• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

WALIMU NA WANAFUNZI KIGOMA/UJIJI WAPONGEZWA KWA KUSHIKA NAFASI YA KWANZA KIMKOA,congratulations,

Posted on: March 2nd, 2021

Na Mwandishi wetu

Baraza la Madiwani Manispaa ya Kigoma/Ujiji jana March 1, 2021 liliipongeza ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kwa kushika nafasi ya kwanza Kimkoa katika ufaulu wa wanafunzi kwa mtihani wa Kitaifa wa kuhitimu darasa la saba uliofanyika Oktoba 2020

Pongezi hizo zilitolewa na wajumbe wa baraza hilo baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Elimu na Afya na diwani wa kata ya Mwanga Kusini Mhe. Mussa Maulid kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa majukumu kwa kipindi cha robo ya pili mwezi Oktoba hadi Desemba 2020/2021


Akiwasilisha taarifa ya kamati  mwenyekiti huyo alisema wanafunzi waliofanya mtihani wa darasa la saba katika Manispaa hiyo ni wanafunzi 4922 wavulana wakiwa 2409 na wasichana wakiwa 2513 na jumla ya ufaulu ukiwa ni asilimia themanini na sita (86%) , wavulana wakiongoza kwa ufaulu wa asilimia themanini na tisa (89%) na wasichana wakiwa na ufaulu wa asilimia themanini na tatu (83%)

Mwenyekiti wa kamati hiyo aliendelea kusema katika matokeo hayo ufaulu umeongezeka kwa asilimia sifuri nukta tano tisa(0.59%) ukilinganisha na matokeo ya mtihani wa darasa la saba kwa mwaka 2019, na katika kata kumi(10) kwa Mkoa wa Kigoma zilizofanya vizuri kata tatu(03) zilitoka Manispaa ya Kigoma/Ujiji ambazo ni Kata ya Kigoma, Mwanga Kusini, na Rusimbi zikiongozwa na kata ya Makere iliyoshika nafsi ya kwanza Kimkoa  inayopatikana Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu


Alihitimisha kwa kusema tayari wanafunzi wote waliofaulu wamejiunga na elimu ya upili katika shule mbalimbali zilizopo Manispaa ya Kigoma/Ujiji na awali wanafunzi mia sita tisini na sita (696) walikosa nafasi kutokana na upungufu wa madarasa na tayari wanafunzi wote wamejiunga na masomo kutokana na kukamilika kwa ujenzi wa Vyumba vya madarasa

Meya wa Manispaa hiyo Mhe. Baraka Lupoli akizungumzia taarifa hiyo alipongeza wadau wote wa elimu na kuwashukuru walimu wote kwa jitihada walizozifanya huku akiwataka kuendelea kufanya vizuri na wanafunzi kufikia ndoto za maisha yao kutokana na elimu watakayoipata na wataalamu wa elimu kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha Manispaa kuendelea kushikilia nafasi ya kwanza  kwa kuzidi kuongeza asilimia ya ufaulu

Naye mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Mwailwa Pangani alisema serikali kupitia wadau mbalimbali inaendelea kuboresha mazingira ya Ufundishaji na Ujifunzaji kwa shule za Msingi na Sekondari na kwa mwaka huu kulikuwa na Upungufu wa vyumba vya madarasa kumi na tatu (13) kwa shule za sekondari suala lililofanya wanafunzi mia sita tisini na sita (696) kushindwa kujiunga na masomo ya upili kwa wakati  na kusema tatizo hilo limetatuliwa kwa kujenga vyumba vya madarasa na wanafunzi wote tayari wameanza masomo

Aliendelea kusema tayari madarasa kumi na sita (16) yamejengwa kupitia mradi wa EP4R na utaratibu wa  ukarabati na ujenzi wa madarasa umeanza na unatarajia kuendelea kwa shule zote huku akisema kiasi cha fedha Million ishirini ( 20,000,000/=) zimeingizwa katika akaunti ya kata ya Kagera ili kuanza ujenzi wa chumba cha darasa la kisasa kwa Shule ya Msingi Kagera

Katika Mtihani wa kuhitimu darasa la saba uliofanyika Nchini kote mwezi Oktoba,2020 Jumla ya wanafunzi elfu thelathini na tisa mia saba sitini na moja(39,761) walisajiliwa kufanya mtihani huo ikipata ufaulu wa asilimia sabini na saba (77%) na Mkoa ukishika nafasi ya ishirini(20) Kitaifa na Halmashauri zote za Mkoa huo zikiwa na Ufaulu zaidi ya asilimia Hamsini (50%) ikiwa na maana ya wanafunzi waliofaulu mtihani huo ni zaidi ya nusu ya wanafunzi wote waliofanya mtihani huo

 

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa