• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

"WAZAZI TOENI USHIRIKIANO KWA WALIMU KUKUZA TAALUMA YA KIGOMA" RC KIGOMA education

Posted on: October 10th, 2022

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Ndugu. Thobias Adengenye   amewataka Wazazi wa Mkoa huo kutoa ushirikiano kwa Walimu wa Msingi na Sekondari katika kutokomeza utoro Shuleni

Ameyasema hayo leo Octoba 10, 2022 katika kikao kazi cha wadau wa  elimu kilichofanyikia katika ukumbi wa jengo la NNSF uliopo Manispaa ya Kigoma/Ujiji kwa lengo la uzinduzi wa miongozo ya kielimu

Katika kikao kazi hicho Mkuu wa Mkoa amesema wazazi wana fursa  kubwa katika kuhakikisha Wanafunzi (watoto) wanapata elimu kwa kuwahimiza kuhudhuria masomo na kufuatilia taaluma na ufaulu wao wawapo Shuleni

Aidha amewataka Maafisa elimu kufuatilia weredi wa ufundishaji wa Walimu ili kuepukana na baadhi yao kuwa watoro wa vipindi na kutohudhuria kazini  

Akizungumza katika kikao kazi hicho Waziri wa kazi, ajira na Vijana ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kasulu Mjini Profesa Joyce Ndalichako  amewataka Viongozi na wadau wa elimu kila mmoja kwa nafasi yake kusimamia miongozo hiyo ya elimu  ili kuinua ufaulu na taaluma katika mkoa huo

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma. Benedict Mwalyambi amesema Mkoa wa Kigoma Umepokea fedha za Kitanzania zaidi ya Billion arobaini na sita (Tsh 46, 190, 000, 000/=) kwa lengo la utekelezaji wa miradi ya Maendeleo  huku zaidi ya fedha za Kitanzania Billion  saba ( Tsh 7, 160, 000,000/=) ikipokelewa kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vipya vya madarasa  kwa Shule za Sekondari

Awali akiwasilisha taarifa Katibu Msaidizi wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Wilaya ya Kigoma  Ndugu. Obadia Makoko amesema katika uboreshaji wa elimu  mkoani Kigoma ujenzi wa miundombinu  umeleta tija ya mahudhurio kwa wanafunzi  huku akiitaka Serikali kuendelea kuboresha Motisha kwa Walimu waliopo kazini,  na kuboresha suala la  Usimamizi na ufautiliaji katika masuala ya elimu kwa kuzingatia mwongozo iliyozinduliwa    

Naye mwenyekiti wa Walimu Wakuu Mkoa wa Kigoma Ndugu. Amando Amando ameipongeza Serikali kwa kuendelea kuboresha Mazingira ya Elimu mkoani humo huku akiwataka Wasimamizi wa elimu kuzingatia mgawanyo Sawa wa Walimu katika maeneo ya utendaji kazi

Katika kikao hicho miongozo iliyozinduliwa ni pamoja na  muongozo wa uteuzi wa Viongozi  wa elimu katika Mamlaka  za Serikali za Mitaa  na Mikoa ,  mwongozo wa Changamoto  katika uboreshaji wa elimu Msingi  na Sekondari na nini kifanyike,   na muongozo wa kitabu cha kuimarisha ufundishaji  na ujifunzaji katika  kwa ngazi ya  elimu msingi

Aidha kikao hicho kimehudhuriwa na Viongozi wa Sekratarieti ya Mkoa, Kamati za Ulinzi na Usalama Mkoa na Wilaya, Wakuu wa Wilaya, Waheshimiwa Wabunge , Wakurugenzi, Meya na Wenyeviti wa Halmashauri,  Wakuu wa Idara na Vitengo, Maafisa elimu Kata, na Walimu Wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa