• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

WATOTO WA MTAANI WASAKWA USIKU NA JESHI LA POLISI MANISPAA YA KIGOMA/UJIJI, MAAFISA USTAWI WA JAMII WAWAUNGANISHA NA FAMILIA ZAO. STREET CHIRDREN

Posted on: February 15th, 2019

Maafisa ustawi wa jamii wakishirikiana na jeshi la Polisi manispaa ya Kigoma/Ujiji jana February 14, wamewaunganisha watoto kumi na sita na familia zao  baada ya msako wa usiku uliofanyika na jeshi la Polisi.

Jeshi la polisi lilifanya msako huo usiku February 13 siku ya Jumatano, mwaka huu baada ya kubaini uwepo wa watoto waishio mtaani, wanaodhurula ovyo na kutumia mda mwingi wa usiku wakiwa katika mabanda ya video na katika kamali za mashine za kichina maarufu kama Game.

watoto hao wamebanishwa kuwa na umri kati ya miaka 4 hadi miaka 15 kutoka katika maeneo ya Vamia, katubuka, mlole, uwanja wa Ndege, Ujiji na mwingine mmoja akibainishwa kutoka katika halmashuri ya Kigoma na kukabidhiwa kwa maafisa ustawi wa halmshauri hiyo.

Akieleza Afisa ustawi wa jamii wa manispaa ya Kigoma/Ujiji Bi. Saada Amani chanzo cha watoto hao kukimbilia mtaani ameeleza kuwa baadhi ya watoto ni kuwa watukutu nyumbani kwao, makundi rika na umaskini uliopo katika baadhi ya familia licha ya baadhi ya wazazi kuwapa watoto uhuru mwingi wa kujiamulia wanavyotaka kama kufika majumbani mda wa usiku bila kuonywa na wazazi wao na hatimaye watoto hao kufanya makazi mtaani huko wanapokuwa.

Aliendelea kusema watoto hao pindi wanapokuwa mtaani hujipatia ajira tofauti tofauti na wengine kutumikishwa jambo ambalo ni kinyume na sheria za kumlinda mtoto na kutoa  onyo kwa wale watu wanaofanya vitendo hivyo kuacha mara moja. 

Naye Afisa wa Jeshi la Polisi dawati la jinsia na watoto Bi. Merry (kwa jina moja) alisema zoezi hilo la kuwasaka watoto waishio mtaani litaendelea na kuhakikisha wanatokomeza watoto hao kwa kuwaunganisha na wazazi wao huku wazazi hao wakichukuliwa hatua za kufunguliwa mashataka kwa kuwatelekeza watoto wao.

Nao baadhi ya wazazi waliweza kueleza  sababu za watoto kukimbia majumbani , Mama Moses wa mtaa wa Mabatini Mwanga alisema mtoto wake anatabia ya kutoroka nyumbani kutokana na mtoto huyo kutopenda kwenda shule jambo linalompa wakati mgumu katika kumshughulikia mtoto huyo.

Naye Baba aliyekabidhiwa mtoto wake Ally miaka 13 amesema mtoto wake alitoweka nyumbani zaidi ya mwaka mmoja uliopita kutokana na makundi ya marafiki zake jambo ambalo limekuwa likimuumiza na amekuwa akimuona mara moja moja akiwa mtaani licha ya kutochukua hatua yeyote huku akisubili mtoto huyo akue akiwa mtaani na baadae kumwendeleza katika fani yeyote.

Katika nyumba ambapo wazazi na walezi wamekabidhiwa watoto maafisa hao wamewaasa kuwa watoto hao hawataweza kurudi mtaani kama amani na chakula vitakuwepo huku wakikwepa kusababisha migogoro ya familia, kufanya kazi kwa kuzalisha chakula na kukumbuka malezi bora yanayofaa baba na mama wakiwa pamoja.

Picha zaidi ingia katika maktaba ya Picha.              

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa