• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua za Watumishi |
    • Malalamiko |
Kigoma Ujiji Municipal Council
Kigoma Ujiji Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa Kigoma Ujiji

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Mipango,Takwimu na Usimamizi
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Uvuvi na Ufugaji
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
    • Vitengo
      • Kitengo cha Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha nyuki
      • Kitengo cha Teknolojia Habari na Mawasiliano
  • Fursa Za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Sekta ya Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha Ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati Za Kudumu Za Halmashauri
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Ukimwi
      • Kamati Ya Maadili
      • Uchumi Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Kamati Za Madiwani
      • Ratiba Kuonana Na Meya
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyo Kamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Picha za Kuona
      • Mh.Meya
    • Tukio
    • Habari

WAZIRI MKUU ASEMA "WAKULIMA WA KIGOMA ANZENI KUPANDA MICHIKICHI YA KISASA, TAYARI TUMEANZA KUIZALISHA" Prime Minisyer

Posted on: May 23rd, 2020

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania(MB) Mhe Kasimu Majaliwa leo may 23, amewataka wakazi wa Mkoa wa Kigoma kuanza kupanda miche ya Kisasa ya michikichi kutokana na Nchi kutumia gharama kubwa kuagiza mafuta ya mawese yatokanayo na zao hilo kutoka mataifa mengine  


Ameyasema baada ya kuwasili mkoani Kigoma katika ziara yake ya Kikazi mkoani hapo, Akiwa katika kitalu cha miche ya michikichi ya Kisasa  Katosha kata ya Kibirizi Manispaa ya Kigoma/Ujiji ameipongeza halmashauri hiyo kwa jitihada za uandaaji wa kitalu hicho kwa lengo la kuwagawia wananchi michikichi hiyo bure pasipo gharama yeyote


Aidha Waziri Mkuu huyo ameendelea kusema kwa sasa Mawese yanaingia nchini kutoka Mataifa Mengine kwa fedha za kitanzania jumla ya Shilingi Billioni 445 hutumika kila mwaka kuagiza katika  Nchi ya Malaysia na Nchini Burundi jambo ambalo wananchi kuanza kulima miche hiyo itaokoa kiwango hicho cha fedha


Waziri Mkuu huyo ameendelea kusema Kwa Mkoa wa Kigoma tayari miche ya kisasa millioni 1, 800,000 tayari imezalishwa na kusema tayari kituo cha utafiti  cha zao hilo la michikichi kimeanzishwa katika mkoa huo eneo la Kihinga jambo litakalofanya kuinua  kwa zao hilo na kuleta tija na kukuza uchumi wa Mwananchi mmoja mmoja, Mkoa na Taifa kwa ujumla


Waziri Mkuu huyo amehitimisha kwa kuwakumbusha wananchi kuendelea kuchukua tahadhari ya kujikinga na Ugonjwa wa Covid-19 kwa kuhakikisha kunawa maji safi yanayotiririka,  kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima na kuvaa barakoa huku wakiendelea kufanya shughuli za uzalishaji mali    


Akiwa katika kitalu hicho alipewa taarifa naKaimu mkuu wa idara ya kilimo, Ushirika na Umwagiliaji  Manispaa ya Kigoma/Ujiji  Ndugu Haruna Mtandanyi kuwa Manispaa ya Kigoma/Ujiji ina lengo la kuzalisha miche ya michikichi ya kisasa Millioni moja (1,000,000) ambayo itagawiwa kwa wananchi bure ambapo kwa sasa mbegu elfu thelathini (30,000)zipo na miche zaidi ya elfu Kumi na saba tayari imepandikizwa katika kitalu sawa na asilimia 58.5% ya lengo la uzalishaji


Naye Meneja Sido Mkoa wa Kigoma amesema katika kuhakikisha zao la michikichi linakua na kukuza uchumi wa Mwananchi serikali imeleta mashine za kuchambua, kuchemsha na kukamua mawese na mafuta hayo kusafishwa kwa lengo la kupata mafuta yaliyo bora, ameendelea kusema tayari mashine hizo zimeanza kufungwa wilaya ya Buhigwe kijiji cha Janda ambapo  mda si mrefu kijiji cha Kinazi na Bukuba vitafungwa mashine hizo ambapo matarajio ni kupata mafuta mengi zaidi kwa wakati mfupi    


Naye Mmoja wa wakulima wa zao hilo katika bonde la mto Ruiche Mzee Mkala  ameishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuja na mkakati wa kuinua zao hilo kibiashara na kuleta tija kwa Mkulima, huku akishukuru  miche hiyo kugawiwa bure na kusema awali miche hiyo walikuwa wakinunua kwa kila mche Shilingi za Kitanzania 6000/- jambo ambalo lingeleta shida kwa wakulima katika kubadili na kuondoa miche ya zamani katika mashamba yao      


Waziri Mkuu yupo Mkoani Kigoma kwa ziara ya Siku moja kukagua uendelezaji wa zao la kimkakati mkoani hapo , baada ya kukagua kitalu cha michikichi eneo la Katosho kata ya Kibirizi kiongozi huyo anaendelea kukagua uendelezaji wa zao la michikichi Gereza la Kwitanga na kushiriki upandaji wa zao hilo na kumalizia kukagua uendelezaji wa zao hilo katika Kikosi cha Jeshi 821 Bulombora

Matangazo

  • NYARAKA ZA WAKUU WA SHULE WALIMU WAKUU October 10, 2022
  • Ufatiliaji wa Kina Kusaka wasiokata Leseni za Biashara 2017 March 20, 2017
  • Fedha za Mradi wa P4R mwezi Machi 2017 April 13, 2017
  • Fedha za Mradi wa Barabara Machi 2017 April 13, 2017
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • NYUMBA YA WALIMU SHULE YA SEKONDARI MJIMWEMA IPO HATUA YA UMALIZIAJI. Building

    May 08, 2025
  • MAANDALIZI MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU YAENDELEA UJIJI, DC AKAGUA MIRADI. National touch

    May 07, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUTOA MSAADA WA KIBINADAMU WAATHIRIKA WA MVUA KIGOMA UJIJI. Flood

    May 05, 2025
  • NMB YAKABIDHI VIFAA TIBA KIGOMA UJIJI. Health

    May 03, 2025
  • Angalia Yote

Picha za Kuona

MWENGE WA UHURU 2023
Picha za Kuona Zaidi

Kurasa za Haraka

  • Ofisi ya Rais Utumishi
  • Ofisi ya Rais Tamisemi
  • Tume ya Ajira

Kurasa Husishi

  • Wizara ya Elimu
  • Wizara ya Afya
  • TCU
  • Mikopo Vyuo Vya Elimu Ya Juu
  • Ofisi ya RAS Kigoma
  • Jiji Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Manispaa ya Kigoma Ujiji

    Sanduku la Posta: S.L.P 44

    Simu: +255 28 2802535

    Namba ya Simu: +255765660847

    Barua pepe: municipal@kigomaujijimc.go.tz ictsecurity@kigomaujijimc.go.tz

Mawasiliano Mbalimbali

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera ya Usiri
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki@2017 Manispaa ya Kigoma Ujiji. Haki Zote Zimehifadhiwa