• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

WAMILIKI WA BAA NA KUMBI ZA STAREHE MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI WAJADILI SHERIA YA MTOTO NO 21 YA MWAKA 2009, child law

Posted on: April 9th, 2021

Na Mwandishi wetu

 Wamiliki wa baa na kumbi za starehe Manispaa ya Kigoma/Ujiji jana April 8, 2021 wakiwa katika ukumbi wa Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa hiyo  walijadili Sheria ya mtoto Namba 21 ya mwaka 2009 kwa lengo la kutokomeza vitendo vya ukatili kwa watoto chini ya umri wa miaka kumi na nane (18)

Wamiliki hao wakiwa na wadau wengine wa kupinga na kutokomeza vitendo vya ukatili walijadiliana hatua za kuchukua katika maeneo yao ili kutokomeza vitendo vya ukatili vinavyoweza kujitokeza wakiwa katika maeneo yao ya kazi

Afisa ustawi wa Jamii Manispaa ya Kigoma/Ujiji Bi. Agnes Punjila aliwataka wamiliki hao wa kumbi za starehe na baa kuwa wana wajibu wa kuwalinda watoto kwa kuhakikisha hawaonekani katika maeneo hayo baada ya saa moja jioni mara tu baada ya burudani za watoto zinapomalizika

Afisa ustawi wa jamii huyo akifafanua kifungu namba 17 cha sheria hiyo alisema mtoto yeyote haruhusiwi kuingia katika kumbi za starehe, video, na muziki  majira ya usiku na kufanya hivyo ni kinyume na sheria hiyo, huku akitoa onyo kwa wazazi na walezi wanaotembea na watoto wao maeneo hayo na kusema kuwa kufanya hivyo ni kuendeleza ukatili jambo ambalo linaweza kusababisha adhabu na kifungo cha jela  kwa wazazi hao

Aliendelea kusema kuwa mzazi ni lazima awajibike kwa kumtunza mtoto kwa kuhakikisha anampatia elimu, malazi , chakula na mtoto kuwa na furaha wakati wote  na wazazi hao waepuke kuwaagiza watoto kununua sigara, pombe, na aina yoyote ya kilevi madukani na kufanya hivo ni kukiuka sheria

Afisa dawati la Jinsia na Watoto wa jeshi la Polisi Esther Andrew aliwataka wadau hao waliohudhuria kikao kila mmoja kuwa mlinzi wa mtoto na kuitaka jamii kutoa ushirikiano mara baada ya mtuhumiwa wa vitendo vya ukatili kufikishwa mahakamani na kutoyamaliza kindugu kutokana na athari zinazoweza jitokeza

Afisa huyo alisema vitendo hivyo ni lazima viishe ili kuwa na jamii yenye maadili na kufanya kazi kwa ushiriki wa kila mmoja huku akisema kwa mwezi January hadi February 2021 mimba kumi (10) za utotoni zililipotiwa huku watu watatu (03) wakifikishwa mahakamani kwa kuhusika na vitendo hivyo

Aliendelea kusema katika kuhakikisha vitendo hivyo vya ukatili vinamalizika kila Mwana jamii ana wajibu wa kutoa taarifa za ukatili ambao utafanyika kwa mtoto na mtu yeyote ili mradi awe na ushahidi kuwa haki za mtoto zinakiukwa na wao kama jeshi la polisi wataendelea kufanya ukaguzi katika maeneo mbalimbali ili kuhakikisha haki ya mtoto inalindwa

Naye afisa utamaduni wa Manispaa hiyo Ndugu. Abdul Utimbe aliwataka wamiliki wa baa na kumbi za starehe kufanya kazi kwa mjibu wa sheria na kufuata taratibu za vibali wanavyokuwa wakipokea katika sherehe na sikukuu mbalimbali kwa kuhakikisha sherehe za watoto zinamalizika saa moja kamili jioni na kutowaruhusu watoto kuingia katika maeneo hayo majira ya usiku

Mwakilishi kutoka Ngome Urusi Ndugu. John Mlerama alisema wataendelea kupinga vitendo vya ukatili vinavyoweza kufanyika na kuhakikisha watoto hawahudhurii maeneo yenye mikusanyiko ya watu wengi majira ya usiku na hata  mda wa masomo ili kuhakikisha haki za mtoto zinalindwa na makundi mbalimbali ndani ya jamii

Kwa kipindi cha mwaka mmoja kamati ya kutokomeza ukatili kwa watoto na wanawake (MTAKUWWA) Manispaa ya Kigoma/Ujiji ilisimamia mashauri ya ukatili wa kimwili kwa watoto kumi (10), watoto waliotelekezwa na wazazi wao mia moja na arobaini na moja (141) na migogoro arobaini na saba (47) ya ndoa ilitatuliwa huku migogoro mingine ikifikishwa mahakamani

Katika kikao hicho wadau mbalimbali waliohudhuria ni wamiliki na waendeshaji wa kumbi za starehe, baa, wamiliki wa kumbi za video na mziki, ngome za mijadala mbalimbali, watendaji mitaa na kata,maafisa maendeleo, Afisa Utamaduni, Maafisa ustawi wa Jamii na Jeshi la Polisi

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa