• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

WANUFAIKA WA TASAF MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI KUJIIMARISHA KIUCHUMI KUPITIA VIKUNDI VYA WAJASIRIAMALI capacity building

Posted on: June 28th, 2022

Na Mwandishi Wetu

Viongozi wa Vikundi vya huduma ndogo za kifedha kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf) wametakiwa kuimarisha vikundi vyao ili kukidhi vigezo vya kukopeshwa mikopo ya 10% ya Wanawake, Vijana na watu wenye ukemavu inayotolewa na Halmashauri

Viongozi hao wametakiwa na Mratibu wa Mpango wa Kunusuru kaya Masikini (Tasaf) Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Izack Vyabandi Leo June 28, 2022 alipokuwa akiongea na Wenyeviti, Makatibu na Wahasibu wa vikundi hivyo katika Mafunzo ya kuhamasisha wanufaika wa Tasaf kuweka akiba na kukuza uchumi wa Kaya zao

Mratibu huyo amesema Wanachama wa vikundi hivyo elfu tano mia tatu na arobaini (5340) ambao ni wakazi wa Mitaa 49 kati ya 68 iliyopo wanatarajia kunufaika na mafunzo hayo kutoka kwa viongozi wao, Wanawake wakiwa Elfu nne mia tisa kumi na moja (4911) na Wanaume wakiwa  mia nne ishirini na tisa (429)  

Ameendelea kusema lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha vikundi vinaendelea kujiimarisha kiuchumi na kuwa na uwezo wa kujikimu kimaisha ili familia kuendelea kupata mahitaji ya Msingi  na kuwa na Miradi mbalimbali  ya kiuchumi

Aidha amewataka viongozi hao ambao vikundi vyao havijaanza  mpango wa kuweka akiba na kukopeshana kuanza ili kunufaika katika kuwekeza katika Miradi mbalimbali kwa kuzingatia katiba na Miongozo waliyojiwekea

Bi.Maimuna Ibrahimu ambaye ni Mwenyekiti wa Kikundi cha juhudi kilichopo Mtaa wa Masanga Kata ya Gungu Ndugu. Dezidel Kalisa ambaye ni   katibu wa Kikundi cha Ilakoze kilichopo Mtaa wa Gezaulole na kata ya Gungu wamesema mafunzo waliyoyapata wataenda kutoa mafunzo na maelekezo kwa wanachama wengine na kufanya vikundi hivyo vinajiimarisha kiuchumi kutokana na ruzuku ambazo wamekuwa wakiendelea kuzipata mara kwa mara  

Katika mafunzo hayo kwa viongozi wa vikundi hivyo mada mbalimbali zimewasilishwa zikiwemo umuhimu wa kikundi kuwa na katiba, Usimamizi wa mikopo,  utunzaji wa kumbukumbu, usimamizi na utatuzi wa migogoro  

Mwezi March na April, 2022 zaidi ya fedha za Kitanzania Tsh Million 500 ziliwanufaisha walengwa elfu kumi na moja mia tano thelathini na mbili (11532) ambapo zaidi ya Shilingi Milion 226 zilitolewa kwa Taslimu huku fedha zingine zikitolewa kwa njia ya Miamala ya simu na benki.




Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa