   Tarimo amewapongeza kamati ya maandalizi  kwa kuandaa maonesho hayo katika weredi Mkubwa kwa kuhakikisha miundombinu yote inayositahiri inakuwepo huku akiahidi kuwa kuna uwezekano mkubwa kitaifa Maonesho yajayo kufanyikia  Kanda hiyo ya Magharibi huku akisema maonesho hayo Kitaifa  kwa mwaka huu yatamalizika August 10 kutokana waziri wa Kilimo na Ushirika kuongeza siku mbili za maonesho

Ameendelea kusema serikali ya awamu ya Tano imesogeza huduma karibu na wakulima na wafugaji kwa kuhakikisha maafisa ugani wanapatikana katika kata mbalimbali ili kuweza kuwatukia wananchi kwa weredi na kuwasogezea wananchi huduma wanayoitaka huku akiwakumbusha wananchi wa kanda ya magharibi kuchangamkia zao la Korosho , Ufuta na Karanga kutokana na utafiti ulioonesha kuwa mazao hayo yanakubali zaidi katika ukanda huo

Naye Mwakilishi wa Wakulima wa Kanda ya Magharibi akisoma risala ameipongeza serikali ya awamu ya Tano  kwa kuwa karibu kwa wataalamu ambao wameendelea kuwa mchango mkubwa katika shughuli zao za kila siku katika kulima mazao kama vile Tumbaku, Michikichi, Kahawa, na mihogo ambayo imekuwa mazao ya mda mrefu huku wakiomba kutafutiwa Technolojia itakayowasaidia kusonga mbele zaidi katika mazo ya kimkakati ya chakula na biashara

Mkuu wa Mkoa huyo kabla ya kuhutubia wananchi alitembelea mabanda mbalimbali kwa lengo la kuona kile wakulima, wafugaji na wakulima wamekuja kukionesha huku Mkuu huyo akiridhishwa na kufurahishwa na Banda la Manispaa ya Kigoma/Ujiji lililojengwa kwa uzuri na bidhaa walizokuja kuonesha kama ukuzaji wa zao la kimkakati la Mchikichi na uchakataji wa mafuta ya Mawese , techolojia ya ufugaji wa samaki wa kula na wamapambo pamoja na kilimo cha Bustani ya Chakula aidha amonesho hayo ya nane nane kwa mwaka huu yanaenda kwa Kauli mbinu kuwa “kwa Maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi , Chagua Viongozi Bora 2020.


Picha na video zaidi ingia www.kigomaujijimc.go.tz  katika maktaba ya picha


Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa