• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

"WANANCHI WASHIRIKISHWE KATIKA MIRADI YA MAENDELEO" DC KIGOMA Comissioner

Posted on: November 2nd, 2021

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Bi. Ester Alexander Mahawe Jana Novemba 1, 2021 aliwataka Viongozi wa Serikali na Kisiasa  kuwashirikisha Wananchi katika ujenzi wa Miradi ya Maendeleo Manispaa ya Kigoma/Ujiji


Aliyasema hayo katika kikao cha kuweka mikakati na usimamizi wa ujenzi wa Madarasa arobaini na nane(48) kwa shule  za Sekondari kikihusisha Waheshimiwa Madiwani, Wakuu wa idara na Vitengo, Watendaji kata, Watendaji Mitaa, Wenyeviti Mtaa, Wakuu wa Shule na Viongozi wa bodi za Shule kilichofanyikia ukumbi wa Manispaa hiyo


Mkuu huyo wa Wilaya aliwataka viongozi hao kufanya  mikutano ya Wananchi  mara kwa mara kwa kuwajulisha miradi inayotekelezwa katika maeneo yao  ikiwa ni pamoja na kushiriki shughuli za kujitolea katika kuendeleza miradi hiyo


Alisema "Waheshimiwa Madiwani, Watendaji kata na Wenyeviti wa Mitaa mna wajibu wa kutoa taarifa ya miradi yote  inayotekelezwa na Serikali na wadau wengine wa maendeleo katika maeneo yenu ya utawala na wananchi kuwa na uelewa ikiwa ni pamoja na kuisimamia na mradi kuleta tija kwa jamii"


Aidha aliwataka Viongozi hao akiwemo Mkurugenzi na Wataalamu wake kutembelea Mara kwa Mara miradi hiyo katika kipindi chote cha ujenzi utakapokuwa ukiendelea kwa lengo la kusimamia ubora na thamani ya fedha kwa kila darasa


Awali Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Athumani Msabila akiwasilisha taarifa alisema Manispaa ya Kigoma/Ujiji imepokea kiasi cha fedha za Kitanzania Million Mia tisa tisini (960,000,000/=) kwa lengo la  ujenzi wa vyumba vya madarasa arobaini na nane (48) ikiwa ni pamoja na kupambana athari zilizotokana na Uviko-19


Aliendelea kusema fedha hizo zinatarajia kuwanufaisha wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujij kwa kutoa ajira kwa makundi mbalimbali kama vile Mafundi Ujenzi,  wafanyabiashara wa vifaa vya ujenzi, wachimbaji mawe, kokoto, Mchanga na Mama lishe watanufaika kutokana na kukua kwa mzunguko wa fedha  


Afisa Mchunguzi mwandamizi wa Takukuru Bi. Reonida Mshema alizitaka kamati za ujenzi kuwa wakweli katika manunuzi wakizingatia Sheria ya kupinga Rushwa kazini kifungu cha 15 na Kifungu 28 ikiwa ni kosa kupokea Rushwa kwa lengo la kutoa kazi na ubadhilifu wa mali za Umma


Diwani wa Kata ya Kasingirima Mhe. Abdalah Kiembe  alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha za ujenzi wa miundombinu ya elimu huku akisema Wapo tayari katika kuhamasisha wananchi kushiriki shughuli za ujenzi wa madarasa hayo na miundombinu mingine jambo ambalo baadhi wakazi wa Manispaa hiyo wamekuwa wakishiriki kwa kutoa mda na fedha(mali) zao


Picha na video zaidi unapatikana Maktaba ya Picha katika tovuti ya www.kigomaujijimc.go.tz




Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa