• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

WANASIASA NA WATAALAMU WA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI WAPOKEA MFUMO WA GIS KWA SHWANGWE, WASEMA NI MKOMBOZI WA HALMASHAURI. SYSTEM GIS

Posted on: March 11th, 2019

Na mwandishi wetu.

Wanasiasa na wataalamu wa halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji leo march 11, wamepokea mfumo wa taarifa za kijiografia(GIS) kwa furaha huku wakisema utasaidia katika uendeshaji wa halmashauri.

Wameyasema hayo katika ukumbi wa Lake Tanganyika ambapo mafunzo yamefanyika ya kuwafundisha namna mfumo huo wa GIS utakavyofanya kazi, ambapo mafunzo hayo yametolewa na wataalamu kutoka TAMISEMI chini ya mradi wa uendelezaji na ukuzaji miji kimkakati(TSCP).

Katika semina hiyo iliyohudhuliwa na wadau mbalimbali wakiwemo wanasiasa kutoka katika vyama vyao ambapo wawakilishi wametoka katika chama ACT-Wazalendo, Chama Cha Mapinduz(CCM), na CHADEMA, Madiwani lakini pia viongozi wa Masoko yaliyopo katika halmashauri na watalamu kutoka ofsi ya Mkurugenzi wakiwemo na watendaji wa kata.

Akifungua semina hiyo Meya wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Mhe. Hussein Ruhava ameshukuru TAMISEMI kwa kuamua kuanza mafunzo hayo kutolewa katika Manispaa ya Kigoma/Ujiji kati ya halmashauri 8 zinazonufaika na mradi huo wa uendelezaji na ukuzaji wa Miji kimkakati Tanzania(TSCP).

Ameendelea kusema halmashauri ina kila sababu ya kusimamia vyanzo vya mapato kupitia mfumo wa taarifa za kijiografia(GIS) kwa kuwa Manispaa inayejegwa na wakazi wa manispaa wenyewe , wanasiasa na wataalamu waliopo huku akiwataka wakazi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji wapokee mfumo huo kwa mikono miwili kutokana na faida yake.

Naye kiongozi wa msafari wa wataalamu kutoka TAMISEMI na World Bank(WB) Eng. Nanai akiongea katika semina hiyo amesema imefika hatua sasa za halmashauri kuendeshwa kisasa kutokana na mfumo wa ukusanyaji taarifa za Kijiografia(GIS).

Ameendelea kusema halmashauri itatakiwa iwe na taarifa za walipa kodi wote kwani tayari mfumo uko tayari kufanya kazi huku akiwataka wanasiasa, wataalamu na viongozi wa masoko na wafanyabiashara kuwa na nia njema na kufikisha ujumbe kwa wananchi suala hilo.

Naye mtaalamu wa mfumo wa taarifa za kijiografia kutoka TAMISEMI Bi. Grace (kwa jina moja) amesema wamekuja kwa ajili ya kuwezesha halmashauri kutumia taarifa na namna zitakavyokuwa zikichakatwa kuingizwa katika mfumo.

Ameendelea kusema ni wajibu wa kila halmashauri kuajili wataalamu wa GIS kutokana na mfumo wa utambuzi wa taarifa za watu wote wakiwemo wakazi, wafanyabiashara na shughuli zinazofanyika katika kila eneo la halmashauri kwa kuzingatia mitaa pamoja na kata zote zilizopo.

Ameendelea kusema katika mfumo huo hauna madhara kwa wananchi bali unafaida katika upatikanaji wa taarifa za kijiografia uendeshaji na usimamizi wa halmashauri maeneo ya Masoko na utambuzi wa makazi lakini pia ikienda sambamba na kupunguza gharama za uendeshaji wa halmashauri.

Naye mmoja wafanyabiashara aliyehudhulia mafunzo hayo na Mwenyekiti wa wafanyabiashara soko la Mwanga amepongeza kwa mfumo huo na kusema utaleta ufanisi katika utendaji kazi mzuri wa halmashauri kuwafikia wananchi katika kutoa huduma mbalimbali huku akiahidi wafanyabiashara kupokea mfumo huo katika hali ya uzuri.

Nao baadhi ya washiriki wa semina hiyo wakichangia mada katika semina hiyo diwani wa kata ya Kigoma mjini Mhe. Hussein Kariango na Mhe Kacheche wamepongeza TAMISEMI kwa mfumo ambao wamekuja nao kwani utaweza kukuza mapato ya halmashauri na kuondoa migogoro baina ya wafanyabiashara wa halmashauri hiyo.

Akiongea kwa niaba ya Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji mchumi wa halmashauri hiyo Ndugu. Frednandi Filimbi ameishukuru serikali kwa kuja na mfumo ambao utakuwa ni mkombozi katika uendeshaji wa halmashuri na kusema halmashauri kupitia watendaji na wataalamu wameupokea kwa mikono miwili na kuwataka wanasiasa nao kutoa ushirikiano katika maeneo yao ya utawala.

PICHA ZAIDI INGIA KATIKA MAKTABA YA PICHA.


Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa