• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

WATAALAMU KUTOKA OFISI YA RAISI TAMISEMI NA BENKI YA DUNIA WATEMBELEA MIRADI INAYOTEKELEZWA MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI. guest from World Bank

Posted on: July 16th, 2019

Timu ya wataalamu kutoka benki ya dunia, ofisi ya  Rais TAMISEMI , na wataalamu kutoka jiji la Arusha jana July 16  iliwasili katika halmashauri ya manispaa ya kigoma/Ujiji kukagua miradi inayofadhiliwa na benki ya dunia (WB) chini ya mradi wa  uendelezaji wa miji  ya kimkakati Tanzania (TSCP).

Timu ya wataalamu iliwasili mapema asubuhi katika ofisi ya Mkurugenzi wa manispaa ya Kigoma/Ujiji na kufanya kikao ambapo taarifa ilisomwa namna miradi ya TSCP  ilivyotekelezwa na namna inavyotekelezwa.

Akiwasilisha taarifa ya miradi Mhandisi wa manispaa hiyo Eng. Wilfred Shimba alisema miradi ilitekelezwa  na inayoendelea kutekelezwa ni pamoja na ujenzi wa barabara, ujenzi wa mifereji inayopita katikati ya makazi ya watu, ujenzi wa dampo, zoezi la ukusanyaji wa taarifa za kijiografia (GIS), ujenzi wa mifereji wa  maji taka ndani ya manispaa hiyo.

Aliendelea kusema barabara zinazojengwa ndani ya manispaa hiyo ni nane(8) zenye urefu wa km 11.97 ambazo ni barabara ya Kaaya-Simu, barabara ya Mwanga-Kitambwe-Mwembetogwa, barabara ya Wafipa-Kagera, barabara ya Kagashe, barabara ya Kakolwa, barabara ya Nazarethi ya Nazareth-Ujenzi, barabara ya kuingia hospitali ya Maweni na barabara ya  Burega, huku akitaja mifereji iliyojengwa inayopita katika makazi ya watu ikiwa ni Km 2.35 ambapo ni mfereji wa Mlole na mfereji wa Katonyanga ambapo miradi hiyo inatekelezwa kwa fedha za kitanzania Billion 18,626,006,976.27/=

Aliendelea kutoa taarifa ya ujenzi wa mifereji ya mifumo ya maji taka ndani ya manispaa hiyo ambapo mradi huo unatarajiwa kutekelezwa ndani ya miaka ishirini kuanzia mwaka 2020-2040 ambapo shughuli zitakazotekelezwa ni pamoja na ujenzi wa maeneo ya vyanzo vya maji kuepusha mmomonyoko  wa ardhi, ukusanyaji maji taka  na kutibu maji taka hayo jambo litakalonufaisha wakazi wa manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa kuepukana na mmonyoko wa ardhi kutokana na athari za mvua na kuharibu makazi.

Aliendelea kusema mradi huo kwa sasa Manispaa hiyo imeingia mkataba na kampuni ya M/s Cheil Engineering Co. Ltd. In with DOCH Limited  ina yoandaa mpango na ramani za mabwawa na mfumo wa maji taka ambapo tayari kampuni hiyo imeanza kazi tangu may 2019, na kukamilika may 2020 kwa kiasi cha dola za kimarekani 719, 428.00.

Ameendelea kusema miradi mingine iliyotekelezwa ni ya ukusanyaji wa taarifa za kijiografia katika kata 4 zilizopo ndani ya manispaa ya kigoma/Ujiji  huku kata 15 bado hazijafanyiwa kazi ambapo ofisi ya Rais TAMISEMI inalifanyia kazi katika kutekeleza shughuli hiyo.

Naye mwakilishi  wa Benki ya dunia Eng. Nanai amepongeza ripoti iliyotolewa huku akisema mpango wa uendelezaji wa miji kimkakati Tanzania (TSCP) ifikapo may 2020 mradi  huo utafungwa kutokana na mda wake kuisha ambapo ulianza mwaka 2010 huku akisisitiza miradi inayoendelea kutekelezwa halmashauri ihakikishe inamalizika kwa wakati.

Naye Eng. Jovin Biguye kutoka Ofisi ya Rais Tamisemi akiwa katika miradi inayotekelezwa alisema zipo changamoto ambazo zinajitokeza katika miradi hiyo ikiwa ni pamoja na kukosekana kwa alama za usalama barabarani katika maeneo yanayojengwa,  na kukosekana kwa vivuko vya mda kwa wakazi katika barabara zinazojengwa jambo ambalo mhandisi na msimamizi wa mradi huo Eng. Basaya watarekebisha katika changamoto zilizojitokeza.

Naye mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Mwailwa Pangani aliwashukuru kwa kuja kutembelea miradi inayotekelezwa katika halmashauri hiyo huku akiahidi kupitia wakandarasi waliowaweka wataendelea kusimamia na kufatilia miradi hiyo ili ikamilike kwa wakati na kuweza kuleta manufaa kwa wananchi na wakazi.

         Picha zaidi ingia katika maktaba ya picha.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa