• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

WATAALAMU WA BENKI YA DUNIA WATEMBELEA MIRADI WALIYOIFADHILI MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI , WAAHIDI KUFADHILI MIRADI MINGINE, new project

Posted on: March 10th, 2020
Na Mwandishi wetu

Wataalamu kutoka Benki ya Dunia (WB) wamefanya ziara ya siku mbili katika manispaa ya kigoma/Ujiji kukagua ubora wa miradi iliyojengwa chini ya mradi wa Uenderezaji wa Miji na Majiji Tanzania(TSCP) huku wakionesha kuridhishwa na kuahidi kuleta miradi mingine katika halmashauri hiyo

Ziara hiyo ilianza jana march 10 na kukamilika leo march 11 ambapo wataalamu hao wameambatana na wataalamu kutoka TAMISEMI ,wataalamu kutoka wizara ya Fedha ,na wataalamu kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa halmashauri kama wenyeji

Wataalamu hao wametembelea barabara  nane(8) za lami zenye urefu wa Km  11.97,  dampo la msimba na mifereji ya maji ya mvua ya Katonyanga na Mlole  yenye urefu wa Km 2.32 ambapo wameridhishwa na ujenzi wa miradi hiyo

Akizungumzia ujenzi wa miradi hiyo iliyokamilika Eng. Fredrick  Nkya kutoka Benki ya Dunia amesema Mradi huo wa TSCP unatarajia kufungwa May 26, mwaka huu  kwa mikoa na halmashauri ambayo inahusika na miradi hii na kuitaka Halmashauri kusimamia maeneo ambayo hayajakamilika katika ujenzi wa barabara hizi

Amesema katika barabara zilizojengwa yapo mapungufu ambayo hayajafanyia kazi na mkandarasi aliyejenga barabara hizo anatakiwa ayakamilishe kabla ya kukabidhi barabara hizo na mda wa mradi kuisha ili kuepusha gharama kwa zinazoweza kujitokeza kwa Manispaa baadae

Amesema mambo ambayo mkandarasi hajayakamilisha katika ujenzi ni pamoja na uwekaji wa alama za barabarani, kukarabati nyumba zilizoathiriwa na mradi kipindi cha ujenzi, kufungwa kwa taa mia moja na kumi(110) ambazo ni nyongeza katika barabara hizo  na kuitaka Halmashauri kupitia Kaimu Mkurugenzi  kukamilisha upandaji wa miti ya michikichi katika barabara hizo ili kuinua na kuendeleza zao la Michikichi

Naye Mtaalamu kutoka Wizara ya Fedha Eng.Kenneth Nichie  ameipongeza halmashauri kwa usimamizi uliofanyika katika miradi iliyojengwa huku akiendelea kuwaasa wataalamu wa Halmshauri kuendelea kusimamia ubora wa kazi ukilinganisha na malipo yanayokuwa  yanafanyika kwa miradi inayojengwa

NayeMtaalamu kutoka ofisi ya Raisi Tamisemi Bi.Grace Kyaruzi amewapongeza wageni hao kutoka Benki ya dunia na kuwataka wataalamu wa Halmashauri kuendelea kusimamia na kutekeleza maelekezo yaliyotolewa ili kuweza kuleta tija kwa miradi iliyotekelezwa

Amesema “miradi yetu ya barabara tuliyoijenga hatutaki ije ilete madhara kwa wananchi bali wananchi wafurahie maendeleo yao, hivyo kwa yale yaliyoagizwa kwa Manispaa hebu myatekeleze, yale yanayohitaji kushirikiana na mamlaka zingine fanyeni hivo, shirikianeni na jeshi la polisi (trafiki) ili kuweka alama za barabarani na kuleta furaha ya matumizi ya miundombinu kwa watu wote na rika zote”

Akitoa pongezi zake Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigoma/Ujiji Ndugu. Frednand Filimbi amewapongeza wageni hao kutoka Benki ya Dunia na kuahidi kusimamia maelekezo waliyoyatoa katika ziara waliyoifanya na kusema watashirikiana na jeshi la Polisi(Trafiki) kuandaa alama za Usalama barabarani ili kuweza kuepusha ajali zinazoweza kujitokeza huku akiahidi suala la upandaji michikichi kando ya barabara hizo kufikia mwishoni mwa mwezi march upandaji huo utakuwa umekamilika

Aidha  wataalamu hao wametembelea miradi mingine nayotarajiwa kujengwa katika mradi mwingine mpya wa TACTIC unaotariwa kuanza mwezi july baada ya mradi wa TSCP utakapokuwa umefungwa mwezi may mwaka huu

Miradi hiyo mingine waliyotembelea kama rasimu ya awali ni uendelezaji wa ujenzi wa barabara ya wafipa-kagera  hadi mto Ruiche ambapo daraja  litajengwa kuunganisha eneo la Mgumile, barabara ya Ujiji-Burega –Bangwe, Barabara ya kasulu road kutoka Ujiji hadi Msimba, ujenzi wa Ukumbi  mikutano wa kisasa eneo la Mwanga Community Centre, Uendelezaji wa standi ya Malori eneo la Gungu, Ujenzi wa Machinjio ya Kisasa Ujiji na uendelezaji wa ujenzi wa mifereji ya Maji  Katonyanga na Mlole kuelekea ziwani

Katika miradi pendekezwa wamemtaka Mkurugenzi wa Manispaa hiyo kukutana na wadau mbalimbali, vyama vya kisiasa na kupokea maoni  ya  wananchi  kwa miradi mipya itakayojengwa kupitia mradi mkubwa wa TACTIC utakoanza mapema mwezi july.

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa